Kumbe JK alikuwa anampinga Lowassa kimya kimya?

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Date::7/11/2009

Kikwete apinga hoteli kujengwa mbugani

Na Peter Edson

RAIS Jakaya Kikwete amepinga hoja ya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowasa aliyoitoa bngeni enzi za uongozi wake ya kutaka zijengwe hotel nyingi maeneo ya hifadhi za taifa.

Badala yake Rais Kikwete ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha kuwa inadhibiti ujenzi holela wa hoteli katika maeneo ya mbuga za wanyama.

Akizungumza wakaki wa uzinduzi wa hoteli ya kitalii ya Bilila Kempinsk yenye hadhi ya nyota tano katika mbuga ya wanyama ya Serengeti, Rais Kikwete alisema kama kutakuwepo na ujenzi holela wa hotel katika mbuga baadaye kunaweza kuleta athari kwa wanyama.

“Tunahitaji hoteli nzuri za kitalii zenye sifa na siyo kila mtu aje mbugani kujenga hoteli. Haitaleta maana yeyote, hivyo nawagiza ninyi Tanapa (Shirika la Hifadhi la Taifa) na wizara husika kusimamia vyema jambo hili,” alisema Kikwete.


Mwaka 2007, Lowasa aliwahi kulieleza bunge kuwa serikali inakusudia kuanza kujenga hotel kwa wingi katika maeneo ya mbuhgani kwa lengo la kuvutia watalii kutokana na ukosefu wa hoteli zenye hadhi nchini.


Alisema sekta ya utalii ni eneo muhimu katika ukuaji wa uchumi hapa nchini kwani katika kipindi cha mwaka 2007/2008 sekta hiyo iliweza kuchangia pato la taifa kwa asilimia 17.2 na kuingiza fedha za kigeni kwa asilimia 25, jambo ambalo halikuwahi kutokea huko nyuma.

Alisema kukamilika kwa hotel hiyo ni sehemu ya kutangaza utalii katika mbuga ya Serengeti nje ya nchi, hivyo ni vema wamiliki na wafanyakazi katika hotel hiyo wakafanya kazi kwa uaminifu ili kuvutia zaidi wawekezaji.

“Tutapokea watalii wengi katika hoteli hii, lakini hata sisi tumepata ajira kutokana na kukamilika kwa hoteli hii, msiiharibu, ipendeni ili nayo iendelee kuwalea,” alisema Rais Kikwete.
Alisema hivi sasa Serikali ipo katika mchakato wa kupunguza kiwango cha malipo kwa hati ya kusafiria kwa watalii kutoka asilimia 100 hadi kufikia 50 kwa mtalii mmoja, lengo likiwa ni kuondoa vikwanzo vinavyosababisha kupungua kwa watalii nchini hasa katika kipuindi hiki cha kuyumba kwa uchumi duniani.


Mwananchi Tanzania Newspaper(MCL)
 
Last edited by a moderator:
Date::7/11/2009Kikwete apinga hoteli kujengwa mbugani

Na Peter Edson

RAIS Jakaya Kikwete amepinga hoja ya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowasa aliyoitoa bngeni enzi za uongozi wake ya kutaka zijengwe hotel nyingi maeneo ya hifadhi za taifa.

Badala yake Rais Kikwete ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha kuwa inadhibiti ujenzi holela wa hoteli katika maeneo ya mbuga za wanyama.

Akizungumza wakaki wa uzinduzi wa hoteli ya kitalii ya Bilila Kempinsk yenye hadhi ya nyota tano katika mbuga ya wanyama ya Serengeti, Rais Kikwete alisema kama kutakuwepo na ujenzi holela wa hotel katika mbuga baadaye kunaweza kuleta athari kwa wanyama.

"Tunahitaji hoteli nzuri za kitalii zenye sifa na siyo kila mtu aje mbugani kujenga hoteli. Haitaleta maana yeyote, hivyo nawagiza ninyi Tanapa (Shirika la Hifadhi la Taifa) na wizara husika kusimamia vyema jambo hili," alisema Kikwete.


Mwaka 2007, Lowasa aliwahi kulieleza bunge kuwa serikali inakusudia kuanza kujenga hotel kwa wingi katika maeneo ya mbuhgani kwa lengo la kuvutia watalii kutokana na ukosefu wa hoteli zenye hadhi nchini.


Alisema sekta ya utalii ni eneo muhimu katika ukuaji wa uchumi hapa nchini kwani katika kipindi cha mwaka 2007/2008 sekta hiyo iliweza kuchangia pato la taifa kwa asilimia 17.2 na kuingiza fedha za kigeni kwa asilimia 25, jambo ambalo halikuwahi kutokea huko nyuma.

Alisema kukamilika kwa hotel hiyo ni sehemu ya kutangaza utalii katika mbuga ya Serengeti nje ya nchi, hivyo ni vema wamiliki na wafanyakazi katika hotel hiyo wakafanya kazi kwa uaminifu ili kuvutia zaidi wawekezaji.

