Korea Kaskazini kurusha kombora kwenda mwezini!

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,399
Nchi ya Korea kaskazini inafanya maandalizi kurusha kombora la majaribio ambalo limebeba kituo cha satelite kwa ajili ya kutoa taarifa za hali ya hewa.

Viongozi wa kijeshi ambao wamekuwa wakifanya matayarisho ya majaribio wamesisitiza kwamba majaribio ya urushaji wa kombora hilo ni katika kuhakikisha kwamba makombora hayo yana uwezo wa kufikia maeneo ambayo itakuwa ni rahisi kujibu mashambulizi ya nchi maadui.

Kombora hili litarushwa kutoka katika kituo cha Sohae kilichopo karibu na mpaka na nchi ya China ambako maandalizi ya kombora hilo lenye urefu wa mita 30 na liitwalo Unha-3 yalikuwa yakifanywa. Sehemu hiyo ni ileile ambayo majaribio ya awali yalifanywa. Urushaji wa kombora hilo unatarajiwa kufanywa kati ya April 12 na 16.

Siku ya Jumapili waandishi kadhaa wa kigeni walipewa nafasi ambayo ni nadra sana kutolewa, kutembelea kituo hicho na wakajionea wenyewe maandalizi ya urushaji huo wa kombola la Unha-3.

Urushaji wa kombora hilo kwa mujibu wa mkurugenzi wa kituo hicho ni katika sehemu ya sherehe ya kutimiza miaka 100 kwa kiongozi muasisi wa kwanza wa nchi hiyo Kim II Sung ambae pia mwanae Kim iL Jong alifariki mwezi December mwaka jana na mjukuu wake (Kim iL Sung) Kim Jong Un akatwaa madaraka.

nk-3.jpg


Eneo la maandalizi likiwa limekamilika

Nchi za US, Korea ya Kusini na Japan zimelaani mipango hiyo na kusema kwamba Korea Kaskazini inaficha azma yake ya kutupa makombora ya nyuklia, lakini China imesema maneno machache mno kuzingatia kwamba ni wachina wenyewe ndio wanaowapa Korea kskazini technolojia ya kutengeneza makombora hayo.

Nchi za Japan na Korea Kusini zimetoa onyo kwamba endapo mabaki ya kombora hilo yataelekea kwenye anga zao watajibu kwa kupiga makombora yao ambayo yataharibu kabisa mabaki hayo kitendo ambacho hakijawastua kabisa Korea Kaskazini.

Hofu tayari imezuka katika eneo lote la kipande cha Korea au Korean Peninsula) ambao lipo katika eneo zima la Asia Mashariki. Eneo hili limeundwa na pande la ardhi lenye urefu wa kilomita karibu 1100 na linalala likielekea kwenye bahari ya Pasific.

Upande wa mashariki eneo hili limezungukwa na bahari ya Japan na magharibi limezungukwa na bahari ya njano katikati pakiwa na pande la ardhi la Korea ambalo linaunganisha bahari hizo mbili.

Kabla ya vita kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini kwisha mwaka 1953 nchi hizi mbili zilikuwa ni kaichi kamoja na ni mkataba wa Armistice ndio unaotoa fursa kwa kila nchi kuwa huru na mambo yake Korea Kaskazini wakishikilia ukomunisti ambao unafadhiliwa na China na Russia na Korea Kusini kufuata ubepari ambao leo hii umeifanya nchi hiyo kuwa na soko kubwa na bidhaa za kitechnolojia zikiwemo za Samsung na LG.

Pia nchi ya Korea Kusini imewekeza sana kwenye elimu na ni nchi ambayo wananchi wake wote wanapata matangazo ya televisheni kupitia kwenye magari yao ambayo inaitwa DMB au digital Multimedia Broadcasting, pia ndio nchi ambayo inatengeneza magari maarufu na yenye bei nafuu ya KIA na Hyundai.
 
