MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Kila nikitazama kulia,kushoto,juu na Chini Lowassa ndiye Rais ajaye wa nchi hii! Nilikua Siamini hili Ila nimefanya utafiti kwa makundi ambayo zamani yalikua ni magumu sana kuamini katika upinzani na mabadiliko! Makundi haya ni ya wanawake na wazee kwa kuwauliza ni Rais gani mnafikiri atatusha kwa wakati huu?Majibu yao ni Lowassa na wengine ni CCM,Magufuli bado hawamjui! Sijui ni kwanini viongozi wa CCM hawatoi Elimu kwa wapiga kura huko vijijini?
Kilichompa Lowassa nguvu ni ule wakati wa harakati zake kutafuta wadhamini wakati yuko CCM,kwani alifika maeneo mengi nchini na kufahamika zaidi! Tatizo kwa Magufuli ni kile kitendo cha kutafuta wadhamini kimya kimya, kwani kwa sasa anapata ugumu kwa kutumia nguvu nyingi sana!Lowassa alijiwekea hazina kubwa ya wapiga utafikiri alijua kwamba atatimkia upinzani!
Faida nyingine anayoipata Lowassa ni kutojibu tuhuma anazotupiwa na mahasimu wake, Watu wengi wanamuona ni kama mtu mustaarabu asiyependa kujibizana hovyo,asiyependa malumbano! mpaka wengine kudai kwamba si kweli kwamba LOWASSA ni mtu wa visasi! Hasa kwa makundi haya ya wazee na wakinamama yakiwa kama makundi ya watu wasiopenda kelele na vurugu zozote. Hapa ndipo utakapoamini kwamba LOWASSA anaijua siasa, anajua namna watanzania walivyo na wanahitaji kitu gani kwa sasa! Sijazungumzia kundi la vijana ambalo kwa kiasi kikubwa ndio mtaji wake wa kura!
Kitu kiingine kinachomsaidia LOWASA kupaa ni kujitokeza kwa watu maarufu kutumia muda mwingi kumponda bila hata yeye kujibu na kukupuuza kelele hizo kama ile methali isemayo "kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji" Mfano kujitokeza kwa aliyekua katibu mkuu wa CHADEMA Dr Slaa kumtukana na kumponda Mh LOWASSA ni kitendo ambacho kimechukuliwa na umma kama chuki binafsi zisizokua na msingi wowote kwa mtu mzima kama yule.Dr Slaa umeonekana kama aina ya mwanasiasa mwenye ubinafsi,mwongo na Mtu mwenye visasi visivyokua na maana kwa umri wake ule.
Kujitokeza kwa vikundi vya waandamanaji vinavyoratibiwa na baadhi ya viongozi wa CCM wakivalishwa nguo za CHADEMA kijifanya kuunga mkono kauli za Dr Slaa! Mfano ni kitendo kilichofanywa na aliyekua Meya wa jiji la DSM Didas Masaburi kuwarubuni vijana wa Manispaa ya Kinondoni kuandamana mitaani kijifanya wao ni wanachadema wakiunga mkono kauli za Dr Slaa na akijinasibu kua Kikwete,Kinana na Magufuli wanajua anachokifanya. Kwa maoni ya watanzania wengi wamedai kua huu ni aina ya uchochezi unaofanywa na wanaccm ambapo huenda baadaye wakatengeneza kikundi cha uasi endapo watashindwa kwenye Uchaguzi! Kitendo hiki nacho kimeonekana kama kuishiwa Sera na hoja maana badala ya kuishawishi jamii iwaamini lakini wao wanashawishi vurugu mitaani, Hapa pia ndipo Lowassa anapopata mteremko wa aina yake kwenye ushindi kwa kupuuzia propaganda hizo.
Kilichompa Lowassa nguvu ni ule wakati wa harakati zake kutafuta wadhamini wakati yuko CCM,kwani alifika maeneo mengi nchini na kufahamika zaidi! Tatizo kwa Magufuli ni kile kitendo cha kutafuta wadhamini kimya kimya, kwani kwa sasa anapata ugumu kwa kutumia nguvu nyingi sana!Lowassa alijiwekea hazina kubwa ya wapiga utafikiri alijua kwamba atatimkia upinzani!
Faida nyingine anayoipata Lowassa ni kutojibu tuhuma anazotupiwa na mahasimu wake, Watu wengi wanamuona ni kama mtu mustaarabu asiyependa kujibizana hovyo,asiyependa malumbano! mpaka wengine kudai kwamba si kweli kwamba LOWASSA ni mtu wa visasi! Hasa kwa makundi haya ya wazee na wakinamama yakiwa kama makundi ya watu wasiopenda kelele na vurugu zozote. Hapa ndipo utakapoamini kwamba LOWASSA anaijua siasa, anajua namna watanzania walivyo na wanahitaji kitu gani kwa sasa! Sijazungumzia kundi la vijana ambalo kwa kiasi kikubwa ndio mtaji wake wa kura!
Kitu kiingine kinachomsaidia LOWASA kupaa ni kujitokeza kwa watu maarufu kutumia muda mwingi kumponda bila hata yeye kujibu na kukupuuza kelele hizo kama ile methali isemayo "kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji" Mfano kujitokeza kwa aliyekua katibu mkuu wa CHADEMA Dr Slaa kumtukana na kumponda Mh LOWASSA ni kitendo ambacho kimechukuliwa na umma kama chuki binafsi zisizokua na msingi wowote kwa mtu mzima kama yule.Dr Slaa umeonekana kama aina ya mwanasiasa mwenye ubinafsi,mwongo na Mtu mwenye visasi visivyokua na maana kwa umri wake ule.
Kujitokeza kwa vikundi vya waandamanaji vinavyoratibiwa na baadhi ya viongozi wa CCM wakivalishwa nguo za CHADEMA kijifanya kuunga mkono kauli za Dr Slaa! Mfano ni kitendo kilichofanywa na aliyekua Meya wa jiji la DSM Didas Masaburi kuwarubuni vijana wa Manispaa ya Kinondoni kuandamana mitaani kijifanya wao ni wanachadema wakiunga mkono kauli za Dr Slaa na akijinasibu kua Kikwete,Kinana na Magufuli wanajua anachokifanya. Kwa maoni ya watanzania wengi wamedai kua huu ni aina ya uchochezi unaofanywa na wanaccm ambapo huenda baadaye wakatengeneza kikundi cha uasi endapo watashindwa kwenye Uchaguzi! Kitendo hiki nacho kimeonekana kama kuishiwa Sera na hoja maana badala ya kuishawishi jamii iwaamini lakini wao wanashawishi vurugu mitaani, Hapa pia ndipo Lowassa anapopata mteremko wa aina yake kwenye ushindi kwa kupuuzia propaganda hizo.