Kulingana na ushahidi wa kesi ndogo ndani ya kesi kubwa uliotolewa, Je unadhani maelezo ya Adamoo aliyoandikisha polisi yatapokelewa kama ushahidi..?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
Wengi tunahudhuria mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu .

Wengine tunafuatilia mitandaoni hatua kwa hatua mwenendo wa kesi nzima....

Kwa ambao hawajui au hawakumbuki au kusahau ni kuwa, kinachoendelea sasa ni kesi ndogo ndani ya kesi kubwa (trial within a trial)...

Kinachobishaniwa ni aidha maelezo ya mshitakiwa wa 1 Adamoo na wenzake waliyoyatoa polisi yapokelewe au yasipokelewe kama kielelezo cha ushahidi upande wa mashitaka...

UPANDE WA MASHITAKA, unadai yapokelewe kwa sababu yalichukuliwa kwa utaratibu wa kawaida kwa mujibu wa sheria na PGO na watuhumiwa kusaini wenyewe kwa hiari yao...

UPANDE WA UTETEZI NA WASHITAKIWA WENYEWE, unapinga yasipokelewe kwa sababu unadai maelezo hayo yalichukuliwa kinyume cha sheria (chini ya shinikizo la mateso makubwa kwa watuhumiwa) kama njia ya kuwalazimisha kukubali na kusaini maelezo ambayo hawajui yameandikwa na nani...!!

Hii ndiyo sababu upande wa mashitaka waliwekewa "OBJECTION" na washitakiwa (utetezi) katika hili na kuzaa kesi ndogo ndani ya kesi kubwa na ndiyo inayosikilizwa sasa...

Ni katika hatua hii ya kesi hii ishu ya PGO imezuka kwa namna ya kipekee sana na watu kujua kumbe polisi wanapaswa kutekeleza wajibu wao wa kipolisi wa kila siku ikiwemo kukamata na kuhoji watuhumiwa, kuwasafirisha kutoka eneo moja kwenda jingine nk nk kwa mujibu wa PGO...!!

Kwa vyovyote vile itakavyokuwa, maamuzi yoyote ya kesi hii ndogo ndiyo yàtakayotoa uelekeo wa kesi kubwa ambayo huko mbele tutamkuta kinara anayelengwa kuangamizwa au kufungwa (mshtakiwa namba 4, yaani Mh. Freeman A. Mbowe)...

MASWALI YA KUTUONGOZA KATIKA MJADALA HUU NI HAYA;

1. Je, mpaka hatua hii kwa wote mnaofuatilia kesi hii, na kwa mtazamo wa kila mmoja based on the evidence uliokwisha kutolewa, unadhani objection ya upande wa utetezi itatoboa....?

2. Kwa maelezo ya mshtakiwa namba 1 na 2 ambao pia ndiyo mashahidi wenyewe wa kesi hii ndogo, unadhani wameweza kuishawishi mahakama kuwa ni kweli waliteswa kama njia ya kuwalazimisha kukubali maelezo waliyoyatoa polisi chini ya kiapo cha "onyo?"...

3. Ili kuthibitisha kuwa mtu fulani aliteswa, ukiachilia mbali maelezo ya mdomo kuwa nilipigwa sana na kufanyiwa hivi au vile, ushahidi mkubwa huwa ni alama za makovu ya vidonda katika mwili...

Je, mashahidi walionesha alama zozote zinazoashiria tendo la kupigwa na kuteswa lilitendeka kweli....?

Alamsiki. Karibuni kwa mjadala...
 
Wengi tunahudhuria mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu .

Wengine tunafuatilia mitandaoni hatua kwa hatua mwenendo wa kesi nzima....

Kwa ambao hawajui au hawakumbuki au kusahau ni kuwa, kinachoendelea sasa ni kesi ndogo ndani ya kesi kubwa (trial within a trial)...

Kinachobishaniwa ni aidha maelezo ya mshitakiwa wa 1 Adamoo na wenzake waliyoyatoa polisi yapokelewe au yasipokelewe kama kielelezo cha ushahidi upande wa mashitaka...

UPANDE WA MASHITAKA, unadai yapokelewe kwa sababu yalichukuliwa kwa utaratibu wa kawaida kwa mujibu wa sheria na PGO na watuhumiwa kusaini wenyewe kwa hiari yao...

