Kuchagua mawaziri kuwa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa bunge la Katiba tunajifunza nini?

Mkodoleaji

JF-Expert Member
Apr 27, 2008
458
138
Jamani naona mimi kuna somo moja ambalo bado napenda kujifunza kwenye hilo bunge la katiba nalo ni somo la utawala bora. Hivi hawa wajumbe walioenda kule wakachagua mawaziri (mwenyekiti-Sitta na makamu-Samia) hawajui masuala ya utawala bora? Hawakuangalia mgongano wa maslahi? Hapa kuna viongozi wa serikali ambayo inaonekana ina msimamo fulani halafu hao wanachagulia kuongoza bunge la katiba ambalo linategemea lisiegemee upande wowote je kweli hili linawezekana?

Kwangu mimi somo ninalojifunza hapa ni kwamba wengi wa wajumbe somo la utawala bora na mgongano wa maslahi bado halijawaingia na inaonekana hata wakiongea kwenye vyombo vya habari huwa wanaongea wasichokiamini.
 
Mchakato huu kuanzia ile sheria yenyewe ya Mabadiliko ya KATIBA tuliukosea sana. Kwa kuwa tulikuwa na "hamu kubwa" ya katiba mpya, haya ndio matokeo yake.

Watu wanadhani Samweli Sitta ataliongoza Bunge hili maalum kama alivyofanya kule Bunge la tisa la JMT. Wamekosea sana. Kule Bunge la JMT alisukumwa na kulipiza kisasi kwa Lowasa na Jakaya. Mazingira ambayo kwa sasa hayapo. Alipigwa chini alipotaka kugombea tena, akashika adabu, akajifunza. Ujasiri huo kwa sasa hatakuwa nao. Atabaki tu kushambuliana na akina Mtikila basi.
 
Mchakato huu kuanzia ile sheria yenyewe ya Mabadiliko ya KATIBA tuliukosea sana. Kwa kuwa tulikuwa na "hamu kubwa" ya katiba mpya, haya ndio matokeo yake.

Watu wanadhani Samweli Sitta ataliongoza Bunge hili maalum kama alivyofanya kule Bunge la tisa la JMT. Wamekosea sana. Kule Bunge la JMT alisukumwa na kulipiza kisasi kwa Lowasa na Jakaya. Mazingira ambayo kwa sasa hayapo. Alipigwa chini alipotaka kugombea tena, akashika adabu, akajifunza. Ujasiri huo kwa sasa hatakuwa nao. Atabaki tu kushambuliana na akina Mtikila basi.

Wildcard nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa. Lakini kinachonishangaza kwangu siyo wale wajumbe tu mle ndani, hata wachambuzi wa mambo ya siasa bado walikuwa wakishadidia uteuzi wa hawa mawaziri. Na kama ulivyosema kwamba Sitta anaweza asiwe na ujasiri kama wa zamani na pia Mama Samia yeye ndiyo kabisa. Sasa wachambuzi hata media zetu zilishindwa kuliona hilo?
 
Wildcard nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa. Lakini kinachonishangaza kwangu siyo wale wajumbe tu mle ndani, hata wachambuzi wa mambo ya siasa bado walikuwa wakishadidia uteuzi wa hawa mawaziri. Na kama ulivyosema kwamba Sitta anaweza asiwe na ujasiri kama wa zamani na pia Mama Samia yeye ndiyo kabisa. Sasa wachambuzi hata media zetu zilishindwa kuliona hilo?
Hapa mkuu Watz wengi tumeshaharibikiwa na sehemu ambayo ingelituokoa ni media, sasa huko nako ni pabovu zaidi ya hata sisi wanavijiji. Ndio kisa cha haya yote kutokea. Uwezekano wa kupata katiba ya kweli ni 30/70.

 
Wildcard nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa. Lakini kinachonishangaza kwangu siyo wale wajumbe tu mle ndani, hata wachambuzi wa mambo ya siasa bado walikuwa wakishadidia uteuzi wa hawa mawaziri. Na kama ulivyosema kwamba Sitta anaweza asiwe na ujasiri kama wa zamani na pia Mama Samia yeye ndiyo kabisa. Sasa wachambuzi hata media zetu zilishindwa kuliona hilo?
WaTanzania wachache sana wanafahamu namna CCM inavyofanya mambo yake ili iendelee kuwa madarakani. Tulipaswa kujiuliza kuanzia mwanzo kabisa ni nini kilimsukuma Jakaya kuitaka KATIBA MPYA ambayo haikuwa kwenye ILANI ya CCM wala haikupata kujadiliwa kwa kina kwenye vikao vyake.

Ikatungwa sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Bado hatukuona muundo kuanzia ule wa Tume ya Mabadiliko hadi huu wa Bunge Maalum la Katiba kama vilikuwa na kasoro. Mwenyekiti wa Bunge hili angalau alipaswa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa sio wa kuchaguliwa kwa ushabiki na makundi.

Vyombo vya habari nchi hii vipo kuripoti matukio tu. Afadhali kidogo TV zinajitahidi kwa mijadala ingawa waalikwa mara zote wanakuwa ni walewale.
 
hayo mbona yalikuwa yanafahamika, viongozi wote mpaka kwenye kamati za bunge hilo watatoka CCM kwa sababu ndiyo wanauwakilishi mkubwa, na ndiyo maana wanataka kura ya wazi tena simple majority ili wapitishe katiba ya CCM na sio katiba ya watanzania. WANANCHI TUJIPANGE KUDAI KATIBA YETU ENDAPO CCM WATAVURUGA MCHAKATO HUU.
 
[FONT=trebuchet
ms]Hapa mkuu Watz wengi tumeshaharibikiwa na sehemu ambayo ingelituokoa
ni media, sasa huko nako ni pabovu zaidi ya hata sisi wanavijiji. Ndio
kisa cha haya yote kutokea. Uwezekano wa kupata katiba ya kweli ni
30/70.

[/FONT]

huyo/hao asiye/wasio (ma)waziri bila kusimamishwa na CCM (w)angelipita?
 
WaTanzania wachache sana wanafahamu namna CCM inavyofanya mambo yake ili iendelee kuwa madarakani. Tulipaswa kujiuliza kuanzia mwanzo kabisa ni nini kilimsukuma Jakaya kuitaka KATIBA MPYA ambayo haikuwa kwenye ILANI ya CCM wala haikupata kujadiliwa kwa kina kwenye vikao vyake.

Ikatungwa sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Bado hatukuona muundo kuanzia ule wa Tume ya Mabadiliko hadi huu wa Bunge Maalum la Katiba kama vilikuwa na kasoro. Mwenyekiti wa Bunge hili angalau alipaswa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa sio wa kuchaguliwa kwa ushabiki na makundi.

Vyombo vya habari nchi hii vipo kuripoti matukio tu. Afadhali kidogo TV zinajitahidi kwa mijadala ingawa waalikwa mara zote wanakuwa ni walewale.


Nimeupenda huu uchambuzi kwa kweli. Hapo sasa Wildcard unaweza kujiuliza kuhusu viongozi wa vyama vya upinzani na vyama vya kijamii
 
Wildcard unavuta shuka wakati kunapambazuka? Nakubaliana na wewe kabisa kuwa Mwenyekiti angekuwa Jaji hata kama ni mstaafu. Sio kwamba CCM hawajui ila wanafanya makusudi ili waendelee kuwa madarakani milele. Kama haitaandikwa katiba ya wa TZ basi hali itajionyesha hata kabla bunge lenyewe halijakamilisha kikao chake. Wale wanaowakilisha wananchi mlw ndani tunataka tuwaone wakitutetea vinginevyo ni wale wale wa mfumo wa kichama!
 
huyo/hao asiye/wasio (ma)waziri bila kusimamishwa na CCM (w)angelipita?

