MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,604
Mwanamke mmoja alikuwa wa ki-leo sana kiasi kwamba sehemu kubwa ya pato lake na mume wake liliishia katika kubadilisha samani na vyombo vya matumizi ya nyumbani na kuweka vya umeme: jiko, sufuria, jokofu, radio, fagio...vyote vya umeme. Mume akawa anajitahidi kukidhi matakwa ya mke wake mpaka wakamaliza mahitaj yote. Mume akafikiri "sasa nitapumua", lakini wapi. Siku moja mke akadai:
"Mume wangu, leo nikirejea kazini nitapita madukani ninunue kiti cha umeme"
Mume wala hakujibu, alipotoka kuenda kazini hakurejea nyumbani hadi leo.
"Mume wangu, leo nikirejea kazini nitapita madukani ninunue kiti cha umeme"
Mume wala hakujibu, alipotoka kuenda kazini hakurejea nyumbani hadi leo.