"Tutapokea watalii wengi katika hoteli hii, lakini hata sisi tumepata ajira kutokana na kukamilika kwa hoteli hii, msiiharibu, ipendeni ili nayo iendelee kuwalea," alisema Rais Kikwete.
Alisema hivi sasa Serikali ipo katika mchakato wa kupunguza kiwango cha malipo kwa hati ya kusafiria kwa watalii kutoka asilimia 100 hadi kufikia 50 kwa mtalii mmoja, lengo likiwa ni kuondoa vikwanzo vinavyosababisha kupungua kwa watalii nchini hasa katika kipuindi hiki cha kuyumba kwa uchumi duniani.
Hapo nadhani namna mwandishi alivyoiframe tu. Suala la ujenzi wa hoteli lilikuwa na upinzani muda mrefu hata huyo JK naye ametaka utafiti ufanyike kabla ya ujenzi. Kwahiyo hiyo ni stahili ya uandishi wetu
 
Last edited by a moderator:
Lakini upinzani wa wakati JK alikuwa kimya kama Rais mbona hakusema lolote hadi sasa anapo enda kuifungua hii , ambayo inasemekana ana mkono wake na labda tajiri kasema hakuna hotels zaidi ili kumpa nafasi kuwa bingwa mbugani , na mshindani pekee ndipo kauli zinatoka ?Bado nadhani kuna sense ndani yake maana JK daima huwa hasemi kwa uwazi .
 
Ni mbinu za kuzuia competition tu na faida binafsi. Si porini si mjini mbona Mengi walimnyima Kilimanjaro? It is a chain and if you connect dots utajua nini kinawendelea.
 
Ni mbinu za kuzuia competition tu na faida binafsi. Si porini si mjini mbona Mengi walimnyima Kilimanjaro? It is a chain and if you connect dots utajua nini kinawendelea.

I buy your story 220% but again why go public against mshikaji wake ? Si kwamba pia ni kampeni hizi na kuwapoza wadanyika kwamba Jamaa anajali ?
 
I buy your story 220% but again why go public against mshikaji wake ? Si kwamba pia ni kampeni hizi na kuwapoza wadanyika kwamba Jamaa anajali ?


....hiii ndio ile hoteli tuliyosemaga hapa kuwa bwana mkubwa ana ubia ...serengeti...!!

conflicts of interest hapo...mzee hiyo kuzuia hotel kujengwa mbugani ameona leo...
 
....hiii ndio ile hoteli tuliyosemaga hapa kuwa bwana mkubwa ana ubia ...serengeti...!!

conflicts of interest hapo...mzee hiyo kuzuia hotel kujengwa mbugani ameona leo...


Hotel ya Bilila Kempinsk imeshajengwa na sasa anazuia nyingine kujengwa ili kuipa Hotel hii impya ambayo tetesi zinasema ana ubia nayo isipate ushindani.
 
anapinga kujengwa hoteli Serengeti wakati akifungua hoteli iliyojengwa humo? Je zikitaka kujengwa hoteli kama za ubora wa hiyo aliyoifungua atakuwa na matatizo nayo?
 
Ni mbinu za kuzuia competition tu na faida binafsi. Si porini si mjini mbona Mengi walimnyima Kilimanjaro? It is a chain and if you connect dots utajua nini kinawendelea.
Mengi alishindwa kushindana si kwamba alinyimwa. Yapo mahoteli mengine huko, sidhani kama njia hiyo inatosha kuzuia competition
 
anapinga kujengwa hoteli Serengeti wakati akifungua hoteli iliyojengwa humo? Je zikitaka kujengwa hoteli kama za ubora wa hiyo aliyoifungua atakuwa na matatizo nayo?
Mzee Mwanakijiji mwanzo nilikuona kama mtu mwenye busara lakini sasa naanza kupata mashaka kidogo kwamba ndiye mwanakijiji huyu huyu aliyekuwa anatuletea hadithi za kuvutia au mwingine. Katika hali ya kawaida kwa binadamu yeyote mwenye busara hivi tunahitaji kweli kuwa na Hotel nyingi katika mbuga za kuhifadhi wanyama? Mimi sidhani JK kwa kusema hivyo alikuwa anafanya makosa.
 
Mzee Mwanakijiji mwanzo nilikuona kama mtu mwenye busara lakini sasa naanza kupata mashaka kidogo kwamba ndiye mwanakijiji huyu huyu aliyekuwa anatuletea hadithi za kuvutia au mwingine. Katika hali ya kawaida kwa binadamu yeyote mwenye busara hivi tunahitaji kweli kuwa na Hotel nyingi katika mbuga za kuhifadhi wanyama? Mimi sidhani JK kwa kusema hivyo alikuwa anafanya makosa.