Ni haki kwa Korea ya kaskazin kufanya majaribio yao,hakuna hata siku moja Usa imehojiwa kuhusu technolojia yake ya kivita ndio maana umoja wa mataifa hautaweza kuzuia mataifa mengine kujaribu technolojia za kijeshi kwa kua mataifa haya yanaona UN kama chombo kandamizi na kinachoipendelea USA.
 
ss-120326-misp-01.grid-9x2.jpg


Washirika wakiwa mwezini.

Tarehe 25 March mwaka huu Russia ilirusha kombora lililobeba chombo cha US kiitwacho US Intelsat-22 satellite kutoka kwenye kituo chake kilichopo nchini Kazakhstan kiitwacho Russian-leased Baikonur cosmodrome. Hatua hiyo itaifanya kampuni ya Intelsat Corp kuwa na uwezo wa kufanya mawasilano yenye uhakika.

Chombo hiki cha Intelsat-22 kimeundwa na kampuni ya US iitwayo Boeing Space System.

Sasa je vipi kuhusu Korea Kaskazini kurusha chombo chao kwa ajili tu ya kupata taarifa za hali ya hewa?
 
Mkuu kitu ambacho huwa kinanikela zaidi ni hizi nchi za magharibi kujaribu ku-muzzle nchi nyingine katika mambo ya kisayansi na technolojia. Wana propaganda za ajabu sana, kwa mfano: Korea Kusini nayo utengeneza roketi za kwenda into outer space, Japan vile vile na actually nchi hiyo ya Japan ina technolojia ya kuhunda makombora ya nuclear-why pick on DPRK.

Mbinu hizo hizo ndizo zinatumika kuisakama IRAN awataki nchi hiyo ipige hatua katika nyanja za Hi-Tech, wanatoa visingizio chungu mzima kutisha watu kuhusu nchi hiyo kurutubisha nuclear feul-lakini wanakingia kifua Israel isikaguliwe vinu vyake vya nuclear vilivyo jengwa kwenye jangwa la NEGEV-cha ajabu International Community ina-swallow a bait and a sinker za propaganda za watu hawa wa magharibi.
 
Frankly we are going to die soon if we cannot cope the current world challenges BY HARNESSING our own resources. See N. KOREA..............

By CHOE SANG-HUN
Published: April 10, 2012

SEOUL, South Korea — North Korea said on Tuesday that it had completed preparations to launch a satellite into orbit, as South Korea and other Asian nations told their airlines and ships to change their routes to avoid the North Korean rocket.

Mr. Ryu said North Korea would launch the satellite as scheduled. When asked about the chances of persuading North Korea to change its mind, Victoria Nuland, a spokeswoman of the United States State Department, said on Monday: “We’re not in the hope business here. We’re simply making clear we think this would be a very bad idea.”

North Korea told international aviation authorities that its rocket would blast off from its launching station near its northwestern border with China between 7 a.m. and noon and fly southward. Its first-stage section is expected to fall in the sea about 90 nautical miles off Kunsan, a city on the South Korean west coast. The second-stage section is expected to hit the waters east of the Philippines.

In Washington, Jay Carney, the White House spokesman, warned that if the North went ahead with the satellite launching, the United States would probably cancel promised food aid shipments and would “continue to do the things that we have been doing in the past to isolate and pressure North Korea.”

In the 2009 launching, experts said the first two stages of the North’s Unha-2 launch rocket appeared to have worked but the third stage did not ignite. Looking at the photos filed by reporters from the North Korean launching site, they said that the North’s new Unha-3 rocket appeared very similar to the Unha-2, indicating that North Koreans were continuing to improve the technology they tested in 2009.
 
kAKA NASI TUANGALIE WAPI NCHI YETU ILIJIKWA NI KATIKA SIASA, SAYANSI AU KUTOTAMBUA WATAALAM WENGI TULIONAO. KILA KITU KINAWEZEKANA. HATA CHURA ANAPELEKWA MAREKANI??????????????????????? INAUMA SANA
 
DPRKwako serious sana kuhusu huu mpango wao wa kurusha satelite,na wanaapa kuwa yeyote atakayejaribu ku-intercept route ataadhibiwa vikali
 
Updates:

Korea kaskazini imekwishajitayarisha kwa shughuli pevu la kurusha kombora lake kuelekea mwezini.

OB-SO015_0411nk_G_20120411073822.jpg

Luninga la kuangalilia mwenendo wa kombora hilo ikiwa tayari kwenye kituo cha satelite nje kidogo wa mji mkuu wa Pyongyang.

Korea Kaskazini wamesema yoyote atakaejaribu kutungua mabaki ya kombota hilo yatakapokuwa yakirudi duniani atakuwa anatafuta vita.

Nchi nyingi zilizoendelea zikiongozwa na US zinaamini kwamba kombora hilo ni la masafa marefu kuweza kufikia US na na maeneo mengine.

Maofisa wa Korea Kaskazini wamesema vituo vya kimataifa vya anga na majini vimearifiwa juu ya zoezi hilo na mashirika ya ndege ya Japan, Phillipines na Korea Kusini yamekwishjiandaa kwa kutafuta njia mbadala za kupita ndege.
 
mbona heading inasema wamerusha? Hata mimi najua bado laki heading inachanganya kidogo.
 
Nchi ya Japan imejiandaa kukabiliana na hali yoyote ile ya mabaki ya kombora litakalorushwa kwenda mwezini yasije yakadondokea nchini humo.

US ambayo ina kambi zake za jeshi katika pande zote za bahari ya Pacific, nayo imejiweka kwenye hali ya tahadhari.

2012041000360_0.jpg

Kifaa cha kuzuia kombora kiitwacho Patrioty Advanced Capability- 3 kutoka ardhini kwenda angani kikiwa tayari kutumika kwenye kituo cha kijeshi nje kidogo ya mji wa Tokyo.

Wakati huohuo Korea Kaskazini imesema kitendo cha kombora hilo kurushwa hadi kufikia Orbit na kuweka satelite itachukua kama dakika kumi 10 kukamilisha zoezi zima.

Akiongea na waandishi wa habari mjini Pyongyang naibu mkurugenzi wa kituo cha mambo ya anga cha Korea Kaskazini bwana Ryu kum-Ch, amesema technolojia inayotumika sasa ni tofauti na ile iliyotumika mwaka 2009 ilifanya zoezi hilo kutumia muda mchache zaidi wa dakika kati ya 4 na 6 kukamilika kabla ya mabaki kuanguka.

2012041100552_0.jpg

Ryu kum-Chol naibu mkurugenzi wa kituo cha technolojia cha Korea Kaskazini akiongea na waandishi kutoka vyombo mbalimbali ya habari duniani mjini Pyongyang.
 
Pentagon has said that the North Korean long-range rocket broke apart moments after launch...Details being awaited from observatory.

120409031843-north-korea-missile-check-t1-main.jpg
 
Pyongyang, North Korea (CNN) -- Defying warnings from the international community, North Korea launched a long-range rocket on Friday, but it appears to have broken apart before escaping the earth's atmosphere, officials said.
No element of the rocket reached space, said a U.S. official, who based that conclusion on data collected by the United States from its first few moments aloft.
"This was supposed to be associated with (Kim Jong Un's) ascension to power. So for this thing to fail ... is incredibly embarrassing," said Victor Cha, former director of Asian affairs for the U.S. National Security Council and now a Georgetown University professor.
 
_59590922_hpasmskw.jpg


North Korea confirms its controversial rocket launch failed, as observers report it broke up and crashed into the sea shortly after blast-off.
BBC News - North Korea rocket launch fails

Hawa jamaa raia wao hawana chakula badala ya kushughulikia maendeleo ya raia wanashughulikia maendeleo ya silaha. Ukitoka nchi masikini hata kufikiri kwako ni tatizo pia.
 
Back
Top Bottom