Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
KUINGIA NDOANI NA MTU USIYEMPENDA KUTAKUZIDISHIA UPWEKE.
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Kuishi mwenyewe ni kazi, kunachosha, kunakufanya uwe mpweke. Hapo Maisha yanapoteza mvuto. Lakini kuishi na Mwenza usiyempenda na asiyekupenda ndio kubaya zaidi na kunaleta upweke zaidi.
Ninaposema utafute Mwanamke anayekupenda na unayempenda ninamaanisha kuyapa Maisha yako maana na furaha. Kuondoa upweke ambao hakuna Dawa ya upweke zaidi ya upendo.
Tafuta Mwenza ambaye Mtakuwa washkaji, marafiki, mnao-share interests nyingi(sio zote) na hobbies.
Ili hilo litokee lazima mpendane Sana.
Nakuhakikishia kama hampendani lazima Moto uwawakie, Utapeli utawaua, maumivu Makali yatawashusha kuzimu polepole Kwa uchungu mkali,
Watoto mtakaowazaa sio chanzo cha kuondoa upweke wenu. Mapenzi yenu ndio chanzo kikuu cha kuondoa upweke wenu.
Kijana wa miaka 30 iwe ni Binti au kijana wakiume anaweza asielewe nini ninasema hapa. Lakini Watu wazima wanajua nazungumzia nini hapa.
Bar haiwezi kukupa Kampani, vijiwe haviwezi kukupa Kampani, saluni au vilinge vya umbea havijawahi kuondoa upweke. Mumeo au Mkeo mnayependana ndiye MTU pekee anayeweza kuondoa Upweke wako.
Sio Baba yako, sio Mama yako atakayeweza kuondoa upweke wako.
Elewa kuwa kadiri unavyokua mkubwa ndivyo unavyozidisha umbali na Wazazi wako, kama ukiwa mdogo ulizoea kuwasiliana na mzazi wako masaa yote, basi ukifika umri wa balehe masaa hupungua, na itafikia Wakati Kwa Siku unaweza kuongea na mzazi dakika zisizozidi thelasini.
Na kuna Wakati inaweza kupita siku nzima hujaongea naye. Unajua hiyo inamaanisha nini? Jibu lako ni Stori ya siku nyingine.
Utamu wa ndoa upo katika umri wa utu uzima hasahasa Watoto wakishakuwa wamekuwa wakubwa, hapo Watoto wanaanza kutawanyika na kutafuta Maisha Yao. Hapo ndipo mambo huweza kuwa mazuri au mabaya ikiwa hamkuwa mnapendana kama Mume na Mke kweli.
Elewa kuwa kama hakuna mapenzi, unaweza kuwa umeolewa lakini bado ukawa mpweke, yaani unaishi na MTU lakini kama hayupo. Hakuna Stori, hakuna Michezo, hakuna matani, hakuna burudani, hakuna kucheza pamoja.
Yaani mnakuwa kama mpo kwenye Kampuni mnafanyakazi, yaani mmeajiriwa. Muda wote mpo serious kama vile vibarua walioajiriwa na Mjerumani.
Mkipendana, ninyi ndio Ma-boss WA nyumba yenu. Msipopendana ninyi wote ni watumwa, au mmoja WA hiyo Ndoa anaweza kuwa mtumwa WA mwenzake. Muda wote hofu, muda wote mashtaka, muda wote kushutumiana, muda wote kulaumiana na kurushiana maneno, muda wote kutafutiana Makosa.
Nafsi ikiwa uchi hata mwili uvalishwe nguo hautastirika. Upweke utakufanya uyachukie Maisha.
Pesa kamwe sio Dawa ya Upweke na haijawahi kuondoa upweke. Upweke SULUHU yake ni MTU unayempenda na anayekupenda. Hiyo ndio SULUHU.
Unaweza ukawa ndani ya jumba la ghorofa lakini ukawa mpweke na ukayaona Maisha mabaya Sana. Lakini mwingine anaweza akawa yupo Mkuranga kwenye nyumba ya nyasi lakini akawa na Kampani na furaha na kuyaona Maisha yanamaana kubwa.
Sio rahisi Watoto wadogo kunielewa, lakini zaidi sio rahisi Watu wenye upeo Mdogo au wavivu wa kufikirisha Akili zao kuelewa Taikon anazungumzia Jambo Gani.
Binti zangu, Mimi kama Baba yenu, kama nilivyowausieni, tafuteni wanaume wanaowapenda na mnaowapenda. Mimi kama Baba yenu siwezi kuwaingilia katika Jambo Hilo.
Hakuna mwanaume atakayeweza kununua moyo wako, wala hakuna thamani yoyote inayotosha kununua moyo wako zaidi ya moyo WA mwanaume unayempenda na anayekupenda.
Vivyohivyo Kwa Vijana wangu wa kiume, msilazimishe Mapenzi. Kama Mwanamke Hakupendi msimlazimishe, oeni Wanawake mnaowapenda na wanaokupendeni.
Msije mkajidanganya kuwa atakupenda hivyohivyo au atajifunza kukupenda. Huko ni kujidanganya. Wengi wameteseka.
Wengi wamewaona Wanawake ni wachawi, wabaya na wenye Roho Mbaya lakini kumbe kosa lilikuwa Lao kuwalazimisha wawapende, nao Wanawake wakajaribu kujifunza kuwapenda lakini siku zote kitu kisicho cha asili hushindikana.