Kama wachambuzi na media wangepasha sauti zao kwa nguvu kupinga mawaziri na watu wa vyama kuongoza hilo bunge, kuna uwezekana mkubwa CCM wasingekaa kama caucus ili wateue mtu mmoja
 
Mchakato huu kuanzia ile sheria yenyewe ya Mabadiliko ya KATIBA tuliukosea sana. Kwa kuwa tulikuwa na "hamu kubwa" ya katiba mpya, haya ndio matokeo yake.

Watu wanadhani Samweli Sitta ataliongoza Bunge hili maalum kama alivyofanya kule Bunge la tisa la JMT. Wamekosea sana. Kule Bunge la JMT alisukumwa na kulipiza kisasi kwa Lowasa na Jakaya. Mazingira ambayo kwa sasa hayapo. Alipigwa chini alipotaka kugombea tena, akashika adabu, akajifunza. Ujasiri huo kwa sasa hatakuwa nao. Atabaki tu kushambuliana na akina Mtikila basi.
mchakato ulipofikia haususiki tena - tumeshayavulia nguo.....
 
Tatizo kubwa ni kwamba baadhi ya Watanzania wanapenda kushabikia mambo yasiyo ya maana na kubeza mambo ya msingi. Uenyekiti wa bunge la katiba sasa umekuwa ni mtu siyo taasisi. Watu wamepata ugonjwa unaoitwa Sitta-mania.. Kuanzia wachambuzi, waandishi wa habari, wanasiasa na baadhi ya wananchi. Wengine wamefikia kiwango cha juu cha huu ugonjwa kiasi cha kuona anafaa Urais kisa ushabiki. Wamepata upofu kiasi cha kushindwa kuona kuwa yeye ni kizazi kile kile kilichotufikisha hapa tulipo kama nchi. 'We need to grow up seriously..'
 
Tatizo kubwa ni kwamba baadhi ya Watanzania wanapenda kushabikia mambo yasiyo ya maana na kubeza mambo ya msingi. Uenyekiti wa bunge la katiba sasa umekuwa ni mtu siyo taasisi. Watu wamepata ugonjwa unaoitwa Sitta-mania.. Kuanzia wachambuzi, waandishi wa habari, wanasiasa na baadhi ya wananchi. Wengine wamefikia kiwango cha juu cha huu ugonjwa kiasi cha kuona anafaa Urais kisa ushabiki. Wamepata upofu kiasi cha kushindwa kuona kuwa yeye ni kizazi kile kile kilichotufikisha hapa tulipo kama nchi. 'We need to grow up seriously..'


Hatiwezi kukua kama vijana wetu wanalipwa ili kuteta uovu, na pili tunaowategemea waandishi wahabari wapo radhi apokee bahasha ya khaki lakini si kusema ukweli.
 
Mleta mada,

Fact 1: CCM ndio ilikuwa na watu wenye sifa kugombea nafasi zote mbili, uenyekiti na makamu mwenyekiti. Sifa hizo zili-range kuanzia elimu mpaka uzoefu wa kuendesha mabunge. Wapinzani siwalaumu kushindwa kwao kusimamisha mgombea kwa kuwa hawana, narudia, hawana mtu mwenye sifa.

Fact 2: CCM ni chama tawala na probably ndio chama chenye kuaminiwa zaidi na wale wajumbe 201. Hivyo, mbali na wale wajumbe kuwa ni wana CCM huenda kabisa wakawa wapenzi wakubwa wa CCM. Hivyo, kivyovyote mgombea wa CCM alikuwa ashinde kwa kishindo.

Fact 3: Wapinzani wana jiaminisha kuwa mhe. Sitta ni msimamia usawa bungeni na hana upande hivyo atatoa fursa sawa kwa wote. Jamani, hata mzee Kificho mwenyewe alikua akitoa fursa kwa mawaziri na wabunge wa CCM kwa kiasi kikubwa na hata maamuzi yake yaliendeshwa kwa misingi hiyo. Hakuna usawa pale, ni kusimamia msimamo wa chama tu.
 
