NewDawnTz
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 1,667
- 362
Kuna tetesi ambazo zimeanza kuzagaa huku niliko (Dom) na jana niliisikia nikapuuzia lakini leo asubuhi hii nimepita mitaa fulani nikasikia watu tena wanazungungumzia habari ya kuwepo na kongamano mbadala la ku-justify kutokuwepo haja ya kufanya mabadiliko ya katiba kwa kipindi cha karibuni kwa kuuonesha umma kuwa wanaolilia katiba mpya ni watu wenye haraka na walioko nje ya system na hawajui ugumu ulioko kwenye kuandika katiba mpya
Mpango wenyewe unazungumziwa kuhusisha pia taasisi ya mojawapo ya elimu ya juu na "wataalamu wa mambo ya katiba" ili kupangua hoja mbalimbali zinazoendelea ku-justify haja ya kuwepo na katiba mpya. Hata hivyo haijawa clear zaidi ni chuo kipi kitatumika kuandaa mpango husika na hao watakaotumika ni wakina nani ila inadaiwa mpango kamambe upo jikoni kwa ajili ya kuweka haya.
Mtazamo wangu: Japo kuwa tetesi hazina haja ya kuzifuatilia lakini naanza kuona hizi zinaweza kuwa na uzito wake maana kama jana nimezisikia kwa mtu niliesoma nae chuo na ni mtu ambae ni kada wa karibu na baba yake aliwahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa mmojawapo kanda ya ziwa na yeye ngazi za jengo la chama anazijua hadi idadi yake
Pia naweza kuhisi uko usahihi katika hili kwa kuangalia namna ambavyo TBC1 walivyoripoti Kongamano la UDASA jana
Kama hili jambo ambalo ni tetesi ni sahihi na huo mpango upo, basi bado watanzania tuna vita kali kuelekea kule tunakofikiri kufika MAANA VIONGOZI WETU NA CHAMA KILICHOSHIKA HATAMU YA DOLA BADO WAKO KWENYE USINGIZI MZITO SANA.
Mpango wenyewe unazungumziwa kuhusisha pia taasisi ya mojawapo ya elimu ya juu na "wataalamu wa mambo ya katiba" ili kupangua hoja mbalimbali zinazoendelea ku-justify haja ya kuwepo na katiba mpya. Hata hivyo haijawa clear zaidi ni chuo kipi kitatumika kuandaa mpango husika na hao watakaotumika ni wakina nani ila inadaiwa mpango kamambe upo jikoni kwa ajili ya kuweka haya.
Mtazamo wangu: Japo kuwa tetesi hazina haja ya kuzifuatilia lakini naanza kuona hizi zinaweza kuwa na uzito wake maana kama jana nimezisikia kwa mtu niliesoma nae chuo na ni mtu ambae ni kada wa karibu na baba yake aliwahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa mmojawapo kanda ya ziwa na yeye ngazi za jengo la chama anazijua hadi idadi yake
Pia naweza kuhisi uko usahihi katika hili kwa kuangalia namna ambavyo TBC1 walivyoripoti Kongamano la UDASA jana
Kama hili jambo ambalo ni tetesi ni sahihi na huo mpango upo, basi bado watanzania tuna vita kali kuelekea kule tunakofikiri kufika MAANA VIONGOZI WETU NA CHAMA KILICHOSHIKA HATAMU YA DOLA BADO WAKO KWENYE USINGIZI MZITO SANA.