Acha nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Kuishi mwenyewe ni kazi, kunachosha, kunakufanya uwe mpweke. Hapo Maisha yanapoteza mvuto. Lakini kuishi na Mwenza usiyempenda na asiyekupenda ndio kubaya zaidi na kunaleta upweke zaidi.
Ninaposema utafute Mwanamke anayekupenda na unayempenda ninamaanisha kuyapa Maisha yako maana na furaha. Kuondoa upweke ambao hakuna Dawa ya upweke zaidi ya upendo.
Tafuta Mwenza ambaye Mtakuwa washkaji, marafiki, mnao-share interests nyingi(sio zote) na hobbies.
Ili hilo litokee lazima mpendane Sana.
Nakuhakikishia kama hampendani lazima Moto uwawakie, Utapeli utawaua, maumivu Makali yatawashusha kuzimu polepole Kwa uchungu mkali,
Watoto mtakaowazaa sio chanzo cha kuondoa upweke wenu. Mapenzi yenu ndio chanzo kikuu cha kuondoa upweke wenu.
Kijana wa miaka 30 iwe ni Binti au kijana wakiume anaweza asielewe nini ninasema hapa. Lakini Watu wazima wanajua nazungumzia nini hapa.
Bar haiwezi kukupa Kampani, vijiwe haviwezi kukupa Kampani, saluni au vilinge vya umbea havijawahi kuondoa upweke. Mumeo au Mkeo mnayependana ndiye MTU pekee anayeweza kuondoa Upweke wako.
Sio Baba yako, sio Mama yako atakayeweza kuondoa upweke wako.
Elewa kuwa kadiri unavyokua mkubwa ndivyo unavyozidisha umbali na Wazazi wako, kama ukiwa mdogo ulizoea kuwasiliana na mzazi wako masaa yote, basi ukifika umri wa balehe masaa hupungua, na itafikia Wakati Kwa Siku unaweza kuongea na mzazi dakika zisizozidi thelasini.
Na kuna Wakati inaweza kupita siku nzima hujaongea naye. Unajua hiyo inamaanisha nini? Jibu lako ni Stori ya siku nyingine.
Utamu wa ndoa upo katika umri wa utu uzima hasahasa Watoto wakishakuwa wamekuwa wakubwa, hapo Watoto wanaanza kutawanyika na kutafuta Maisha Yao. Hapo ndipo mambo huweza kuwa mazuri au mabaya ikiwa hamkuwa mnapendana kama Mume na Mke kweli.
Elewa kuwa kama hakuna mapenzi, unaweza kuwa umeolewa lakini bado ukawa mpweke, yaani unaishi na MTU lakini kama hayupo. Hakuna Stori, hakuna Michezo, hakuna matani, hakuna burudani, hakuna kucheza pamoja.
Yaani mnakuwa kama mpo kwenye Kampuni mnafanyakazi, yaani mmeajiriwa. Muda wote mpo serious kama vile vibarua walioajiriwa na Mjerumani.
Mkipendana, ninyi ndio Ma-boss WA nyumba yenu. Msipopendana ninyi wote ni watumwa, au mmoja WA hiyo Ndoa anaweza kuwa mtumwa WA mwenzake. Muda wote hofu, muda wote mashtaka, muda wote kushutumiana, muda wote kulaumiana na kurushiana maneno, muda wote kutafutiana Makosa.
Nafsi ikiwa uchi hata mwili uvalishwe nguo hautastirika. Upweke utakufanya uyachukie Maisha.
Pesa kamwe sio Dawa ya Upweke na haijawahi kuondoa upweke. Upweke SULUHU yake ni MTU unayempenda na anayekupenda. Hiyo ndio SULUHU.
Unaweza ukawa ndani ya jumba la ghorofa lakini ukawa mpweke na ukayaona Maisha mabaya Sana. Lakini mwingine anaweza akawa yupo Mkuranga kwenye nyumba ya nyasi lakini akawa na Kampani na furaha na kuyaona Maisha yanamaana kubwa.
Sio rahisi Watoto wadogo kunielewa, lakini zaidi sio rahisi Watu wenye upeo Mdogo au wavivu wa kufikirisha Akili zao kuelewa Taikon anazungumzia Jambo Gani.
Binti zangu, Mimi kama Baba yenu, kama nilivyowausieni, tafuteni wanaume wanaowapenda na mnaowapenda. Mimi kama Baba yenu siwezi kuwaingilia katika Jambo Hilo.
Hakuna mwanaume atakayeweza kununua moyo wako, wala hakuna thamani yoyote inayotosha kununua moyo wako zaidi ya moyo WA mwanaume unayempenda na anayekupenda.
Vivyohivyo Kwa Vijana wangu wa kiume, msilazimishe Mapenzi. Kama Mwanamke Hakupendi msimlazimishe, oeni Wanawake mnaowapenda na wanaokupendeni.
Msije mkajidanganya kuwa atakupenda hivyohivyo au atajifunza kukupenda. Huko ni kujidanganya. Wengi wameteseka.
Wengi wamewaona Wanawake ni wachawi, wabaya na wenye Roho Mbaya lakini kumbe kosa lilikuwa Lao kuwalazimisha wawapende, nao Wanawake wakajaribu kujifunza kuwapenda lakini siku zote kitu kisicho cha asili hushindikana.
Acha nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam