Kosa la huyu mwanaume ni nini?

Kuna jamaa yangu/rafiki yangu kipenzi ana hali ngumu nyumbani kwake ikanibidi niamue kuingia JF kusaka msaada wa ki-mawazo,ijumaa jioni jamaa alipotoka kazini alipitia sehemu akapata Bia zake tatu hivyo mpaka anainingia nyumbani iilikuwa kwenye saa mbili na nusu,alipoingia akasalimiana na mkewe akaenda kuoga then akarudi sitting room akimsubiri mkewe amuite kwenye meza tayari kwa chakula,ghafla ikawa kinyume aliyekuja kumuita ni House girl wake, baada ya kumuambia chakula tayari wakati akiondoka yule jamaa akamwambia "siku hizi unanenepa" yule H/girl hakujibu kitu,kumbe mama watoto kamsikia,yaani ugomvi uliozuka hapo mpaka leo hii hawaongei,sasa waungwana wa JF huyu jamaa kakosea wapi?

Hilo ndio kosa lake.
 
halafu nimeshakugundua wewe.....vitu vingi sana tunaendana.....


Kwani anapowasifia mabaamedi huko alikokuwa anakunywa bia unakuwepo? By the way, hapo hakuongea yeye, ziliongea bia tatu... na zingekuwa nne lazima zingapapasa bambataa, zingekuwa tano, jamaa angekuwa lupango saa izi...
 
Shwaini kabisa, mke naye kayataka mwenyewe...........ilimpasa amkaribishe mwenyewe mumewe chakula. Huyo hausigeli hataipataje.............atapewa likizo haraka sana, japo sio kosa lake lakini nani kamwambia anenepe hovyo na kujitingisha mbele ya bosi wake
 
Kosa ni kumsifia hausigelo, mwambie asirudie tena kwani maza hausi hapendi
 
Kosa ni kumsifia hausigelo, mwambie asirudie tena kwani maza hausi hapendi

Unajua jamaa anajiteteaje vipi lakini bado haleweki,anasema kuwa kumwambia mtu umenenepa sio kumsifia kwani mtu kuwa mnene ni sifa?yeye alimaanisha kuwa kanenepa tu tofauti na alivyokuwa zamani lakini sio kwamba kasifia.
 
Preta taratibu
mambo haya mnayalea wenyewe
we mke umekaa jikoni huko unafanya mambo yako au sijui uko wapi unamuachia house gal kuja kuniitia chakula
Sifa nitatoa kwake maana ungekuja mwenyewe ningekupa hiyo sifa wewe na wala nisingemuona house gal kuwa kanenepa
Hapo na akija kesho yake namwambia tena duh una mwanya mzuri hata kama hanao ili uzidi kupasuka
Mnawapa air time wenyewe wakiingia hewani mnaaanza kulalamika
(sorry kuna mtu kaiba paswedi yangu hapa )

Mmmmh!!!! dah kuishi na mwanaume ni kipaji!!!!
 
Huyo mwanaume hana adabu kabisa!unene wa housegirl unamuhusu nini?tena si ajabu alikua anamwambia huku anajichekesha shenz type!acha anuniwe hadi akome..
 
pombe hizo mwana , ila umekosea kichizi mkali..next tm, uwe hata unachungulia jikoni kama mama watoto yupo ndo uongee na beki tatu maneno kama hayo..
 
wivu tu wa kijinga huo
kwani kumwambia kanenepa ndio anamtaka?
ajiulize anapokuwa bar anakuwa nae huko?
acheni hizo utani ni kawaida ktk nyumba.huyo anune hadi apasuke
nahisi ni mbaya kuliko dada wa ndani ndio maana anajisikia vibaya na hajiamini
 
Kuna jamaa yangu/rafiki yangu kipenzi ana hali ngumu nyumbani kwake ikanibidi niamue kuingia JF kusaka msaada wa ki-mawazo,ijumaa jioni jamaa alipotoka kazini alipitia sehemu akapata Bia zake tatu hivyo mpaka anainingia nyumbani iilikuwa kwenye saa mbili na nusu,alipoingia akasalimiana na mkewe akaenda kuoga then akarudi sitting room akimsubiri mkewe amuite kwenye meza tayari kwa chakula,ghafla ikawa kinyume aliyekuja kumuita ni House girl wake, baada ya kumuambia chakula tayari wakati akiondoka yule jamaa akamwambia "siku hizi unanenepa" yule H/girl hakujibu kitu,kumbe mama watoto kamsikia,yaani ugomvi uliozuka hapo mpaka leo hii hawaongei,sasa waungwana wa JF huyu jamaa kakosea wapi?
Wote wanamakosa
Mume Kakosea sana na kaonyesha dhalau kwa mkewe,na pia mkewe nae kakosea sana kumuagiza"AMIR MAFTAH"kwenda kumkaribishia mumewe mezani.
 
Mi naona vitu vingine si rahisi kujugde mpaka uwe kwenye eneo la tukio.
Huyo baba anaweza kuwa na kosa au la.
Voice tone aliyoitumia kusema hayo maneno na jinsi alivyokua akimwangalia huyo binti wakati akiyasema hayo ndio inaweza ikakufanya mtu ujue mmmmh huyu tayari anamtamani housegirl au kamwambia tu.
Jamani sio dhambi baba kuongea na housegirl cha msingi ni wanaongea vipi tu,dada naye ni binadamu na anapokua nyumbani kwako ni kama tu sehemu ya familia hivyo sio kila baba akiongea au kucheka naye tu iwe tatizo.
 
amekosea ndio....
Mnaanzaga hivyo hivyo...
Oooh umenenepa.......
Kesho utamwambia ana mikono mizuri....
Keshokutwa utamsifia kijungu.....
Mwisho uuze mechi
 
na nyie wanaume,hebu punguzeni uvivu,aah.kwani kuna shida gani ya kuuliza jee niwasaidie kitu gani,au kama chakula tayari,ningependa kukichukua mwenyewe kukiweka mezani.wewe umetoka kazini,moja kwa moja baa.huyo mke inaonyesha hiyo ni kama sababu tu ya kulalamika.ila ana masononeko mengine.hebu wapeni attention wake zenu,mnatakiwa na nyinyi wanaume mfundwe

triple like
 
Mmmmh!!!! dah kuishi na mwanaume ni kipaji!!!!

tena jipaji cha hali ya juu...
Wote mmetoka ofisini, wewe utapita kwenye biashara then utarudi nyumbani uandae chakula, umwandalie nguo zako, zake za watoto, home work ya watoto, usimamie watoto waoge, wale nk.....

Yeye atapita bar, anyweeeee arudi nyumbani akae sebuleni akusubiri umwandalie maji ya kuoga na hguo then akakae sebuleni, asubiri umuite akale maana .......

Mbaya zaidi inabidi umchunge akipata upenyo tu ataflirt na hg.........

Kweli kuolewa si lelemama...
 
wivu tu wa kijinga huo
kwani kumwambia kanenepa ndio anamtaka?
ajiulize anapokuwa bar anakuwa nae huko?
acheni hizo utani ni kawaida ktk nyumba.huyo anune hadi apasuke
nahisi ni mbaya kuliko dada wa ndani ndio maana anajisikia vibaya na hajiamini
Hata mim kama najua nimekamilika kushinda housegirl wangu wala sitaona tatizo akisifiwa.
Tatizo unakua mwanamke kama Lucy Kibaki unaenda kuleta kabinti ka Jocate hapo lazima hata kama baba wa watu hayuko huko wee utadhani anamtamani tu.
Tatizo jengine watu wanawachulia mahousegirl kama maadui,hapo huyo binti cha moto anakiona.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom