Peter Stephano 809
Senior Member
- Feb 29, 2020
- 120
- 162
"Hatuwezi kutatua matatizo kwa kuyafanya hayapo" hii ni nukuu màarufu na inayopendwa na wanaharakati wengi.
Katika nukuu hii inaonyesha kuwa ili utatue tatizo ni lazima ukubali kuwa lipo kisha utafute suluhisho lake.
Pia nukuu hii inaonyesha kuwa huwezi kutatua tatizo kwa kulificha lisionekane.
Ni wazi kuwa mfumuko wa bei umetamalaki dunia nzima kwa sababu mbalimbali zinazotajwa na wataalamu wa uchumi Kama vile athari za ugonjwa wa virusi vya Corona na mgogoro wa Urusi na Ukraine.
Mfumuko wa bei kwenye bidhaa hasa mafuta na gesi umekuwa mkubwa na kupelekea ugumu wa maisha kwenye jamii.
Kama ilivyo nchini Tanzania nako hali si shwari kutokana na changamoto hii ya kupanda kwa bei za bidhaa. Kwa mfano bei ya mche mmoja wa sabuni kutoka 2000 mpaka 4000 kwa wastani, bei ya mafuta ya petrol na diesel kufikia 2800 kwa lita na kuendelea.
Huku bei ya mafuta ya kupikia ikiibua hisia za tofauti kwa kupanda hadi 8000 kwa lita katika baadhi ya maeno nchini. Kadhalika bei ya vifaa vya ujenzi imezidi kuwa gumzo kwa kuendelea kupanda kila kukicha. Mfumuko huu unahusishwa na sababu mbili nilizozitaja hapo awali.
Katika mtazamo wa kawaida sababu hizi zinaweza kuwa kuu kidunia lakini zina Sababu "sindikizi" nyingi ndani yake ambazo zimepelekea makali makubwa ya mfumuko wa bei hapa nchini.
Sababu anuai ni kauli za Viongozi wa serikali juu ya mfumuko wa bei ambazo zinaleta jeuri kwa wafanyabiashara kupandisha bei wanavyotaka kwakua wanajua Viongozi wa serikali hawana cha kuwafanya.
Wiki chache zilizopita Rais Samia Suluhu alisema Watanzania wajiandae na kupanda kwa bei za bidhaa. Kauli hii ilikua ni tahadhari lakini haikuwa na afya kutamkwa na kiongozi mkuu wa nchi.
Siku chache baada ya kauli hii ilianza kushuhudiwa bei za bidhaa kupanda kwa kasi zaidi ya ilivyotegemewa. Huenda wafanyabiashara na wasambazaji wa bidhaa waliichukulia kauli hii Kama mwanya wa kupandisha bei za bidhaa wanavyotaka.
Sababu ya pili ni kutokuwepo na chombo madhubuti kinachoshughulika na upangaji, usimamizi wa bei za bidhaa nchini hivyo kupelekea wafanyabiashara kujipangia bei wenyewe kinyume na uhalisia. Sababu ya tatu ni uwepo wa viashiria vya wafanyabiashara kufanya hujuma kama kuficha bidhaa kwenye maghala ili ziadimike Sokoni kisha wapandishe bei kwa makusudi.
Haingii akilini ukimwambia mwanachi wa Makete kule njombe ndani ndani ukimwambia kuwa bei ya sabuni inayotengenezwa kwa mawese ya Kyela imepanda kwa sababu ya Vita ya Ukraine. Hata aliye mjini hawezi kukubali kuambiwa kuwa bei ya simenti ya mtwara imepanda kwa sababu ya Vita ya Ukraine.
Sababu hizi kuu mbili zina mashiko kwa ukubwa wake lakini hazina uhalisia katika jamii iliyokubwa kushinda sababu nilizozitoa hapo.
Hayati Magufuli alifanikiwa kupunguza athari za Ugonjwa wa virusi vya Corona kwa kuaminisha raia kuwa Ugonjwa haupo na hauna madhara makubwa.
Silaha hii inaweza kutumika kuzuia mfumuko wa bei kwa serikali kuweka usimamizi makini katika upangaji wa bei za bidhaa nchini.
