Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,014
- 9,883
Jela miaka 30 kwa kumpa mimba mwanae
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kiteto, imemhukumu kifungo cha miaka 30, Yerenia Chidaka, mkazi wa Kijiji cha Dongo wilayani humo, baada ya kumtia mimba mtoto wake wa miaka 16.
Mtuhumiwa amekiri kosa hilo hii Septemba 7, 2022, mbele ya Hakimu Mkazi Mosi Sasy, na kusema hataki kuisumbua Mahakama kwa kuwa aliamua kutembea na mtoto wake huyo hakutaka aolewe na kabila la Wakamba.
Aidha Baba huyo imeelezwa kuwa alipomuuliza mke wake juu ya suala la kutotaka mtoto wao aolewe na Wakamba, mkewe alimjibu kwa dhihaka kwamba kama hataki aolewe basi amuoe yeye na ndipo alipoamua kumpa ujauzito.
Alipotakiwa kujitetea, mtuhumiwa aliiomba Mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa shetani alimpitia kutenda kosa hilo,huku Mwendesha Mashtaka wa Polisi Mahakamani hapo Inspekta Wilfred Mollel, akisema Jeshi la Polisi halina taarifa kama mtuhumiwa aliwahi kufanya kosa zaidi ya hilo na kumwomba Hakimu kumpa adhabu inayostahiki.
EATV
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kiteto, imemhukumu kifungo cha miaka 30, Yerenia Chidaka, mkazi wa Kijiji cha Dongo wilayani humo, baada ya kumtia mimba mtoto wake wa miaka 16.
Mtuhumiwa amekiri kosa hilo hii Septemba 7, 2022, mbele ya Hakimu Mkazi Mosi Sasy, na kusema hataki kuisumbua Mahakama kwa kuwa aliamua kutembea na mtoto wake huyo hakutaka aolewe na kabila la Wakamba.
Aidha Baba huyo imeelezwa kuwa alipomuuliza mke wake juu ya suala la kutotaka mtoto wao aolewe na Wakamba, mkewe alimjibu kwa dhihaka kwamba kama hataki aolewe basi amuoe yeye na ndipo alipoamua kumpa ujauzito.
Alipotakiwa kujitetea, mtuhumiwa aliiomba Mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa shetani alimpitia kutenda kosa hilo,huku Mwendesha Mashtaka wa Polisi Mahakamani hapo Inspekta Wilfred Mollel, akisema Jeshi la Polisi halina taarifa kama mtuhumiwa aliwahi kufanya kosa zaidi ya hilo na kumwomba Hakimu kumpa adhabu inayostahiki.
EATV