Kodi katika mishahara ya watumishi kupunguzwa

Magazetini

JF-Expert Member
Aug 16, 2014
588
1,698
balozi-ombeni_300_170.jpg


SERIKALI imesikia kilio cha watumishi wa umma, baada ya kuahidi kupunguza viwango vya makato ya kodi katika mishahara ya watumishi hao kutoka asilimia 12 za sasa hadi kiwango kinachofikia tarakimu moja.

Viwango vya makato ya kodi kwa sasa katika mishahara ya watumishi wa umma ni asilimia 12 na lengo ni kupunguza zaidi katika kipindi cha miaka mitatu ijayo ili kuwaondolea mzigo watumishi hao.

Akizungumza na watumishi mbalimbali wa umma mkoani Kilimanjaro, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, alisema serikali inasikia maombi ya watumishi hao kwani lengo si kuwakomoa.

Hata hivyo, Balozi Sefue alisema pamoja na maombi ya muda mrefu ya watumishi hao lakini serikali imekuwa ikijitahidi kushusha makato hayo, kwani awali ilikuwa asilimia 16, ikashuka hadi asilimia 13 na sasa asilimia 12.

Aidha Katibu Mkuu Kiongozi aliwaonya watumishi wa umma kutojihusisha na siasa na kwamba wale watakaobainika kufanya hivyo watachukuliwa hatua za kinidhamu.

"Ukiwa mtumishi wa umma, unatakiwa uchague moja, kama unaingia katika siasa acha kazi ya utumishi wa umma, vinginevyo usichanganye haya majukumu," alisema.

Alisema taifa linaelekea katika Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge na Rais mwakani na kwamba ni mwiko kwa watumishi kujiingiza katika siasa, kwani kwa kufanya hivyo ni kuchanganya majukumu na moja wapo halitafanyika kikamilifu.

Balozi Sefue alitaka watumishi hao kuzingatia sheria, maadili, kanuni na taratibu za utumishi wao kwani watambue kuwa yote wanayofanya kwa mujibu wa sheria wanamwakilisha Rais Jakaya Kikwete kwani asingeweza kuwa katika kila wilaya.

Hata hivyo, alitaka mamlaka za nidhamu kuhakikisha zinawaadhibu baadhi ya watumishi ambao wanakwenda kinyume na sheria na taratibu zilizopo ili kujenga nidhamu ya utumishi.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Jumanne Sagini, alionya tabia ya baadhi ya halmashauri zote nchini kutumia fedha za miradi ya maendeleo badala ya kuzihamishia miaka inayofuata.

"Zipo halmashauri za wilaya zinapewa mabilioni ya fedha kwa miradi ya maendeleo, lakini cha ajabu ni kwamba wanakaa na fedha hizo na mwisho wa mwaka zinahamishiwa mwaka unaofuata hii haikubaliki," alisema.

Kwa upande wao baadhi ya watumishi waliomba serikali kulipa madeni ya watumishi ili kuwapa ari ya kufanya kazi kwa bidii zaidi kuliko hali ilivyo sasa.

CHANZO: Habari Leo
 
balozi-ombeni_300_170.jpg


SERIKALI imesikia kilio cha watumishi wa umma, baada ya kuahidi kupunguza viwango vya makato ya kodi katika mishahara ya watumishi hao kutoka asilimia 12 za sasa hadi kiwango kinachofikia tarakimu moja.

Viwango vya makato ya kodi kwa sasa katika mishahara ya watumishi wa umma ni asilimia 12 na lengo ni kupunguza zaidi katika kipindi cha miaka mitatu ijayo ili kuwaondolea mzigo watumishi hao.

Akizungumza na watumishi mbalimbali wa umma mkoani Kilimanjaro, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, alisema serikali inasikia maombi ya watumishi hao kwani lengo si kuwakomoa.

Hata hivyo, Balozi Sefue alisema pamoja na maombi ya muda mrefu ya watumishi hao lakini serikali imekuwa ikijitahidi kushusha makato hayo, kwani awali ilikuwa asilimia 16, ikashuka hadi asilimia 13 na sasa asilimia 12.

Aidha Katibu Mkuu Kiongozi aliwaonya watumishi wa umma kutojihusisha na siasa na kwamba wale watakaobainika kufanya hivyo watachukuliwa hatua za kinidhamu.

"Ukiwa mtumishi wa umma, unatakiwa uchague moja, kama unaingia katika siasa acha kazi ya utumishi wa umma, vinginevyo usichanganye haya majukumu," alisema.

Alisema taifa linaelekea katika Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge na Rais mwakani na kwamba ni mwiko kwa watumishi kujiingiza katika siasa, kwani kwa kufanya hivyo ni kuchanganya majukumu na moja wapo halitafanyika kikamilifu.

Balozi Sefue alitaka watumishi hao kuzingatia sheria, maadili, kanuni na taratibu za utumishi wao kwani watambue kuwa yote wanayofanya kwa mujibu wa sheria wanamwakilisha Rais Jakaya Kikwete kwani asingeweza kuwa katika kila wilaya.