Viongozi wetu kuendelea kutuambia kuwa mfumuko wa bei katika bidhaa zote ni kutokana na vita ya Ukraine ni kuendelea kutuangamiza na huu ugumu wa Maisha.
Katika nukuu hii inaonyesha kuwa ili utatue tatizo ni lazima ukubali kuwa lipo kisha utafute suluhisho lake.
Pia nukuu hii inaonyesha kuwa huwezi kutatua tatizo kwa kulificha lisionekane.
Ni wazi kuwa mfumuko wa bei umetamalaki dunia nzima kwa sababu mbalimbali zinazotajwa na wataalamu wa uchumi Kama vile athari za ugonjwa wa virusi vya Corona na mgogoro wa Urusi na Ukraine.
Mfumuko wa bei kwenye bidhaa hasa mafuta na gesi umekuwa mkubwa na kupelekea ugumu wa maisha kwenye jamii.
Kama ilivyo nchini Tanzania nako hali si shwari kutokana na changamoto hii ya kupanda kwa bei za bidhaa. Kwa mfano bei ya mche mmoja wa sabuni kutoka 2000 mpaka 4000 kwa wastani, bei ya mafuta ya petrol na diesel kufikia 2800 kwa lita na kuendelea.
Huku bei ya mafuta ya kupikia ikiibua hisia za tofauti kwa kupanda hadi 8000 kwa lita katika baadhi ya maeno nchini. Kadhalika bei ya vifaa vya ujenzi imezidi kuwa gumzo kwa kuendelea kupanda kila kukicha. Mfumuko huu unahusishwa na sababu mbili nilizozitaja hapo awali.
Katika mtazamo wa kawaida sababu hizi zinaweza kuwa kuu kidunia lakini zina Sababu "sindikizi" nyingi ndani yake ambazo zimepelekea makali makubwa ya mfumuko wa bei hapa nchini.
Sababu anuai ni kauli za Viongozi wa serikali juu ya mfumuko wa bei ambazo zinaleta jeuri kwa wafanyabiashara kupandisha bei wanavyotaka kwakua wanajua Viongozi wa serikali hawana cha kuwafanya.
Wiki chache zilizopita Rais Samia Suluhu alisema Watanzania wajiandae na kupanda kwa bei za bidhaa. Kauli hii ilikua ni tahadhari lakini haikuwa na afya kutamkwa na kiongozi mkuu wa nchi.
Siku chache baada ya kauli hii ilianza kushuhudiwa bei za bidhaa kupanda kwa kasi zaidi ya ilivyotegemewa. Huenda wafanyabiashara na wasambazaji wa bidhaa waliichukulia kauli hii Kama mwanya wa kupandisha bei za bidhaa wanavyotaka.
Sababu ya pili ni kutokuwepo na chombo madhubuti kinachoshughulika na upangaji, usimamizi wa bei za bidhaa nchini hivyo kupelekea wafanyabiashara kujipangia bei wenyewe kinyume na uhalisia. Sababu ya tatu ni uwepo wa viashiria vya wafanyabiashara kufanya hujuma kama kuficha bidhaa kwenye maghala ili ziadimike Sokoni kisha wapandishe bei kwa makusudi.
Haingii akilini ukimwambia mwanachi wa Makete kule njombe ndani ndani ukimwambia kuwa bei ya sabuni inayotengenezwa kwa mawese ya Kyela imepanda kwa sababu ya Vita ya Ukraine. Hata aliye mjini hawezi kukubali kuambiwa kuwa bei ya simenti ya mtwara imepanda kwa sababu ya Vita ya Ukraine.
Sababu hizi kuu mbili zina mashiko kwa ukubwa wake lakini hazina uhalisia katika jamii iliyokubwa kushinda sababu nilizozitoa hapo.
Hayati Magufuli alifanikiwa kupunguza athari za Ugonjwa wa virusi vya Corona kwa kuaminisha raia kuwa Ugonjwa haupo na hauna madhara makubwa.
Silaha hii inaweza kutumika kuzuia mfumuko wa bei kwa serikali kuweka usimamizi makini katika upangaji wa bei za bidhaa nchini.
Viongozi wetu kuendelea kutuambia kuwa mfumuko wa bei katika bidhaa zote ni kutokana na vita ya Ukraine ni kuendelea kutuangamiza na huu ugumu wa Maisha.