Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Mbona uchaguzi wa mitaa ni mwezi wa kumi? Iweje hao wachague sasa? Hii habari ni kama imekaa upande vile.
 
Hapana habari ipo sahihi ila jamaa kachanganya mambo! Uchaguzi wa jana ulikua katika ngazi ya chama ambbapo ccm walikua wakitafuta wagombea wao ktk uchaguzi wa serikali za mtaa octoba
 
Hata mimi huu uchaguzi wa Serikali za Mtaa sifahamu unaendaji, je Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa anachaguliwa vipi na nani akishateuliwa huko kwenye vyama. Sielewi kabisa ninachoelewa ni madiwani, Bunge na rais.
 
Mkuu huo si uchaguzi wa serikali za mitaa, ni kura za maoni ndani ya chama, uchaguzi wenyewe ni mwezi october 2009.

Ni utaratibu ambao chama cha mapinduzi kimejiwekea kupata wagombea wanafasi mbalimbali watakaogombea kushika nafasi mbalimbali katika serikali.
 
Kaka si kweli kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa umefanyika. Kinachoendelea ni kura za maoni ndani ya Chama. Hivi uwenyeji tu ndio sifa bora ya kupata madaraka.Sisemi kuwa fedha ndio sifa bora la hasha, uchaguzi unacomprise vitu vingi likiwemo suala la uadilifu, kushirikiana na watu.

Ukiangalia kwa Tanzania, ukiachana na part partisanship, personality ina influence kubwa katika kutwaa madaraka. Angalia voters choice in Tanzania.
 
Nadhani watoto wa Kariakoo au teseme wenyeji wa Kariakoo mnajua kuwa weekend hii tulikuwa na chaguzi zetu haku mitaani lakini ya kusikitisha na ya ajabu ni ile ya kata ya Gerezani ambako Bwana MATIMBWA alipewa kura zaidi ya 300 za maoni za wanachama lakini MAFISADI ndani ya kamati ya Chama kwa sababu zao zisizo na kichwa wala miguu wameamua kumpa mtu aliyepewa kura 23 za maoni!!!

Halafu tunajiuliza tatizo letu liko wapi

Kule Kwingine nako FITNA imefanyika mpaka DIGOSI naye wakaamua kumwangusha lakini at least kwa haraka haraka nasikia mwenyewe alishachoka hiyo shughuli yenyewe

Naona anayepeta ni TAMBAZA alakini I'm not sure for how long

ninachotaka kusema ni kuwa CCM kwa mwenendo huu wa kuwapatia wananchi watu ambao hawawataki utajawatokea puani
 
gt wewe uliishi mtaa upi wa kariakoo?mi nilizaliwa livingstone.gerezani now nipo tegeta.
 
Wana ndugu naona wakti huu muafaka kutaka kuonyesha tumecchoka na siasa chafu za ccm...jamani tumechoka na tumchoka kweli...kama viongozi wanachaguliwa 2005 wanakuja 2009 kupiga pojoro za kuchaguliwa kuna haja ya kuwa na watu kama hawa....wahuni watupu

jamani tuanze na serikali za mitaa tucsichague CCM
 
baada ya serikali za michezo jamani tuwaondoe kabisa kwenye udiwani wakati wakisubiri hukumu ya UBUNGE
 
Wana ndugu huu ni uhuni wa siasa usioruhusiwa kabisa;
kama ni kashfa na uchafu wote basi iunge na CCM...jamani
majuzi hapo kimara mwisho kulikuwa na zoezi la kupiga kura
wagombea wa serikali za mitaa;baada ya zoezi kupita Bw MMOJA
anaitwa MSABAHA akashinda;mara yule anaemaliza na mashabiki wake wakaanza fujo...ndipo wakaamua majina yaende mbele;;walipofika huko
diwani wa sasa hivi kama mnavyomjua FISADI MTOTO RINGO aakawahadaa wenzake wamchague mchaga mwenzake anaitwa MASSAWE.......CCM WAMESHATANGAZIWA RASMI KIFO CHA MOTTO UPANDE WA KIMARA NA KAMA HAWATAAMINI HILI TUNAMKARIBISHA DIWANI RINGO KWENYE SHUGULI KAMILI AONE JINSI TUNAVYOWACHAGUA WAPINZANI....HATUDANGANYIKI TENA HIVI SASA....
 
Ha ha haa Uchaguzi unaosimamiwa na TAMISEMI ya Kombani! CCM wanapiga bao tu
 
Vijana hasa naomba tulisaidie taifa letu kwa kugombea serikali za mitaa. Mi nimeshafanya uwamuzi. Nitagombea kwa nia ya kushinda uwenyekiti wa mtaa. Wewe unafanya nini kuinusuru TANZANIA na uharibifu wa CCM??
 
Hili ni suala nimekuwa najiuliza sana huko Tanzania. Tunaelewa kuwa Mwaka huu mwezi Oct kuna chaguzi za Serikali za mitaa yaani kuchagua wenyeviti wa Serikali za mitaa na wajumbe wao.

naona kuwa mpaka sasa hakuna msisimko wowote wa maandalizi kwa vyama vya siasa na hata Serikali kijumla kama maandalizi ya chini chini aliyoanza kwa uchaguzi mkuu mwakani october.

Ukisoma Katiba ya Tanzania , Ibara ya 146 (1) inazungumzia madhumuni ya kuepo ka serikali za Mitaa ni kupeleka madaraka kwa wananchi.

katiba inazungumzia vizuri sana umuhimu wa kuimarisha demokrasia hususan katika ngazi za mitaa na kuelekea kwenye serikali kuu.

nauliza kwanini chaguzi zake hazina mashamsham?

Nitapembua kutoka kwenye katiba ya tanzania umuhimu na uhalali wa Serikali za mitaa ukilinganisha na serikali kuu.

Nasriyah Saleh Al-Nahdi.

Uchaguzi huu ni jeki ya kuweka chama tawala madarakani. ndio maana wenyewe wamechangakia kimya kimya toka zamani, lakini wengine hawana habari kabisa. Waziri tamisemi ndio sterling, unategemea nini kwenye huu uchaguzi??
 
Uandikishwaji wapigakura waleta vituko
Richard Makore

Zoezi la uandikishwaji wapiga kura jijini Dar es Salaam jana lilijawa na vitimbi baada ya mjumbe wa CCM tawi la Mkunduge kukamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi na wafuasi wa CUF kwa madai ya kutaka kujiandikisha sehemu asiyostahili.
Kadhalika wafuasi wa CCM jana walimteka mwandikishaji na kumuamuru awaandikishe kwa nguvu katika mtaa wa Tandale kwa Tumbo.
Ofisa Mtenadji wa mtaa huo, Peter Mkongereza, alikiri kutokea matukio hayo na kusema kuwa kutokana na hali hiyo alilazimika kufunga vituo vitano kati ya saba vilivyokuwa vikitumika.
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jana alisema kuwa wafuasi wa CUF ndiyo waliomgundua mjumbe huyo aliyetoka eneo lingine na kwenda mtaa usiokuwa wa kwake na kutaka aandikishwe. Wafuasi wa CUF baada ya kumshtukia mjumbe huyo kuwa sio mkaazi wa pale walimkamata na kumuweka chini ya ulinzi lakini baadaye walimuachia.
Aidha, katika zoezi hilo ziliibuka vurugu baada ya wafuasi wa CUF kupinga kuwepo vituo saba katika mtaa huo kinyume na makubaliano ya viongozi wa vyama vya siasa ya kutaka kituo kiwe kimoja.
Mkongereza alikiri kufungwa kwa vituo hivyo na kudai kuwa aliamua kuweka vituo vingi baada ya kupata maagizo kutoka kwa Mtendaji wake wa Kata.
Wafuasi wa CUF mapema jana asubuhi waliwahi vituoni ili kuangalia zoezi linavyokwenda na baada ya kuingiwa na wasiwasi ndipo walipoamua kumhakiki kila mtu aliyekuwa akifika hapo kujiandikisha.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Ofisa Mtendaji wa mtaa wa Tandale kwa Tumbo, wafuasi hao baada ya kuendelea kuhakiki watu waliokuwa wakifika hapo kujiandikisha walipomgundua mjumbe wa CCM na walipomuuliza maswali alikiri kuwa yeye sio mkaazi wa pale na kwamba alitaka ajiandikishe kinyemela.
Kuhusu wafuasi wa CCM kumteka mwandikishaji na kumuingiza ndani ya nyumba ya mtu na kamuamuru awaandikishe alikiri kuwepo kwa tukio hilo.
Alisema kilichozua vurugu na kusababisha kuwachukua waandikishaji na kuwaweka ofisini kwake ni kutokana na kukiukwa kwa makubaliano ya awali yaliyofikiwa ambapo walikubaliana kiwepo kituo kimoja ambapo waandikishaji wote watakuwa pamoja.Mtaa wa Tandale kwa Tumbo una idadi ya wakaazi 21,415 na Kaya 4,283 ni moja ya ngome ya CUF.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo anayemaliza muda wake anatoka CUF.


