AlWatan Nyuki
New Member
- Jan 10, 2012
- 4
- 10
Jamaa mmoja kutoka bara ya Kenya alikuwa anafanya kazi mjini Mombasa. Siku moja, kutokana na msongamano wa magari, alichelewa kufika kazini. Akiwa njiani sehemu za Mwembe Tayari ndani ya matatu (daladala),aliamua kumtumia boss wake message ya kuwa atachelewa kufika kutokana na msongamano wa magari. Alipomaliza kuiandika message kabla hajaituma, mwizi mmoja alinyapa akampora ile simu kwa dirishani. Jamaa kwa kuchanganyikiwa, badala ya kupiga kelele za 'mwizi, mwizi', akawa anamuambia mwizi hivi:
" Nanii tafadhali bonyeza SEND, bonyeza SEND tafadhali."
" Nanii tafadhali bonyeza SEND, bonyeza SEND tafadhali."