Kumpoteza Mama

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,904
Ni moja wapo ya mambo mabaya zaidi ulimwenguni. Inatokea na kwa namna fulani tunapata nguvu ya kuendelea.

Siku zinageuka kuwa wiki, wiki zinageuka kuwa miezi, na kabla hatujajua hapa ni miaka baadaye, tukishangaa jinsi tumeweza kufikia hapa bila yeye kimwili katika maisha yetu.

Ningependa kufikiria kuwa mtu tunayempenda anapokufa mwili wake huenda lakini upendo wake unabaki. Wanaishi kupitia sisi. Kupitia mambo waliyoacha nyuma na kumbukumbu walizofanya.

Utamkumbuka mama yako kila wakati lakini kuna nyakati maishani unamkumbuka zaidi ya kawaida. Utamkumbuka unapokuwa dukani na kuona watoto wengine wakiwa na mama zao.
Utamkumbuka wakati huwezi kusahau mambo aliyokusihi ujifunze. Utamkumbuka mtu mwingine atakapompoteza mama yake. Utamkumbuka jambo kubwa likitokea na yeye ndiye mtu wa kwanza unayetaka kumpigia simu lakini unajua ukijaribu, haitakuwa sauti yake upande mwingine.

Utamkumbuka Siku ya Akina Mama wakati kila mtu anapoadhimisha mama zao na utajihisi upweke. Utamkumbuka wakati umekuwa na siku mbaya na unajua kwamba kumbatio lake pekee ndilo linaweza kukuokoa.

Mama wakati uliponiacha

moyo wangu uligawanyika vipande viwili. Upande mmoja uliojaa kumbukumbu, upande mwingine ulikufa na wewe, mara nyingi nililala macho usiku wakati ulimwengu umelala sana, na kuchukua njia ya kumbukumbu na machozi kwenye shavu langu.

KUKUKUMBUKA ni rahisi, nafanya hivyo kila siku, lakini kukukosa ni uchungu wa moyo usioisha ninakushikilia kwa nguvu ndani ya moyo wangu na hapo utabaki. Unaona maisha yameenda bila wewe, lakini hayatawahi kuwa sawa

Mama Mara milioni nimekuhitaji, mara milioni nimelia. Ikiwa upendo pekee ungeweza kukuokoa, haungekufa kamwe. Katika maisha nilikupenda sana, katika kifo bado nakupenda. Katika moyo wangu unashikilia mahali, hakuna mtu mwingine anayeweza kujaza. Ilinivunja moyo wangu kukupoteza,
lakini hukuenda peke yako. Sehemu yangu nilienda nawe, siku ambayo Mungu alikuchukua nyumbani.

MUNGU BABA NAHITAJI KIBALI

NAOMBA UNMKUMBATIE MAMA YANGU NA KUM'BUSU SHAVUNI NA KUMWAMBIA LIMETOKA KWANGU!


Ujumbe maalum kwa wote waliopoteza wazazi, lakini huu ukimzingatia mama zaidi!
Ujumbe pia kwa wale wote ambao wazazi wao bado wako hai lakini hawawajali kivile! Siku wakiondoka ndio watajua hawajui.

1de365c79400c82366633200b9949e61.jpg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah inatia uchungu mno, mama yangu alienda mapema sana nakumbuka nilikuwa youngster kichizi.

It was really unfair to me sababu pia sikuishi nae mda mrefu nakumbuka ilikuwa ni baada ya mid term ya std 3 tu. Ile likizo imekwisha tu nashangaa naambiwa jiandae na safari ya Dar usiende shule. Nafika mtaani dah nakuta watu kibao huku na huku mara bi mkubwa huyu hapa kwenye jeneza.