JK hafanyi makosa haya leo lakini wakati kaingia madarakani na mshikaji wake Lowasa ndiyo walio komaa na ujenzi wa mahoteli na uwanja wa ndege .Haya hakuyaona ama kaona baada ya Hotel yake kuisha ? Now Mwanakijiji hapa kakosa busara wapi ? Soma tena bandiko lake na utajua kwamba kaweka alama ya kuuliza na hajasema watu wakajenge huko hoteli .
 
Mkuu,
Tutegemee nini kutoka kwako pale unapotaka kulazimisha hoja juu ya JK dhidi ya Lowasa?
Kauli ya JK haipingani kwa namna yeyote na hiyo kauli ya Lowasa.
Lowasa amesema zijengwe hoteli nyingi na JK amesisitiza zisijengwe kiholela ni lazima ziwe na ubora wa hali juu zitazovutia watalii. Kwa maana hiyo basi hata zikijengwa 1000 lakini zikiwa nzuri kama Bilila, RUXAAA!!!!!
 
Ipole,
Ni lini mheshimiwa rais alipotambua kwamba kuna hatari ya kujenga hoteli nyingi katika mbuga za wanyama? Baada ya hoteli ya rafiki yake kumalizika? Na kwa nini?
 
JK amekuwa na maono ya mbali. Hakunahaja ya kujengwa kwa hoteli nyingi mbugani mfano wa hiyo aliyoifungua, ni vema ukabuniwa utaratibu wa kuwa na hoteli za mfuto ambazo si kama zao huku marekani na ulaya. wenzetu wanataka vitu tofauti. kuwajengea mahoteli kama yaliyoko kwao si kuwavutia bali kuwfukuza
 
Ipole,
Nadhani Mwanakijiji alichosema ni kwamba kama JK alikuwa akipinga iweje yeye alikwenda kufungua Hotel iliyopo ktk mbuga hizo hizo..Kama imewezekana moja itashindikana vipi kufunguliwa ya pili au tatu zenye ubora kama huo au zaidi..
 
Wandugu kwenye siasa au ungwini hakuna aliye sahihi na ambaye si sahihi, kilichopo ni kujenga hoja na kuitetea hoja.

Kikwete amewahi kutofautiana kikauli na Lowassa mara nyingi, mojawapo ikiwa ni ile ya "Mamilioni ya Jakaya". Lowassa alitaka watendaji wa Benki wasilete urasimu wa kutoa fedha zile, na Kikwete akasema Fedha zile ni Mikopo, na taratibu zote za kibenki za kugawa mikopo nafuu zifuatwe, na hakuna kugawa fedha kiholela holela. Ni hoja tu, na jinsi mtu anapoweza kuzijenga na kukubalika.

Na wakati mwingine mwenye kisu kikali ndiye mla nyama, na JK ana kisu cha Urais, na mara nyingi yeye husema mwishoni.
 
Wandugu kwenye siasa au ungwini hakuna aliye sahihi na ambaye si sahihi, kilichopo ni kujenga hoja na kuitetea hoja.

Kikwete amewahi kutofautiana kikauli na Lowassa mara nyingi, mojawapo ikiwa ni ile ya "Mamilioni ya Jakaya". Lowassa alitaka watendaji wa Benki wasilete urasimu wa kutoa fedha zile, na Kikwete akasema Fedha zile ni Mikopo, na taratibu zote za kibenki za kugawa mikopo nafuu zifuatwe, na hakuna kugawa fedha kiholela holela. Ni hoja tu, na jinsi mtu anapoweza kuzijenga na kukubalika.

Na wakati mwingine mwenye kisu kikali ndiye mla nyama, na JK ana kisu cha Urais, na mara nyingi yeye husema mwishoni.
Sawa mkuu, lakini matokeo ya hizo mabillioni ya Kikwete mbona ziligawawiwa kiholela!
Alichopinga mwanzo na kikatendeka kile kile alichopinga ndio kupinga gani huko, wakati mwenye last say ni yeye sii Lowassa..
 
Binafsi sioni kama JK anapingana na aliyosema Lowassa. Kwanza Lowassa alisema mwaka 2007 ambao ni muda mrefu na huenda tayari hotel zinaanza kuwa nyingi kiasi cha JK kuona kuna haja ya kufanya control.

Mwandishi kaongeza chumvi labda ili kuuza magazeti lakini sioni hii habari inaendana na kichwa cha habari, naona mwandishi ana create a storm in a tea cup.
 
Wakuu tatizo la Tanzania si nani kasema nini lini na wapi. Cha msingi ni nani kafanya nini lini na wapi. Maneno ya hawa woooote JK na genge lake yamekuwa na utata mara nyingi sana. Kitakachosemwa kinaweza kumaanisha kitu kingine kabisa au ni mtego wa kumyaka ngedere mwingine aliye mbali!!!
 
Back
Top Bottom