UPANDE WA UTETEZI NA WASHITAKIWA WENYEWE, unapinga yasipokelewe kwa sababu unadai maelezo hayo yalichukuliwa kinyume cha sheria (chini ya shinikizo la mateso makubwa kwa watuhumiwa) kama njia ya kuwalazimisha kukubali na kusaini maelezo ambayo hawajui yameandikwa na nani...!!

Hii ndiyo sababu upande wa mashitaka waliwekewa "OBJECTION" na washitakiwa (utetezi) katika hili na kuzaa kesi ndogo ndani ya kesi kubwa na ndiyo inayosikilizwa sasa...

Ni katika hatua hii ya kesi hii ishu ya PGO imezuka kwa namna ya kipekee sana na watu kujua kumbe polisi wanapaswa kutekeleza wajibu wao wa kipolisi wa kila siku ikiwemo kukamata na kuhoji watuhumiwa, kuwasafirisha kutoka eneo moja kwenda jingine nk nk kwa mujibu wa PGO...!!

Kwa vyovyote vile itakavyokuwa, maamuzi yoyote ya kesi hii ndogo ndiyo yàtakayotoa uelekeo wa kesi kubwa ambayo huko mbele tutamkuta kinara anayelengwa kuangamizwa au kufungwa (mshtakiwa namba 4, yaani Mh. Freeman A. Mbowe)...

MASWALI YA KUTUONGOZA KATIKA MJADALA HUU NI HAYA;

1. Je, mpaka hatua hii kwa wote mnaofuatilia kesi hii, na kwa mtazamo wa kila mmoja based on the evidence uliokwisha kutolewa, unadhani objection ya upande wa utetezi itatoboa....?

2. Kwa maelezo ya mshtakiwa namba 1 na 2 ambao pia ndiyo mashahidi wenyewe wa kesi hii ndogo, unadhani wameweza kuishawishi mahakama kuwa ni kweli waliteswa kama njia ya kuwalazimisha kukubali maelezo waliyoyatoa polisi chini ya kiapo cha "onyo?"...

3. Ili kuthibitisha kuwa mtu fulani aliteswa, ukiachilia mbali maelezo ya mdomo kuwa nilipigwa sana na kufanyiwa hivi au vile, ushahidi mkubwa huwa ni alama za makovu ya vidonda katika mwili...

Je, mashahidi walionesha alama zozote zinazoashiria tendo la kupigwa na kuteswa lilitendeka kweli....?

Alamsiki. Karibuni kwa mjadala...
Mzee Kuna mateso mengine huwa hayaachi alama nje ya mwili, na pia kwa muda waliokaa jela kama Ni uvimbe ushapungua
 
Sijui kwa nini judge asisimamishe hii kesi maana Mpaka sasa tayari amekwisha sikia mengi ya kumfanya aamue...ya nini kuendelea kuwahoji mashahidi wengine waliobaki ili hali waliobaki wote watakuja kusema au ku collaborate yote ya ushahidi wa utetezi? Sioni kama kuna haja ya kuendelea maana amekwisha sikia mengi tayari Mpaka sasa na anaweza kutoa maamuzi kwa yale yote aliyoyasikia...

serikali wamefunga ushahidi tayari... au labda ni kuwaruhusu waendelee ili mawakili waendelee kula fedha za umma tu kama akina kingai na Mahita?

Au labda ni kuwaruhusu cdm waendelee tu kusema halafu judge aseme ushahidi unapokelewa halafu kesi kubwa ya Msingi inaendelea na tayari mashahidi wa chadema wanakuwa wameisha na hakuna jipya?

Je kamanda Sirro ataitwa katika hii kesi ndogo au ni katika kesi kubwa tu? Nasikia huwa anatuma wawakilishi tu - MaRPC wamuwakilishe, sijui hii itakuwaje Sirro akitaka hivyo?

Kesi yote Mpaka sasa ni ya kupoteza muda tu na kuwasumbua watuhumiwa... ikiisha tu, moto wa katiba mpya utarudi na hapo ndio utakuwa mwanzo wa vurugu kati ya JWTZ, polisi na wananchi... subiri tu... ndio hayo yanakuja kutokea, hata wakifungwa, ni hayo hayo maana JWTZ wamedharirishwa vibaya sana na hawa polisi uchwara wasio jua hata miongozo yao ya kazi...

Issue Kubwa kwa judge Kuamua ni je kutokufuata miongozo ya kazi kunaifanya hiyo kazi kuwa batili? Ni Hilo tu ndilo linalotakiwa kuamuliwa mengine yote ni Isidingo...
 