Moyo ulikufa ganzi mno kwa uchungu niliokuwa nao sikuweza hata kulia siku ile ila ndio siku ambayo niliona machozi ya mshua alililia sana. Tangu siku ile nilijua maisha yangu hayataweza kuwa sawa tena katika hii dunia baada ya kuona ndugu zangu wakubwa wakihuzunika na kulia kwa uchungu, mimi pekee ndio nilikuwa mziwanda kwa mama na hadi leo namkumbuka kwa upendo mkubwa aliokuwa akinionesha pamoja na ucheshi wake. Rest in Peace my mother siku moja naamini ntakuja kukuona tena.

Uchungu haukuishia hapo baada ya week mbili za kumzika mama nilimpoteza kaka yangu mwengine ambaye nae alikuwa ni kipenzi changu sana pamoja na mama yangu. Naamini alimfuata rafiki yake mama maana asingeweza kuishi bila yeye. Rip my lovely brother Yusuph alias "Makamba" maana alikufa kipindi mzee makamba akiwa ni mkuu wa mkoa wa Dar.

Mwaka 2001 utabaki kuwa na historia chungu sana kwenye maisha yangu yote hapa duniani. Uliondoka na ndugu wengi sana ninaowapenda kama pia ilivyotokea 2021.
 
Dah inatia uchungu mno, mama yangu alienda mapema sana nakumbuka nilikuwa na umri wa miaka 10 tu.

It was really unfair to me sababu pia sikuishi nae mda mrefu nakumbuka ilikuwa ni baada ya mid term ya std 3 tu. Ile likizo imekwisha tu nashangaa naambiwa jiandae na safari ya Dar usiende shule. Nafika mtaani dah nakuta watu kibao huku na huku mara bi mkubwa huyu hapa kwenye jeneza.

Moyo ulikufa ganzi mno kwa uchungu niliokuwa nao sikuweza hata kulia siku ile ila ndio siku ambayo niliona machozi ya mshua alililia sana. Tangu siku ile nilijua maisha yangu hayataweza kuwa sawa tena katika hii dunia baada ya kuona ndugu zangu wakubwa wakihuzunika na kulia kwa uchungu, mimi pekee ndio nilikuwa mziwanda kwa mama na hadi leo namkumbuka kwa upendo mkubwa aliokuwa akinionesha pamoja na ucheshi wake. Rest in Peace my mother siku moja naamini ntakuja kukuona tena.

Uchungu haukuishia hapo baada ya week mbili za kumzika mama nilimpoteza kaka yangu mwengine ambaye nae alikuwa ni kipenzi changu sana pamoja na mama yangu. Naamini alimfuata rafiki yake mama maana asingeweza kuishi bila yeye. Rip my lovely brother Yusuph alias "Makamba" maana alikufa kipindi mzee makamba akiwa ni mkuu wa mkoa wa Dar.

Mwaka 2001 utabaki kuwa na historia chungu sana kwenye maisha yangu yote hapa duniani. Uliondoka na ndugu wengi sana ninaowapenda kama pia ilivyotokea 2021.
Pole sana mkuu. Kwenye maombi yako tuombee na wenye mama ili tuwapende kadri tunavyoweza. Life hili halina maana. Mama waliokufa miaka elfu mbili iliyoyopita wako wapi leo? Watoto wao na wajukuu wao na vitukuu wao waliowapenda kwa dhati wako wapi leo? Tuombeani wote tupate rehema za Mungu.
 
Pole sana mkuu. Kwenye maombi yako tuombee na wenye mama ili tuwapende kadri tunavyoweza. Life hili halina maana. Mama waliokufa miaka elfu mbili iliyoyopita wako wapi leo? Watoto wao na wajukuu wao na vitukuu wao waliowapenda kwa dhati wako wapi leo? Tuombeani wote tupate rehema za Mungu.
Amen mkuu. Tuwaombee Rehema na huruma ya Mungu wanapoikabili afterlife.
 
