Korea Kaskazini yawataka raia wake wafuge mbwa kwa ajili ya nyama

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
Serikali ya Korea Kaskazini imepiga marufuku wananchi wake kufuga mbwa na kuishi nao kama sehemu ya familia, badala yake wametakiwa kufuga kwa ajili ya kula nyama na kuchuna ngozi yake.

Tangazo la kupiga marufuku ufugaji wa mbwa kama wanyama pendwa wa kuzurura nao mitaani, lilitolewa kwenye mkutano wa Umoja wa Wanawake wa Kisoshalisti wa Korea kwenye jimbo la kusini la Pyongan lililopo kaskazini mwa mji mkuu wa Pyongyang. Korea Kaskazini inaongozwa na Kim Jong Un.

Akizungumza na gazeti la Daily NK la nchi jirani ya Korea Kusini, mmoja wa wanaharakati (bila kutaja jina lake) aliorodhesha makosa ambayo mmiliki wa mbwa anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria na Serikali ikiwamo ufugaji mbwa kama mwanafamilia.

“Kumfanya mbwa kama sehemu ya familia, kula na kulala naye kwenye familia ni kinyume na maelekezo ya serikali na kunatakiwa kuepukwa,” alisema mtoa taarifa.

Pia, alisema makosa mengine ni kumvalisha mbwa nguo, kama alivyofanya Paris Hilton wa Marekani kwa mbwa wake. Paris Hilton aliyezaliwa Februari 17, 1981 ni mfanyabiashara, mwanamitindo, mwimbaji, DJ, na mwigizaji ambaye familia yake ndiyo inamiliki mtandao wa hoteli za Hilton duniani kote.
 
Km aambiwe wenzie kusini wameacha kula nyau na wow,hata kama njaa yupo rafiki yake atampa ngano na mazao mengine ya kilimo,au hata ni bora akampa dubu ila sii wow🤪
 
Serikali ya Korea Kaskazini imepiga marufuku wananchi wake kufuga mbwa na kuishi nao kama sehemu ya familia, badala yake wametakiwa kufuga kwa ajili ya kula nyama na kuchuna ngozi yake.

Tangazo la kupiga marufuku ufugaji wa mbwa kama wanyama pendwa wa kuzurura nao mitaani, lilitolewa kwenye mkutano wa Umoja wa Wanawake wa Kisoshalisti wa Korea kwenye jimbo la kusini la Pyongan lililopo kaskazini mwa mji mkuu wa Pyongyang. Korea Kaskazini inaongozwa na Kim Jong Un.

Akizungumza na gazeti la Daily NK la nchi jirani ya Korea Kusini, mmoja wa wanaharakati (bila kutaja jina lake) aliorodhesha makosa ambayo mmiliki wa mbwa anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria na Serikali ikiwamo ufugaji mbwa kama mwanafamilia.

“Kumfanya mbwa kama sehemu ya familia, kula na kulala naye kwenye familia ni kinyume na maelekezo ya serikali na kunatakiwa kuepukwa,” alisema mtoa taarifa.

Pia, alisema makosa mengine ni kumvalisha mbwa nguo, kama alivyofanya Paris Hilton wa Marekani kwa mbwa wake. Paris Hilton aliyezaliwa Februari 17, 1981 ni mfanyabiashara, mwanamitindo, mwimbaji, DJ, na mwigizaji ambaye familia yake ndiyo inamiliki mtandao wa hoteli za Hilton duniani kote.
Kamwenee🙂
 
Wenzako wanakula hio kitu wanaishi miaka 100 sasa wewe unajivunia uislam wastani wa maisha yako miaka 40 maradhi kibao hadi kifoo
Kuna uhusiano gani mkuu kula mbwa eti uishi miaka 100 na usile uishi umri mdogo, elimu yako ni ipi
Unataka kuniambia wewe unakunywa supu ya mbwa?
 
Serikali ya Korea Kaskazini imepiga marufuku wananchi wake kufuga mbwa na kuishi nao kama sehemu ya familia, badala yake wametakiwa kufuga kwa ajili ya kula nyama na kuchuna ngozi yake.

Tangazo la kupiga marufuku ufugaji wa mbwa kama wanyama pendwa wa kuzurura nao mitaani, lilitolewa kwenye mkutano wa Umoja wa Wanawake wa Kisoshalisti wa Korea kwenye jimbo la kusini la Pyongan lililopo kaskazini mwa mji mkuu wa Pyongyang. Korea Kaskazini inaongozwa na Kim Jong Un.

Akizungumza na gazeti la Daily NK la nchi jirani ya Korea Kusini, mmoja wa wanaharakati (bila kutaja jina lake) aliorodhesha makosa ambayo mmiliki wa mbwa anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria na Serikali ikiwamo ufugaji mbwa kama mwanafamilia.

“Kumfanya mbwa kama sehemu ya familia, kula na kulala naye kwenye familia ni kinyume na maelekezo ya serikali na kunatakiwa kuepukwa,” alisema mtoa taarifa.

Pia, alisema makosa mengine ni kumvalisha mbwa nguo, kama alivyofanya Paris Hilton wa Marekani kwa mbwa wake. Paris Hilton aliyezaliwa Februari 17, 1981 ni mfanyabiashara, mwanamitindo, mwimbaji, DJ, na mwigizaji ambaye familia yake ndiyo inamiliki mtandao wa hoteli za Hilton duniani kote.
Nchi inayoongozwa na wavuta bange.
 
Daa,mbona kulazimishwa kutenda uovu....mbona unyama sana huo
Mila za watu hizo .... Unajua Korea Kusini amepiga marufuku lini!?? ..... January 2024, lakini SHERIA itaanza kufanya kazi mwaka 2027. Vipi Bado una swali!!?
 
Nchi inayoongozwa na wavuta bange.
Haujui kitu Kaa kimya ndugu..... Vipi na Hawa ndugu zenu waKorea Kusini nao ni wavuta bange!??? ..... Mkishalishwa propaganda mnazibeba kama dekio...... Korea Kusini ni wabepari wenzenu!?? ....hao hapo.... Wamepotisha SHERIA January,2024 lakini itaanza kutumikia 2027 ...Kwa nini!??.....
 

Attachments

  • Screenshot_20240315-102300.jpg
    Screenshot_20240315-102300.jpg
    347.4 KB · Views: 2
Kuna uhusiano gani mkuu kula mbwa eti uishi miaka 100 na usile uishi umri mdogo, elimu yako ni ipi
Unataka kuniambia wewe unakunywa supu ya mbwa?
Hizo ni Mila zao ....mnashindwa Nini kuheshimu Mila na tamaduni za watu!?? hapo south Korea tu bepari mwenzenu wanakuja mbwa haohao.... Wakila wa kaskazini mnadharau!?? Ficheni basi ujinga hata kidogo...
 
Kumfanya mbwa kama sehemu ya familia, kula na kulala naye kwenye familia ni kinyume na maelekezo ya serikali na kunatakiwa kuepukwa,” alisema mtoa taarifa.
Naunga mkono hoja, kama huwezi kula nyama ya mbwa basi mfanye awe mlinzi tu lakini sio mwanafamilia ni ujinga wa hali ya juu kabisa.
 
Back
Top Bottom