Wengi tunahudhuria mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu .

Wengine tunafuatilia mitandaoni hatua kwa hatua mwenendo wa kesi nzima....

Kwa ambao hawajui au hawakumbuki au kusahau ni kuwa, kinachoendelea sasa ni kesi ndogo ndani ya kesi kubwa (trial within a trial)...

Kinachobishaniwa ni aidha maelezo ya mshitakiwa wa 1 Adamoo na wenzake waliyoyatoa polisi yapokelewe au yasipokelewe kama kielelezo cha ushahidi upande wa mashitaka...

UPANDE WA MASHITAKA, unadai yapokelewe kwa sababu yalichukuliwa kwa utaratibu wa kawaida kwa mujibu wa sheria na PGO na watuhumiwa kusaini wenyewe kwa hiari yao...

UPANDE WA UTETEZI NA WASHITAKIWA WENYEWE, unapinga yasipokelewe kwa sababu unadai maelezo hayo yalichukuliwa kinyume cha sheria (chini ya shinikizo la mateso makubwa kwa watuhumiwa) kama njia ya kuwalazimisha kukubali na kusaini maelezo ambayo hawajui yameandikwa na nani...!!

Hii ndiyo sababu upande wa mashitaka waliwekewa "OBJECTION" na washitakiwa (utetezi) katika hili na kuzaa kesi ndogo ndani ya kesi kubwa na ndiyo inayosikilizwa sasa...

Ni katika hatua hii ya kesi hii ishu ya PGO imezuka kwa namna ya kipekee sana na watu kujua kumbe polisi wanapaswa kutekeleza wajibu wao wa kipolisi wa kila siku ikiwemo kukamata na kuhoji watuhumiwa, kuwasafirisha kutoka eneo moja kwenda jingine nk nk kwa mujibu wa PGO...!!

Kwa vyovyote vile itakavyokuwa, maamuzi yoyote ya kesi hii ndogo ndiyo yàtakayotoa uelekeo wa kesi kubwa ambayo huko mbele tutamkuta kinara anayelengwa kuangamizwa au kufungwa (mshtakiwa namba 4, yaani Mh. Freeman A. Mbowe)...

MASWALI YA KUTUONGOZA KATIKA MJADALA HUU NI HAYA;

1. Je, mpaka hatua hii kwa wote mnaofuatilia kesi hii, na kwa mtazamo wa kila mmoja based on the evidence uliokwisha kutolewa, unadhani objection ya upande wa utetezi itatoboa....?

2. Kwa maelezo ya mshtakiwa namba 1 na 2 ambao pia ndiyo mashahidi wenyewe wa kesi hii ndogo, unadhani wameweza kuishawishi mahakama kuwa ni kweli waliteswa kama njia ya kuwalazimisha kukubali maelezo waliyoyatoa polisi chini ya kiapo cha "onyo?"...

3. Ili kuthibitisha kuwa mtu fulani aliteswa, ukiachilia mbali maelezo ya mdomo kuwa nilipigwa sana na kufanyiwa hivi au vile, ushahidi mkubwa huwa ni alama za makovu ya vidonda katika mwili...

Je, mashahidi walionesha alama zozote zinazoashiria tendo la kupigwa na kuteswa lilitendeka kweli....?

Alamsiki. Karibuni kwa mjadala...
Tukuulize wewe unaehudhuria mahakamani kama ulivyokwisha jinasibu.

Au kama wewe ni jaji basi toa hukumu tu usisumbue watu vichwa.

Ila kama kweli unahudhuria mahakamani rejea pale shahidi alipoonyesha makovu miguuni,mikononi na kichwani huku wakiomba asioneshe yaliyofichwa maungoni.

Asubuhi njema
 
Sijui kwa nini judge asisimamishe hii kesi maana Mpaka sasa tayari amekwisha sikia mengi ya kumfanya aamue...ya nini kuendelea kuwahoji mashahidi wengine waliobaki ili hali waliobaki wote watakuja kusema au ku collaborate yote ya ushahidi wa utetezi? Sioni kama kuna haja ya kuendelea maana amekwisha sikia mengi tayari Mpaka sasa na anaweza kutoa maamuzi kwa yale yote aliyoyasikia...

serikali wamefunga ushahidi tayari... au labda ni kuwaruhusu waendelee ili mawakili waendelee kula fedha za umma tu kama akina kingai na Mahita?