Mleta mada,

Fact 1: CCM ndio ilikuwa na watu wenye sifa kugombea nafasi zote mbili, uenyekiti na makamu mwenyekiti. Sifa hizo zili-range kuanzia elimu mpaka uzoefu wa kuendesha mabunge. Wapinzani siwalaumu kushindwa kwao kusimamisha mgombea kwa kuwa hawana, narudia, hawana mtu mwenye sifa.

Fact 2: CCM ni chama tawala na probably ndio chama chenye kuaminiwa zaidi na wale wajumbe 201. Hivyo, mbali na wale wajumbe kuwa ni wana CCM huenda kabisa wakawa wapenzi wakubwa wa CCM. Hivyo, kivyovyote mgombea wa CCM alikuwa ashinde kwa kishindo.

Fact 3: Wapinzani wana jiaminisha kuwa mhe. Sitta ni msimamia usawa bungeni na hana upande hivyo atatoa fursa sawa kwa wote. Jamani, hata mzee Kificho mwenyewe alikua akitoa fursa kwa mawaziri na wabunge wa CCM kwa kiasi kikubwa na hata maamuzi yake yaliendeshwa kwa misingi hiyo. Hakuna usawa pale, ni kusimamia msimamo wa chama tu.


Na CCM wanatumia vilivyooo facts zako kufanikishaa malengoo yao..
Tukubali kazi ya kuimarisha upinzani dhidi ya CCM bado ni kubwa pamoja na malalamikoo yote ya kukua kwa umaskini na kukosekana miundo mbinu ya kuwezesha fursa zizilzopo kutumika kwa ajili ya kuharakisha maendeleo nchini.
 
hayo mbona yalikuwa yanafahamika, viongozi wote mpaka kwenye kamati za bunge hilo watatoka CCM kwa sababu ndiyo wanauwakilishi mkubwa, na ndiyo maana wanataka kura ya wazi tena simple majority ili wapitishe katiba ya CCM na sio katiba ya watanzania. WANANCHI TUJIPANGE KUDAI KATIBA YETU ENDAPO CCM WATAVURUGA MCHAKATO HUU.

Mkuu hapa hakuna suala la endapo. Ni dhahiri kwamba tayari CCM walishavuruga Mchakato huu kwa kuhakikisha wanapanga safu yao kuanzia kutungwa kwa sheria, kanuni za Bunge na sasa uchaguzi. Huwezi kuwa na Spika ambaye ni Waziri na Makamu wake ni waziri tena wa Muungano ukategemea Katiba inayotakiwa na wananchi. Tutapata Katiba inayotakiwa na watawala.
 
Na CCM wanatumia vilivyooo facts zako kufanikishaa malengoo yao..
Tukubali kazi ya kuimarisha upinzani dhidi ya CCM bado ni kubwa pamoja na malalamikoo yote ya kukua kwa umaskini na kukosekana miundo mbinu ya kuwezesha fursa zizilzopo kutumika kwa ajili ya kuharakisha maendeleo nchini.

Tunapokubali kuwa kazi ya kuimarisha upinzani bado ni kubwa, tukubali pia kuwa usalama wa Taifa hili, unaopaswa kusimamia maslahi ya wananchi bado nao unahitaji kuimarishwa kwa kuongezewa ari ya uzalendo. Katika Mchakato huu tulikosea katika kutunga sheria. Laiti sheria ingetamka kuwa Mwenyekiti wa Bunge awe ni mtu asiyetokana na chama cha siasa na awe Jaji wa Makahama Kuu au ya Rufaa, ni dhahiri tungepata Katiba nzuri maana maadili ya Jaji yanafahamika kama kweli akiamua kutenda haki kwa mjibu wa maadali ya nafasi yake. Katiba iliyotawaliwa na ushabiki wa kisiasa, tutapata katiba ya wanasiasa!
 
Back
Top Bottom