Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wajumbe wenzangu JF:
Hivi kweli CCM wataweza kumaliza ufisadi hapa nchini? Inakuwaje tuhuma za ufisadi zachunguzwa na kumalizwa na vikao vya CCM badala ya vyombo rasmi vya sheria?
Someni hii:
*************
CCM yamsafisha kada wake kwa ufisadi
Na Debora Sanja, Dodoma
KAMATI ya watu watatu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za ufisadi zilizomkabili Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Kapteni John Barongo imebaini kutokuwepo kwa ufisadi wowote uliofanywa na katibu huyo.
Akisoma taarifa ya kamati hiyo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma William Kusila alisema kamati imeshamaliza kazi yake na kuwa hakuna ufisadi.
Kwa mujibu wa Kusila, kamati hiyo iliyoundwa kuchunguza tuhuma hizo wajumbe wake walikuwa ni Haidery Gulamali, Peter Mavunde na Wales Lusingu ambao wote ni wajumbe wa kamati ya siasa ya Chama ya Mkoa.
Alisema kamati hiyo ilipewa muda wa wiki mbili kukamilisha kazi yake na kutoa taarifa yake kwa kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa.
"Kamati imebaini kuwa madai hayo yaliyotolewa na katibu mwenezi wa CCM Mkoa wa Dodoma Donald Mejetii hayana ukweli wote kwa kuwa hakuna wizi wa fedha uliofanywa na Katibu"
Kutokana na taarifa hiyo ya kamati uongozi wa ngazi ya juu kimkoa inafanya taratibu ili kikao maalumu cha kamati ya siasa kiweze kuona adhabu ya kuumpa Mejitii." alisema Barongo.
Awali katika tuhuma alizozitoa Mejetii alidai katibu huyo wa Mkoa amekula fedha za mradi wa ujenzi wa Jengo la Hosteli ya chama zaidi ya sh. milioni 373.
Pamoja na tuhuma hizo pia alidai katibu Barongo alikodisha gari ya Chama kwa Manispaa ya Dodoma ili liweze kusambaza mitihani ya darasa la saba mwaka jana kwa gharama ya sh, milioni tisa na kula fedha hizo.
Aidha, alidai pia jumla ya Sh milioni nne zililiwa na katibu huyo kutoka Manispaa ya Dodoma ikiwa ni fedha za matengenezo ya gari hilo kabla ya kuchukuliwa kufanya kazi hiyo.
Kusila alisema mara baada ya kupata tuhuma hizo ndipo ilipoundwa kamati maalumu kuchunguza madai hayo.
Mwisho.
Chanzo: MtanzaniaA
Hivi kweli CCM wataweza kumaliza ufisadi hapa nchini? Inakuwaje tuhuma za ufisadi zachunguzwa na kumalizwa na vikao vya CCM badala ya vyombo rasmi vya sheria?
Someni hii:
*************
CCM yamsafisha kada wake kwa ufisadi
Na Debora Sanja, Dodoma
KAMATI ya watu watatu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za ufisadi zilizomkabili Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Kapteni John Barongo imebaini kutokuwepo kwa ufisadi wowote uliofanywa na katibu huyo.
Akisoma taarifa ya kamati hiyo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma William Kusila alisema kamati imeshamaliza kazi yake na kuwa hakuna ufisadi.
Kwa mujibu wa Kusila, kamati hiyo iliyoundwa kuchunguza tuhuma hizo wajumbe wake walikuwa ni Haidery Gulamali, Peter Mavunde na Wales Lusingu ambao wote ni wajumbe wa kamati ya siasa ya Chama ya Mkoa.
Alisema kamati hiyo ilipewa muda wa wiki mbili kukamilisha kazi yake na kutoa taarifa yake kwa kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa.
"Kamati imebaini kuwa madai hayo yaliyotolewa na katibu mwenezi wa CCM Mkoa wa Dodoma Donald Mejetii hayana ukweli wote kwa kuwa hakuna wizi wa fedha uliofanywa na Katibu"
Kutokana na taarifa hiyo ya kamati uongozi wa ngazi ya juu kimkoa inafanya taratibu ili kikao maalumu cha kamati ya siasa kiweze kuona adhabu ya kuumpa Mejitii." alisema Barongo.
Awali katika tuhuma alizozitoa Mejetii alidai katibu huyo wa Mkoa amekula fedha za mradi wa ujenzi wa Jengo la Hosteli ya chama zaidi ya sh. milioni 373.
Pamoja na tuhuma hizo pia alidai katibu Barongo alikodisha gari ya Chama kwa Manispaa ya Dodoma ili liweze kusambaza mitihani ya darasa la saba mwaka jana kwa gharama ya sh, milioni tisa na kula fedha hizo.
Aidha, alidai pia jumla ya Sh milioni nne zililiwa na katibu huyo kutoka Manispaa ya Dodoma ikiwa ni fedha za matengenezo ya gari hilo kabla ya kuchukuliwa kufanya kazi hiyo.
Kusila alisema mara baada ya kupata tuhuma hizo ndipo ilipoundwa kamati maalumu kuchunguza madai hayo.
Mwisho.
Chanzo: MtanzaniaA