Au labda ni kuwaruhusu cdm waendelee tu kusema halafu judge aseme ushahidi unapokelewa halafu kesi kubwa ya Msingi inaendelea na tayari mashahidi wa chadema wanakuwa wameisha na hakuna jipya?

Je kamanda Sirro ataitwa katika hii kesi ndogo au ni katika kesi kubwa tu? Nasikia huwa anatuma wawakilishi tu - MaRPC wamuwakilishe, sijui hii itakuwaje Sirro akitaka hivyo?

Kesi yote Mpaka sasa ni ya kupoteza muda tu na kuwasumbua watuhumiwa... ikiisha tu, moto wa katiba mpya utarudi na hapo ndio utakuwa mwanzo wa vurugu kati ya JWTZ, polisi na wananchi... subiri tu... ndio hayo yanakuja kutokea, hata wakifungwa, ni hayo hayo maana JWTZ wamedharirishwa vibaya sana na hawa polisi uchwara wasio jua hata miongozo yao ya kazi...

Issue Kubwa kwa judge Kuamua ni je kutokufuata miongozo ya kazi kunaifanya hiyo kazi kuwa batili? Ni Hilo tu ndilo linalotakiwa kuamuliwa mengine yote ni Isidingo...
Huo moto wa katiba unasubiri hadi kesi iishe? Isipoisha karibuni basi moto wa katiba nao haupo?? Upinzani wa TZ ni majanga matupu, ni ubatili na kujilisha upepo. Kesi itaisha na hakutakuwa na moto wa katiba wala bibi ya moto wa katiba, hakuna mpinzani mwenye guts za kuanzisha moto wowote hapa TZ, tuna wapinzani wa kuropoka na kupiga makelele nyuma ya keyboard!! Kama kulikuwa kuna jambo la wapinzani kuwasha huo moto unaosema basi ilibidi wauwashe mwenyekiti wao aachiwe, nini kimetokea?? Kwa sasa wanaogopa hata kuvaa Tshirt zao nyekundu mahakamani...
 
Polisi hawawezi kujificha ndani ya kichaka cha mashtaka ya ugaidi au uhujumu uchumi ili kukandamiza haki za watu yaani fundamental rights, right not to be tortured na nyingine nyingi... hii kesi ya mbowe yaweza kuwa precedent au test kesi kwa watu wengi sana kuachiwa baada ya ruling hii kama ikiamulia Kwamba PGO ni msahafu wa polisi na ni lazima ufuatwe 24/7.
Likifanyika hilo, magereza yatapumua kidogo haswa kutokana na technicality hii ya polisi ku breach fundamental rights na kutofuata PGO waliyowekewa...
 
Huo moto wa katiba unasubiri hadi kesi iishe? Isipoisha karibuni basi moto wa katiba nao haupo?? Upinzani wa TZ ni majanga matupu, ni ubatili na kujilisha upepo. Kesi itaisha na hakutakuwa na moto wa katiba wala bibi ya moto wa katiba, hakuna mpinzani mwenye guts za kuanzisha moto wowote hapa TZ, tuna wapinzani wa kuropoka na kupiga makelele nyuma ya keyboard!! Kama kulikuwa kuna jambo la wapinzani kuwasha huo moto unaosema basi ilibidi wauwashe mwenyekiti wao aachiwe, nini kimetokea?? Kwa sasa wanaogopa hata kuvaa Tshirt zao nyekundu mahakamani...
Nimekuelewa, ila mimi nazungumzia big elephant in the room, yaani bifu kati ya polisi na JW... mengi yatafanyika ndani ya carpet na yatakuwa na madhara mskubwa huko safarini
 
Huo moto wa katiba unasubiri hadi kesi iishe? Isipoisha karibuni basi moto wa katiba nao haupo?? Upinzani wa TZ ni majanga matupu, ni ubatili na kujilisha upepo. Kesi itaisha na hakutakuwa na moto wa katiba wala bibi ya moto wa katiba, hakuna mpinzani mwenye guts za kuanzisha moto wowote hapa TZ, tuna wapinzani wa kuropoka na kupiga makelele nyuma ya keyboard!! Kama kulikuwa kuna jambo la wapinzani kuwasha huo moto unaosema basi ilibidi wauwashe mwenyekiti wao aachiwe, nini kimetokea?? Kwa sasa wanaogopa hata kuvaa Tshirt zao nyekundu mahakamani...
Ukikaa huku unabugia ugali ndivyo unavyowaza?Very hopeless!
 