NIPASHE
 
Hakika ukiangalia katiba ya Tanzania Ibara ya 146 (2)(c) inasema malengo ya Serikali za mitaa ni kuimarisha demokrasia na kutumia demokrasia kuharakisha maendeleo ya wananchi.

Sasa utaona hapa ni sehemu muhimu sana kwa Serikali ikiwa pamoja na vyama vya siasa kuanza kujikita ili kujihakikishia ushindi katika uchaguzi mkuu.

Ingawa demokrasia yenyewe imepindishwa na Sheria namba 7 na namba 8 za mwaka 1982 zinazoipa Serikali kuu mamlaka ya kuunda au kuvunja serikali za mitaa bila kujadiliana na wananchi husika.

Mtu anaepewa mamlaka kisheria kuvunja Serikali za mitaa ni waziri wa TAMISEMI. hapo utaona Serikali kuu ndio yenye mamlaka ya kuunda serikali za mitaa na sio wananchi.


Sasa ni vizuri wabunge wetu huko Tanzania mkajikita katika kurekebisha katiba na kuupa uchaguzi huu wa serikali za mitaa chachu ja demokrasia na maendeleo ya nchi.

Nasriyah saleh Al-Nahdi
.

sasa kama sheria zinasema hivyo. Kuna umuhimu gani kufanya au kushiriki chaguzi hizi?
 
Bila kurekebisha katiba huko Tanzania, Uchaguzi utakuwa kiini macho tu.
 
Huu sio uchaguzi ni upuuzi mtupu. Anayeamini kwamba mwaka huu 2009, unaweza kuwa na uchaguzi unaosimamiwa na kada wa CCM na akatoa haki sawa kwa vyama vyote vya siasa basi huyo bado anaishi katika giza nene when it comes to politics za Tanzania.

Dawa ni kuingiza wabunge wa upinzani wengi kwenye bunge lijalo watakaoweza kupiga kura zitakazotosha ili kuuhamisha huu uchaguzi uwe unasimamiwa na Tume ya Uchaguzi badala ya TAMISEMI. Wadau wa chaguzi na wafadhili wanaweza kuibana NEC kwa namna fulani lakini ni vigumu sana kupambana na wizara ya TAMISEMI.
 
Kuiondoa CCM madarakani tuna kazi kubwa Wananchi. Manake wanatumia kila mbinu (fedha, danganya toto, tume za uchaguzi nk) kubaki madarakani.
na sisi miafirika tumezidi ujinga ndio maana tunaongozwa na viongozi wapumbavu
 
Back
Top Bottom