Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,608
- 86,300
Katika pita pita zangu nimekutana na ka' makala kadogo hivi, kazuri kameandikwa na Buyobe wa Twitter. Nikaona si dhambi kukaweka hapa Ili wale wanaotetea "upumbavu" wa CCM Kwa minajili ya "UDINI" wakumbuke hili nalo.
Tarehe 25 December 2017, Askofu Zakaria Kakobe akiwa kanisani kwenye ibada ya Christmas, katika kanisa la FGBF Mwenge jijini Dar es Salaam, alinukuliwa akituma salamu kwa Rais wa JMT, Dkt. John P. Magufuli.
"Rais John Pombe Magufuli, nawe unatakiwa kutubu leo. Unaposherekea sikukuu ya Christmas, ili uridhiwe na Mungu unatakiwa nawe utubu".
"Leo ni siku ya watawala wa Tanzania kutubu. Leo tumeanza kuona misingi ya amani ya nchi yetu ikitikiswa. Amani iliyojengwa kwa gharama kubwa na waasisi wetu. Tumeanza kuona nchi hii ni ya chama kimoja na huu ni uovu. Mungu mwenyewe anaheshimu sheria basi kama na sisi tumeweka sheria tunapaswa kuheshimu sheria tulizojiwekea wenyewe. Hii si nchi ya chama kimoja. Kama mnataka kubadilisha si mbadilishe tu mara moja kupitia wabunge wenu wa CCM, si mko wengi?".
"Sheria ni lazima zizingatiwe! Na kwa hili nitapiga kelele mpaka Mlima Kilimanjaro. Huwezi kusema wewe huwezi kusemwa, wewe ni nani? Mungu anasemwa vibaya sembuse wewe?".
"Mungu mwenye nguvu kuliko Magufuli, ana nguvu kuliko majeshi yote ya nchi, lakini anatukanwa na bado hatumii majeshi yake. Hata wewe unaweza ukawa mvumilivu"
Baada ya kauli hii, Askofu Kakobe alipokonywa passport yake, alihojiwa uraia wake na aliandamwa na TRA kwa madai ya kodi.
Huyu alikuwa ni kiongozi wa dini ya Kikistro na alimkosoa Mkristo Magufuri
Huu ulikuwa udini? Wa dini gani?
Askofu wa Catholic Jimbo la Rulenge (Severine Niwemugizi) alimkosoa mkatoliki mwenzake Magufuri juu ya haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano.
Aliishia kupokonywa passport na kuhojiwa uraia wake.
Alikuwa mdini? Akishabikia dini gani?
Nachukizwa sana na yeyote ambaye atataka kutugawa kwa misingi ya kidini.
Kukosoa haiwezi hata mara moja kuwa udini.
Kuwa kiongozi wa dini hakumnyimi haki kiongozi huyo kupata haki zake za kikatiba kutoa maoni juu ya mambo ya nchi yake kama anavyoweza kufanya Mwalimu, daktari, mkulima au mfugaji.
Tukemee wale wote wanaotaka kujificha kwenye udini pale tu wanapokosolewa kwa makosa waliyoyafanya wenyewe.
Mungu Ibariki Tanzania na watu wote.
Uhuru, Umoja na Amani
From your commander of the hand to mouth battalion
A dull, Colorless and Clueless old man now chewing Mugombero the turbo charger.
Hii ni copy and paste
View: https://twitter.com/fbuyobe/status/1693344546560630858?t=7iwxWIHRnifJmbr1Oh8RyQ&s=19
Tarehe 25 December 2017, Askofu Zakaria Kakobe akiwa kanisani kwenye ibada ya Christmas, katika kanisa la FGBF Mwenge jijini Dar es Salaam, alinukuliwa akituma salamu kwa Rais wa JMT, Dkt. John P. Magufuli.
"Rais John Pombe Magufuli, nawe unatakiwa kutubu leo. Unaposherekea sikukuu ya Christmas, ili uridhiwe na Mungu unatakiwa nawe utubu".
"Leo ni siku ya watawala wa Tanzania kutubu. Leo tumeanza kuona misingi ya amani ya nchi yetu ikitikiswa. Amani iliyojengwa kwa gharama kubwa na waasisi wetu. Tumeanza kuona nchi hii ni ya chama kimoja na huu ni uovu. Mungu mwenyewe anaheshimu sheria basi kama na sisi tumeweka sheria tunapaswa kuheshimu sheria tulizojiwekea wenyewe. Hii si nchi ya chama kimoja. Kama mnataka kubadilisha si mbadilishe tu mara moja kupitia wabunge wenu wa CCM, si mko wengi?".
"Sheria ni lazima zizingatiwe! Na kwa hili nitapiga kelele mpaka Mlima Kilimanjaro. Huwezi kusema wewe huwezi kusemwa, wewe ni nani? Mungu anasemwa vibaya sembuse wewe?".
"Mungu mwenye nguvu kuliko Magufuli, ana nguvu kuliko majeshi yote ya nchi, lakini anatukanwa na bado hatumii majeshi yake. Hata wewe unaweza ukawa mvumilivu"
Baada ya kauli hii, Askofu Kakobe alipokonywa passport yake, alihojiwa uraia wake na aliandamwa na TRA kwa madai ya kodi.
Huyu alikuwa ni kiongozi wa dini ya Kikistro na alimkosoa Mkristo Magufuri
Huu ulikuwa udini? Wa dini gani?
Askofu wa Catholic Jimbo la Rulenge (Severine Niwemugizi) alimkosoa mkatoliki mwenzake Magufuri juu ya haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano.
Aliishia kupokonywa passport na kuhojiwa uraia wake.
Alikuwa mdini? Akishabikia dini gani?
Nachukizwa sana na yeyote ambaye atataka kutugawa kwa misingi ya kidini.
Kukosoa haiwezi hata mara moja kuwa udini.
Kuwa kiongozi wa dini hakumnyimi haki kiongozi huyo kupata haki zake za kikatiba kutoa maoni juu ya mambo ya nchi yake kama anavyoweza kufanya Mwalimu, daktari, mkulima au mfugaji.
Tukemee wale wote wanaotaka kujificha kwenye udini pale tu wanapokosolewa kwa makosa waliyoyafanya wenyewe.
Mungu Ibariki Tanzania na watu wote.
Uhuru, Umoja na Amani
From your commander of the hand to mouth battalion
A dull, Colorless and Clueless old man now chewing Mugombero the turbo charger.
Hii ni copy and paste
View: https://twitter.com/fbuyobe/status/1693344546560630858?t=7iwxWIHRnifJmbr1Oh8RyQ&s=19