Kuna watu hawakuwa happy kuona Makomando wanafanya kazi chini ya Mpinzani..... Wakawaibulia kesi. Period.

Ila kinachoendelea jeshini kinashtua kidogo. Inakuwaje Makomando wa apoteza kazi kiasi hicho. Hao tuliowasikia so far ni watatu.... Je ambao hatujawasikia? No wonder jeshi kila siku tu nasikia linafanya usajili Utafikiri tuko vitani.
 
Mahita alinichekesha sana.Kibatala alimuuliza alitumia PGO katika ukamataji ule?Mahita akajibu kuwa hajawahi kutumia PGO katika ukamataji wake wowote ule.

Kibatala alichanganywa na jibu hili ikabidi amuombe jaji ruhusa ya kuishia hapo na akaenda kukaa kabisa.Baada ya ishu hii ya mahita upande wa jamhuri ilibidi wafunge upande wa mashahidi.It was a big blow.
 
Nimekuelewa, ila mimi nazungumzia big elephant in the room, yaani bifu kati ya polisi na JW... mengi yatafanyika ndani ya carpet na yatakuwa na madhara mskubwa huko safarini
Hamna kitu kama hicho Mkuu, hao ni kitu kimoja!! Dunia ya sasa siyo ile ya zamani kwamba kila kitu kilikuwa kinamalizwa kwa maugomvi, siku hizi mambo mengi yanaisha kwa mazungumzo na compromises!! Ndiyo maana kwa sasa dunia nzima hakuna vita hata moja "direct" kati ya taifa moja na lingine
 
Hamna kitu kama hicho Mkuu, hao ni kitu kimoja!! Dunia ya sasa siyo ile ya zamani kwamba kila kitu kilikuwa kinamalizwa kwa maugomvi, siku hizi mambo mengi yanaisha kwa mazungumzo na compromises!! Ndiyo maana kwa sasa dunia nzima hakuna vita hata moja "direct" kati ya taifa moja na lingine
Sasa mbona hiyo compromise na kwa njia ya mazungumzo ya wanasiasa wetu haipo au ni kwa nini isifuatwe hadi kesi za kutunga tunga ? Polisi wapunguziwe kazi maana hata huo muda wa kuisoma PGO yote na kuielewa practically wanautoa wapi?
 
Naona objection ya upande wa utetezi ina nafasi kubwa ya kutoboa kwasababu;

1. Maelezo ya mshtakiwa wa kwanza na wa pili yote yamethibitisha walikamatwa bila kufuata sheria ( PGO) hawakukamatwa bali walitekwa, na zaidi ilithibitika hata polisi wetu hawavijui vizuri vifungu vya kwenye PGO.

2. Polisi walishindwa kujitambulisha kwa watuhumiwa wao ni akina nani (hawakutoa vitambulisho), na watuhumiwa wana makosa gani.

3. Njia iliyotumika kuwakamata, waliwavizia, mmoja kutoka nyuma akamkaba mtuhumiwa na mwingine mbele, ikiwemo kuwafunika usoni na vitambaa (jacket na shuka) huu haukuwa ukamataji bali ni utekaji.

4. Maelezo ya mshtakiwa wa kwanza, alipokamatwa alipigwa na vishikizo vya mkanda kwenye suruali yake vikakatika na bahati nzuri hiyo suruali ndiyo aliivaa siku ya kutoa ushahidi akiwa ameishikiza kwa kamba.

5. Maelezo ya mshtakiwa wa kwanza na wa pili kufanana kwamba polisi baada ya kumkamata mshtakiwa wa kwanza, walimuwekea madawa ya kulevya, na pistol, mshtakiwa wa pili akaona atoe vitu vyake mfukoni mapema ili kuepusha nae asijekuwekewa vitu kama mwenzake.

6. Haki za watuhumiwa wakiwa mikononi mwa polisi zilikiukwa, kwanza polisi waliwabadilishia majina yao ya asili na kuwapa ya bandia, hili lilifanyika ili ndugu wa watuhumiwa wasijue ndugu zao wako kituo gani cha polisi, pili, kunyimwa chakula kwa siku kumi, na tatu, vipigo walivyopata wakiwa mikononi mwa polisi.

Hapa tunaona mshtakiwa wa kwanza alishindwa kutembea kutokana na kipigo akawa anaburuzwa na polisi, na mshtakiwa wa pili, yeye aliamua kuruka ruka ili apunguze maumivu ya kipigo kwa kuamini kwamba, kama angeendelea kukaa muda mrefu bila kufanya mazoezi ndio maumivu ya kipigo cha polisi yangezidi kwake.

- Vipigo, kauli za vitisho zilizotolewa na polisi kwa watuhumiwa, na kunyimwa chakula kwa siku kumi, vinatosha kuonesha kwamba watuhumiwa walitoa maelezo polisi wakiwa na hofu kwa ukatili waliofanyiwa na polisi/ wakiwa hawana afya njema ya akili kutokana na njaa, hivyo waliona bora watoe maelezo au wasaini maelezo waliyokuta yameshaandikwa tayari, ili kuokoa maisha yao.
 
Naona objection ya upande wa utetezi ina nafasi kubwa ya kutoboa kwasababu;

1. Maelezo ya mshtakiwa wa kwanza na wa pili yote yamethibitisha walikamatwa bila kufuata sheria ( PGO) hawakukamatwa bali walitekwa, na zaidi ilithibitika hata polisi wetu hawavijui vizuri vifungu vya kwenye PGO.

2. Polisi walishindwa kujitambulisha watuhumiwa wao ni akina nani (hawakutoa vitambulisho), na watuhumiwa wana makosa gani.

3. Njia iliyotumika kuwakamata, waliwavizia, mmoja kutoka nyuma akamkaba mtuhumiwa na mwingine mbele, ikiwema kuwafunika usoni na vitambaa (jacket, na shuka) huu haukuwa ukamataji bali ni utekaji.

4. Maelezo ya mshtakiwa wa kwanza, alipokamatwa alipigwa na vishikizo vya mkanda kwenye suruali yake vikakatika na bahati nzuri hiyo suruali ndiyo aliivaa siku ya kutoa ushahidi akiwa ameishikiza kwa kamba.

5. Maelezo ya mshtakiwa wa kwanza na wa pili kufanana kwamba polisi baada ya kumkamata mshtakiwa wa kwanza walimuwekea madawa ya kulevya na pistol, mshtakiwa wa pili akaona atoe vitu vyake mfukoni mapema ili kuepusha nae asijekuwekewa vitu kama mwenzake.

6. Haki za watuhumiwa wakiwa mikononi mwa polisi zilikiukwa, kwanza polisi waliwabadilishia majina yao ya asili na kuwapa ya bandia, hili lilifanyika ili ndugu wa watuhumiwa wasijue ndugu zao wako kituo gani cha polisi, pili, kunyimwa chakula kwa siku kumi, na tatu, vipigo walivyopata wakiwa mikononi mwa polisi.

Hapa tunaona mshtakiwa wa kwanza alishindwa kutembea kutokana na kipigo akawa anaburuzwa na polisi, na mshtakiwa wa pili, yeye aliamua kuruka ruka ili apunguze maumivu ya kipigo kwa kuamini kwamba, kama angeendelea kukaa muda mrefu bila kufanya mazoezi ndio maumivu ya kipigo cha polisi yangezidi kwake.

- Vipigo, kauli za vitisho zilizotolewa na polisi kwa watuhumiwa, vinatosha kuonesha kwamba watuhumiwa walitoa maelekezo wakiwa hofu kwa ukatili waliofanyiwa na polisi, waliona bora watoe maelezo au wasaini maelezo waliyokuta yameshaandikwa tayari, ili kuokoa maisha yao.
safi sana mkuu!! umeelezea kwa ufasaha sana!!
 
Sasa mbona hiyo compromise na kwa njia ya mazungumzo ya wanasiasa wetu haipo au ni kwa nini isifuatwe hadi kesi za kutunga tunga ? Polisi wapunguziwe kazi maana hata huo muda wa kuisoma PGO yote na kuielewa practically wanautoa wapi?
Mazungumzo yapo, ila kuna pande moja kichwa ngumu, wanataka kulazimisha kuishi kama walivyoishi awamu ya 4 bila kutambua kuwa kila awamu ina mtazamo tofauti na awamu nyingine!! Siku wakikubali kuevolve kutokana na vipindi tofauti tofauti basi hii mikwaruzano yote itaisha!! Wewe hapo kazini kwako umesoma miongozo yote, kila nukta yahusuyo kazi yako?
 
Back
Top Bottom