Hata hivyo, alitaka mamlaka za nidhamu kuhakikisha zinawaadhibu baadhi ya watumishi ambao wanakwenda kinyume na sheria na taratibu zilizopo ili kujenga nidhamu ya utumishi.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Jumanne Sagini, alionya tabia ya baadhi ya halmashauri zote nchini kutumia fedha za miradi ya maendeleo badala ya kuzihamishia miaka inayofuata.

"Zipo halmashauri za wilaya zinapewa mabilioni ya fedha kwa miradi ya maendeleo, lakini cha ajabu ni kwamba wanakaa na fedha hizo na mwisho wa mwaka zinahamishiwa mwaka unaofuata hii haikubaliki," alisema.

Kwa upande wao baadhi ya watumishi waliomba serikali kulipa madeni ya watumishi ili kuwapa ari ya kufanya kazi kwa bidii zaidi kuliko hali ilivyo sasa.

CHANZO: Habari Leo
Hiyo ni 'gia' tu ya Chama cha Magamba, kutaka kuvuna kura za wafanyakazi, baada ya kauli ya JK kwa walimu katika kipindi cha kwanza ya awamu yake ya utawala, aliposema kura za walimu hazitaki, ambapo kauli hiyo 'ilimcost' kwa kudrop toka ushindi wa kishindo aliopata mwaka 2005, wa zaidi ya asilimia 80 hadi kupata ushindi 'kiduchu' wa chini ya asimia 60 mwaka 2010.

Hivi kweli kama serikali ya CCM ingekuwa inasympathize na sisi wafanyakazi wa kuajiriwa, hivi ndiyo ingepukuza kodi hiyo 'kiduchu' tu toka asimia 13 hadi 12, wakati wawekezaji wafanyibiashara mabilonea wa kigeni wakiwasamehe kodi za zaidi ya shilingi trilioni 1.3 kila mwaka?!

Inabidi sisi wafanyakazi tutumie umoja wetu mwakani na tutamke kuwa hatudanganyiki tena ng'ooo!!
 
Mfa maji haachi kutapatapa, wasubiri tu kifo kikipisha hodi hakirudi (sera za magamba haziuziki kirahisi tena)
 
Swali kwa huyo katibu? ameongelea kuhusu wafanyakazi wa uma wasijihusishe na siasa! na je analionaje hili la mawaziri kuwa wabunge! au katumwa kuja kufanya siasa za chinichini na kuwapiga mkwara wafanyakazi wa uma. Kwajili ya uchaguzi ujao wa 2015, asijidanganye huyo sasahivi kila mtu anaijuwa haki yake ya msingi, ache mambo ya kizamani ya kudanganyana ili kutetea masrahi yake.
 
Hawa maccm ovyo kabisa, wanatuona sisi watumishi mamburula eeet!! miaka yote hawakulijua hilo au walisubiri karibu na 2015 ili wajipatie kura??? watumishi tusidanganyike na hizi porojo za maccm...
 
haa haa baada ya hapo itarudi kama mwanzo au itapandishwa..


Kitatafutwa kisingizio kingine, then inarudi kulekule!!! ni kama ilivyokuwa kwenye magari walisema wanaondoa ushuru ili watumishi waweze kununua vyombo vya usafiri, waliponunua tu kiwese kikaongezwa bei, road licence nayo bei juu, wakaongeza malipo ya fire extinguisha, tozo ya wiki ya usalama barabarani nayo ikapanda, mtego mwingnine ukawekwa kwa wale wauguzi wanaotoa tiba barabarani, ukipiga hesabu jumla unakuta ule ushuru uliondolewa unaulipia kupitia mlango mwingine, kwahiyo DEMBA kaa chonjo na hizi propaganda
 
Aaaahaaaah!!hawa viongozi wetu wananifurahisha sana.

1. Mimi kama mtumishi wa umma namwakilisha mtumishi mkuu wa umma ambaye ni Rais....Sasa kama ninayemwakilisha ni mwanachama wa chama cha siasa tena ni "MWENYEKITI" wa chama,sasa mtanizuiaje mimi kuwa na Chama cha siasa?!...(hoja hapa nikuwa niwe kada wa CCM tu sio? nisiunge mkono UPINZANI especially CHADEMA)

2. Swala la kupunguza kodi leo nakujifanya wasikivu ndo leo linawajia eeeeh? eti tumesikia kilio...kwanza nani analia? ni nani aliyesababisha huyo mliaji alie?na huyo mliaji amelia tokea lini labda? na kwanini hamkumsikiliza miaka yote aliyokuwa akilia mpaka leo uchaguzi unapokarbia ndo asikilizwe? daaah kweli mnahuruma sana...huruma hii inalenga kitu kimoja tu! KURA ya kuwapa KULA.

3. Binafsi kama mfanyakazi wa serikali (MWALIMU) naelewa na kamwe sitauza KURA yangu tena.. 2015 sitafanya MAKOSA ya miaka nenda rudi...kamwe ''HAMTAKULA'' KURA yangu kwa 2015.....

NIMEKAA NA NYIE,NIMEWAFAHAMU VIZURI na 2015 niwakati wenu KUNIFAHAMU PIA......

TUKUTANE 2015.
 
eti......katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.......AIBU YENU NA WAJUKUU ZENU!
 
Back
Top Bottom