Mganguzi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2022
- 1,037
- 2,774
(1) Freeman Mbowe
Yule wa mwaka 2005-2015, alikuwa mpinzani kweli kweli, chuma hasa hasa! Alikuwa mhimili sio tu kwa chadema Bali kwa vyama vyote vya upinzani.
Kwa sasa amekata pumzi anapigania mkate na huruma ya watawala!
(2) Maalim Seif
Huyu hatuna mfano wake amekufa akiwa shujaa ,hakuwahi kugeuka nyuma ,peke yake tu alikuwa na uwezo wa kukitikisa kisiwa Cha Zanzibar na kikatikisika! Amekufa akiwa shujaa!
(3) Ibrahim Lipumba
Wa enzi zile 1995 -2010 hakuwa na mchezo ,alipoanza tamaa za madaraka na kutengana na maalim mambo yote yaliharibika !kwa sasa yeye na chama hakuna anaepoteza muda kujua wako wapi!
(4) Dkt. Wilbrod Slaa
Alikuwa mpinzani hatari zaidi miaka ya 2005 -2014 baada ya hapo hatujui ninini kilimpata!
(5)Zitto ZuberI Kabwe
Kama asingefanyiwa figisu CHADEMA na tamaa ya kutaka kumtoa Mbowe kwenye nafasi yake nahisi hakuna mpinzani angemfikia, alikuwa moto kweli kweli,kwa sasa ananguvu na hoja zenye msimamo japo chama chake kimekosa nguvu na mvuto!
(6)David Kafulila
Huyu mwamba akiwa mpinzani moto uliwaka kweli kweli alikuwa haogopi mtu na mbunge alilimudu sana kwa sasa ni kada wa CCM!
(7) Mabere Malando
Ilikuwa nguzo sana kwa upande siasa za upinzani miaka ya 2000-2010
(8) Salum Mwalimu na Profesa Jay, Sugu, Peter Msigwa, Heche na Halima Mdee
Ilikuwa ndio mbegu changa inayoibuka kwa Kasi kwa sasa hawana pumzi Tena!
(9) Tundu Lissu
Ni mwanasheria na nguli wa siasa za kisasa ,anapaswa kurudi bungeni na sio kugombea urais Tena( 10) nassoro mazrui ni hatari na nusu, huyu ndiye anaweza kuwa mrithi sahihi wa maalimu seif pale Zanzibar, kwa hao na wengine wengi walikuwa Bora sana siku za nyuma kwa sasa waruhusu kizazi kipya kinyume na hapo siku zijazo hatutakuwa na upinzani tena.
Yule wa mwaka 2005-2015, alikuwa mpinzani kweli kweli, chuma hasa hasa! Alikuwa mhimili sio tu kwa chadema Bali kwa vyama vyote vya upinzani.
Kwa sasa amekata pumzi anapigania mkate na huruma ya watawala!
(2) Maalim Seif
Huyu hatuna mfano wake amekufa akiwa shujaa ,hakuwahi kugeuka nyuma ,peke yake tu alikuwa na uwezo wa kukitikisa kisiwa Cha Zanzibar na kikatikisika! Amekufa akiwa shujaa!
(3) Ibrahim Lipumba
Wa enzi zile 1995 -2010 hakuwa na mchezo ,alipoanza tamaa za madaraka na kutengana na maalim mambo yote yaliharibika !kwa sasa yeye na chama hakuna anaepoteza muda kujua wako wapi!
(4) Dkt. Wilbrod Slaa
Alikuwa mpinzani hatari zaidi miaka ya 2005 -2014 baada ya hapo hatujui ninini kilimpata!
(5)Zitto ZuberI Kabwe
Kama asingefanyiwa figisu CHADEMA na tamaa ya kutaka kumtoa Mbowe kwenye nafasi yake nahisi hakuna mpinzani angemfikia, alikuwa moto kweli kweli,kwa sasa ananguvu na hoja zenye msimamo japo chama chake kimekosa nguvu na mvuto!
(6)David Kafulila
Huyu mwamba akiwa mpinzani moto uliwaka kweli kweli alikuwa haogopi mtu na mbunge alilimudu sana kwa sasa ni kada wa CCM!
(7) Mabere Malando
Ilikuwa nguzo sana kwa upande siasa za upinzani miaka ya 2000-2010
(8) Salum Mwalimu na Profesa Jay, Sugu, Peter Msigwa, Heche na Halima Mdee
Ilikuwa ndio mbegu changa inayoibuka kwa Kasi kwa sasa hawana pumzi Tena!
(9) Tundu Lissu
Ni mwanasheria na nguli wa siasa za kisasa ,anapaswa kurudi bungeni na sio kugombea urais Tena( 10) nassoro mazrui ni hatari na nusu, huyu ndiye anaweza kuwa mrithi sahihi wa maalimu seif pale Zanzibar, kwa hao na wengine wengi walikuwa Bora sana siku za nyuma kwa sasa waruhusu kizazi kipya kinyume na hapo siku zijazo hatutakuwa na upinzani tena.