Kodi za nyumba Dar zinapanda kwa spidi ya hatari (maisha yanatisha)

Shirika la nyumba limeshindwa kuhudumia wananchi wenye kipato kidogo. Shirika hilo lilianzishwa kwa madhumuni ya kuhudumia wananchi hasa waishio mijini ambapo shirika hilo mwanzoni liliijenga nyumba nyingi ambazo zilikuwa rahisi kupangisha. Wapangaji walikuwa wakilipa kodi kwa mwezi.

Shirika la nyumba la taifa la sasa limejenga nyumba ambazo zinauzwa kwa bei kubwa mno kiasi ambacho wananchi wengi hawawezi kumudu kununua. Ushauri wangu ni kuwa shirika hilo lirudi kwenye misingi yake ya awali kwa kujenga nyumba nyingi na rahisi kwa ajili ya kupangisha na kodi iwe inalipwa kwa mwezi. Nyumba hizo zijengwe kwa aina tofauti ili kukidhi mahitaji tofauti ya wapangaji. Kwa mfano zijengwe nyumba ambazo mpangaji anaweza kupanga chumba kimoja tu, au mwingine anaweza kupanga nyumba ndogo yenye vyumba viwili, sebule choo na bafu n.k

Kwa kufanya hivyo serikali itakuwa imewapunguzia wananchi wengi adha ya kutafuta mahali pa kukaa hasa mijini. Ikumbukwe pia kuwa si kila mtu anaweza kurudi vijijini. Wengi wapo mijini kwa shughuli za kikazi na zinginezo nyingi.


Sahihi Mkuu!

NHC sasa imehodhiwa na matajiri huku watu wa kipato cha chini wakifanyiwa kiini macho. Kuna jambo mimi silielewi na sijui kama litakuja kuniingia akilini. NHC ina nyumba nyingi maeneo ya Upanga (Mashariki na Magharibi), hizi nyumba sasa zinavunjwa na kujengwa mpya ambazo shirika linaziuza. Ndio hizi wanazoita za kipato cha juu.

Hoja nisiyoielewa mimi hapo ni suala la shirika kuuza nyumba zilizo kwenye prime areas ambazo zingepangishwa zingeliingizia shirika mapato makubwa kiasi cha kujenga zingine nje ya mji ili na sisi tupange. Nachokiona mimi, ni kwamba WATU FULANI wenye hati miliki ya nchi wanauziana mji. Mtu anayenunua nyumba kwa bilioni kadhaa bila shaka kazitoa benki, kwa jina la mkopo. Appartment moja kwa Upanga ni kati ya US$ 2,800 hadi 4,000. Kwa hiyo uhakika wa kulipa deni la benki anao. Sasa kwa nini shirika liziuze badala ya kuzipangisha?

Hao wanaozinunua hata wasipofanya kazi maisha yao yote, watakula na kusaza huku wakitukejeli. Kosa letu ni moja tu.....HATUKOPESHEKI.
 
Wakati tunamaliza chuo pale UDSM nilibishana sana na marafiki zangu, msimamo wangu sitaki kabisa kuishi Dar wao wanakomalia eti hapa hatoki mtu. Nimewaacha huko bana. Dar hapafai kuishi mtu wa hela za kuunga unga, housing mbaya, sanitation mbaya, mara kipindupindu, joto mbaya, usafiri shida, foleni shida, maji shida, hupai fresh air kwa maeneo mengi.

Kuna kipindi nilikuwa na safari ya kikazi hapo Dar, nilifikia kwa rafiki yangu anakaa Kibada kigamboni. Goog thing alikuwa na nyumba kubwa sana na eneo kubwa na iko mlimani kwa hiyo at least ilikuwa nzuri. Sasa kituko, tunapishana siku tatu hatujaonana, alfajiri saa 11 kashaondoka anawahi foleni ili asichelewe ofisini, usiku anarudi saa tano mimi nimeshauchapa usingizi. Haya ni mateso na tunawanyima watoto wetu haki zao za msingi za kukaa na wazazi.

Karibuni huku mikoani aisee, nikiamka najiandaa dakika 15, na kwenda ofisini natumika dakika kumi


Kwahio unachukua experience ya rafiki yako kusema Dar hapafai kuishi?? Na mimi nikikwambia naamka saa moja na nusu,najiandaa nusu saa,na drive 15mins tu nafika ofisini kwangu utasema Dar panafaa! Nyumba unapanga lakini bado unashindwa kuangalia kero zinazoletwa na location na facilities za hio nyumba kosa la nani??

Kuna watu wanachekesha,anakaa Bunju nyumba ya kupanga 350,000 kazi posta, anakataa nyumba 500,000 mwenge akidhania ana save kumbe ukijumlisha gharama za mafuta na muda anatumia hela nyingi kuliko angepanga nyumba karibu na mjini
 
Nahitaji vyumba viwili , na parking Umeme na maji....viwe magomeni, studio mwananyamala, mwenge kurasini....yeyote plz anipm!!
 
Back
Top Bottom