Kweli sisi ni wa muhimu kwa wanetu...umri wako bado unaumia vibaya....Pole mkuu,Mungu akupiganie...ni nyakati ngumu sana ila hakuna namna....tena utashangaa hata uliyemweka ndani kashindwa kuchukua nafasi yake hata kwa asilimia 2....ndo kwanza anakuongezea machungu
 
Wazazi wote ni muhimu hasa Baba akiwa responsible one.

Kuna wakati Mzee anafariki unaona jinsi Mama anavyolia kwa uchungu kwa kuwa anajua Kazi ya kulea watoto/mtoto peke yake itakavyokuwa kubwa.

Bahati mbaya wote hawako hai.

Leo hii nimeanza kupata maokoto ya kuweza kuwajengea nyumba ama kuwakatia bima maalumu kwaajili ya Uzee wao lakini ndiyo hawapo.

Kama kuna siku ya kukutana nao huko ahera, basi lazima nitamchana Mzee ukweli kwamba alikuwa mwoga wa maisha ama nini, kwanini aniache nikiwa na miezi 10?

Bi mkuwa naye lazima nije nimwambie, kwanini aliamua kuondoka wakati nilibakiza miaka 7 aanze kuonja matunda ya jasho lake la kunisomesha na kuniangahikia kote kule.

=======

Hongereni mlio na Mama ~ Bahati Bukuku Song
 
Dah inatia uchungu mno, mama yangu alienda mapema sana nakumbuka nilikuwa na umri wa miaka 10 tu.

It was really unfair to me sababu pia sikuishi nae mda mrefu nakumbuka ilikuwa ni baada ya mid term ya std 3 tu. Ile likizo imekwisha tu nashangaa naambiwa jiandae na safari ya Dar usiende shule. Nafika mtaani dah nakuta watu kibao huku na huku mara bi mkubwa huyu hapa kwenye jeneza.

Moyo ulikufa ganzi mno kwa uchungu niliokuwa nao sikuweza hata kulia siku ile ila ndio siku ambayo niliona machozi ya mshua alililia sana. Tangu siku ile nilijua maisha yangu hayataweza kuwa sawa tena katika hii dunia baada ya kuona ndugu zangu wakubwa wakihuzunika na kulia kwa uchungu, mimi pekee ndio nilikuwa mziwanda kwa mama na hadi leo namkumbuka kwa upendo mkubwa aliokuwa akinionesha pamoja na ucheshi wake. Rest in Peace my mother siku moja naamini ntakuja kukuona tena.

Uchungu haukuishia hapo baada ya week mbili za kumzika mama nilimpoteza kaka yangu mwengine ambaye nae alikuwa ni kipenzi changu sana pamoja na mama yangu. Naamini alimfuata rafiki yake mama maana asingeweza kuishi bila yeye. Rip my lovely brother Yusuph alias "Makamba" maana alikufa kipindi mzee makamba akiwa ni mkuu wa mkoa wa Dar.

Mwaka 2001 utabaki kuwa na historia chungu sana kwenye maisha yangu yote hapa duniani. Uliondoka na ndugu wengi sana ninaowapenda kama pia ilivyotokea 2021.
Pole sana mkuu
 
Ujumbe mzuri sana, ujumbe umebeba hisia nzito sana zinazo gusa moyo kwa pendo la mama, tuongee kila kauli kwa mwanamke lakini mwanamke alikiwa kwenye engo ya mama aiseee!

Binafsi sijawa sikuonja upendo wa mama yangu ila kuna wakina mama walisimama kama mama yangu mpaka nipo hapa leo, kinacho niuma sijawahi kuiona taswira ya mama, wala mfanano wake isipo kuwa kaburi tu ndio nimeonyeshwa!

Mwenyezi Mungu awape mema yote mazuri wakina mama, Mungu awajalie pia mabinti wote wawe wakina mama wazuri ili kutoka kwao na watakao tokana nao watoe sifa zote njema kwa Mungu na kumshukuru.
Asante Mungu , Asante mama.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom