Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Serikali ya Korea Kaskazini imepiga marufuku wananchi wake kufuga mbwa na kuishi nao kama sehemu ya familia, badala yake wametakiwa kufuga kwa ajili ya kula nyama na kuchuna ngozi yake.
Tangazo la kupiga marufuku ufugaji wa mbwa kama wanyama pendwa wa kuzurura nao mitaani, lilitolewa kwenye mkutano wa Umoja wa Wanawake wa Kisoshalisti wa Korea kwenye jimbo la kusini la Pyongan lililopo kaskazini mwa mji mkuu wa Pyongyang. Korea Kaskazini inaongozwa na Kim Jong Un.
Akizungumza na gazeti la Daily NK la nchi jirani ya Korea Kusini, mmoja wa wanaharakati (bila kutaja jina lake) aliorodhesha makosa ambayo mmiliki wa mbwa anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria na Serikali ikiwamo ufugaji mbwa kama mwanafamilia.
“Kumfanya mbwa kama sehemu ya familia, kula na kulala naye kwenye familia ni kinyume na maelekezo ya serikali na kunatakiwa kuepukwa,” alisema mtoa taarifa.
Pia, alisema makosa mengine ni kumvalisha mbwa nguo, kama alivyofanya Paris Hilton wa Marekani kwa mbwa wake. Paris Hilton aliyezaliwa Februari 17, 1981 ni mfanyabiashara, mwanamitindo, mwimbaji, DJ, na mwigizaji ambaye familia yake ndiyo inamiliki mtandao wa hoteli za Hilton duniani kote.
Tangazo la kupiga marufuku ufugaji wa mbwa kama wanyama pendwa wa kuzurura nao mitaani, lilitolewa kwenye mkutano wa Umoja wa Wanawake wa Kisoshalisti wa Korea kwenye jimbo la kusini la Pyongan lililopo kaskazini mwa mji mkuu wa Pyongyang. Korea Kaskazini inaongozwa na Kim Jong Un.
Akizungumza na gazeti la Daily NK la nchi jirani ya Korea Kusini, mmoja wa wanaharakati (bila kutaja jina lake) aliorodhesha makosa ambayo mmiliki wa mbwa anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria na Serikali ikiwamo ufugaji mbwa kama mwanafamilia.
“Kumfanya mbwa kama sehemu ya familia, kula na kulala naye kwenye familia ni kinyume na maelekezo ya serikali na kunatakiwa kuepukwa,” alisema mtoa taarifa.
Pia, alisema makosa mengine ni kumvalisha mbwa nguo, kama alivyofanya Paris Hilton wa Marekani kwa mbwa wake. Paris Hilton aliyezaliwa Februari 17, 1981 ni mfanyabiashara, mwanamitindo, mwimbaji, DJ, na mwigizaji ambaye familia yake ndiyo inamiliki mtandao wa hoteli za Hilton duniani kote.