Ni jambo la kusikitisha jinsi Watanzania, hasa sisi watumishi wa serikali, tunavyoendelea kukandamizwa na baadhi ya viongozi wa serikali walio madarakani lakini tanaogopa kutoa malalamiko adharani na badala yake tunatoa malalamiko kimya kimya kisa tunaogopa kuchukuliwa hatua au kuhusishwa na suala la uvunjivu wa amani.
Ninasema hivi kwa kuwa mwezi uliyopita Octoba 2011, watumishi wengi wa serikali za mitaa/halmashauri nchini wamekatwa kiasi kikubwa cha fedha toka kwenye mishahara yao, na mimi ni mmoja wao, lakini jambo la kusikitisha ni kwamba tulipojaribu kumuuliza Mwajiri wetu juu ya kitendo hicho hatukupata majibu ya kuridhisha hadi sasa. Hata chama chetu cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa(TALGWU) hawajazungumza chochote kuhusiana na jambo hili.
Je kwa kuwa jambo hil linahusu mkataba wa mtumishi na mwajiri ninaweza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Mkurugenzi wangu mimi peke yangu bila kuwahusisha watumishi wengine? Make naona watu wamekaa kimya kana kwamba hakuna kilichotokea na hatujui hatima ya makato hayo!!!
Ninasema hivi kwa kuwa mwezi uliyopita Octoba 2011, watumishi wengi wa serikali za mitaa/halmashauri nchini wamekatwa kiasi kikubwa cha fedha toka kwenye mishahara yao, na mimi ni mmoja wao, lakini jambo la kusikitisha ni kwamba tulipojaribu kumuuliza Mwajiri wetu juu ya kitendo hicho hatukupata majibu ya kuridhisha hadi sasa. Hata chama chetu cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa(TALGWU) hawajazungumza chochote kuhusiana na jambo hili.
Je kwa kuwa jambo hil linahusu mkataba wa mtumishi na mwajiri ninaweza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Mkurugenzi wangu mimi peke yangu bila kuwahusisha watumishi wengine? Make naona watu wamekaa kimya kana kwamba hakuna kilichotokea na hatujui hatima ya makato hayo!!!