Kitengo cha Mawasiliano ya Umma CHADEMA, Kunani?

muhosni

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
1,108
152
Naomba kuweka masikitiko yangu kuhusu kitengo cha mawasiliano ya umma cha Chadema hapa janvini. Watu mbali mbali wamekuwa wakilalamika na kutoa ushauri kwa muda sasa, lakini nasikitika kwamba sijaona jitihada za kuboresha kitengo hiki.

Masikitiko yangu yamejikita zaidi kwenye maandamano na matukio makuu ya Chadema hasa yale yaliyotokea kuanzia Desemba 2010 hadi leo.

Tunaambiwa kwamba kikao cha uchaguzi wa Meya Arusha mjini kilikuwa na vurugu. Hatukupata picha hata moja hadi leo. Tukaambiwa kwamba katika kikao hicho Godbless Lema alipigwa na polisi. Picha pekee tuliyopata ni ile ya Godbless Lema akiwa amelazwa hospitalini

Kukawa na maandamano tarehe 5 Januari, picha tulizopata ni zile za kuokoteza kutoka kwa washabiki tu. Polisi walichakachua picha zoa wakatuonesha lakini Chadema hawajawahi kutuonesha chochote. Kuna watakaodai kwamba TV za Tz hazikubali kurusha vipindi vya Chadema. Mimi nitasema kwamba teknolojia imekua, kuna YouTube, na pia blogs kama JF. Zisambazwe kwa CD.

Tarehe 12 Januari kukawa na mazishi ya waliouawa na polisi. Hadi leo hatujapata picha rasmi kutoka chadema.

Kumekuwa na maandamano yaliyoanzia Mwanza na jana yalikuwa Mara. Hali ni ileile.

Wakati wa tukio, tunapewa taarifa na members pengine na viongozi kama Regia kwamba ni nini kinachoendelea. Lakini hatupati picha za kuanzia mwanzo wa tukio hadi mwisho. Na hatuoni jukumu la kitengo cha mawasiliano ya umma katika hili.

Sipingi wakereketwa na wapenzi kuturushia picha moja au mbili (baada ya kuchelewa na kuomba sana). Sipingi wakereketwa na wapenzi wa Chadema kutupa updates za kinachoendelea kwenye tukio fulani. Tungeweza kupata zaidi kama kuna kitengo rasmi kilichopewa vifaa na kina watendaji waliofuzu kutumia teknolojia ya kisasa.

Kama tungekuwa tunapata picha na taarifa za tukio kadri linavyotokea, polisi na ccm wasingeweza kudanganya wananchi kirahisi. Lakini sasa hivi jambo kubwa linatokea halafu kinachofuata ni malumbano ya maneno kati ya serikali/ccm/polisi na Chadema. Kama vile bado tunaishi katika karne ya 17.

Kuna swala la kutunza kumbukumbu pia, sijui matukio haya makuu yenye historia ya nchi yetu yatakuwa yamehifadhiwa vipi.
 
I have taken note of your contribution. I will personally forward it to those responsible.

Thank you for such progressive thoughts.
 
Umenena ni mambo ya msingi na nataka viongozi wa cdm waliosikia na walitendee kazi asap.
 
Hivi mbona inaonekana ni tatizo sana hiki kitengo kusikia maoni ya watu na kuboresha huduma zake. Ukienda kwenye website yao imelala doro kabisa wakati matukio yanatokea kila siku. Au Chadema hawana kitengo kama hiki? Kama hawana basi waanzishe ASAP!
 
Matatizo haya hajaanza jana hata kipindi cha kampeni kuna kipindi nilikuwa nagundua kuna mkutano wa chadema mchana kupitia JF.. Mfano siku Dr Slaa alipokuja Arusha watu wengi walipata taarifa akiwa ameshafanya mkutano wa kwanza ambao ulifanyika mbauda kisha kuelekea Monduli na baadae kurudi tena Arusha ndipo watu walijitokeza kwa wingi na wengi wakilaumu kutokupewa taarifa mapema, ikafatiwa na mkutano uliofanywa na Mbowe kwenye viwanja vya NMC siku chache kabla ya uchaguzi walitangaza saa 5 asubuhi na mkutano ukafanyika saa 8 mchana, Gari la matangazo lilipita baadhi ya mitaa, kuna kipindi picha za mgombea uraisi zilikuwa hazipatikani hata madiwani hawakuwa na picha za mgombea, tatizo hilo lilikuwa linajitokeza pia kwenye upatikanaji wa bendera za chama...niliamini ilikuwa ni hali ya uchumi kwani chama kilikuwa na mambo mengi sana ukilinganisha na mapato waliyo kuwa wakipata kipindi kilicho pita lakini nitaomba lifanyiwe kazi maana angalau kwasasa mfuko umetuna kidogo.
 
Hivi mbona inaonekana ni tatizo sana hiki kitengo kusikia maoni ya watu na kuboresha huduma zake. Ukienda kwenye website yao imelala doro kabisa wakati matukio yanatokea kila siku. Au Chadema hawana kitengo kama hiki? Kama hawana basi waanzishe ASAP!
Ni swala la kutoa kipaumbele tu, wameshindwa kuajiri webmaster kwa ajiri ya ku-update website ya chama...ni kitu cha kushangaza sana kuona website ya chama iko doro wakati ile wabsite ni dynamic ni rahisi tu ku-update....
 
Naunga Mk0‹2no kwa asilimia zote..katika hali ya sasa Cdm lazima wakiwezeshe kitengo cha habari na kiweze ku updates kila kitu na kwa wakati..tunataka tujue Dr slaa anafanya nini,maandamano yanaendeleaje viongozi wanasemaje, makongomano ,mipango na kila information kwa ajili ya kutupa nguvu na moyo.ukitegemea magazeti na Tv ni rahis kuzichakachua ..Naunga Mkono Hoja
 
Kwa kidogo kilichopo kitumike vizuri ili atimae kilete faida. Kitengo cha habari na mahusiano ya umma kwa CDM inabidi kiboreshwe ili kila tukio linalotokea wadau walipate kwa ufasaha.
naunga mkono hoja.
 
Ni wazo zuri lakini kwa vile SISIEMU na serikali yake bado ni 'wababe', kuwawekea kila kitu hadharani officially vitu vinaweza ku-'back-fire' maana CCM hawachelewi 'kuchakachua' wacha tuendelee 'kuwastukiza na nguvu ya umma' .

Hivyo 'nguvu ya umma' kupitia JF ndiyo mojawapo ya source ya mawasiliano kwa sasa, maana kwa njia hii ya 'ushirikishwaji wa nguvu za umma' katika kueneza sera na habari za CHADEMA, chama kina uhakika kuwa huu moyo wa kujitolea kutoa habari za matukio toka mashinani ni dalili tosha CHADEMA inakubalika na 'kikishaeleweka' baadaye ktk KATIBA MPYA YA TANZANIA basi mambo yatakuwa more official. kwa sasa acha nguvu ya umma iburuzane na SISIEMU iwe maandamano, forums n.k

Mtindo wa mpaka 'katibu mkuu ofisi ndogo ya CCM Lumumba' kuwa njia pekee ya kutoa habari ni sawa na kupora haki za 'nguvu ya umma' kuwasiliana wenyewe kwa wenyewe bila kutegemea mfumo rasmi.
 
ndugu yangu CHADEMA kinakuwa tu kwa nguvu za mungu..wala hakuna kitengo idara wala hata dawati la mawasiliano ya umma...kuna idara ya habari na uenezi ambayo wamemuweka jamaa mmoja aliyewahi kuwa mbunge wa kisesa miaka ya nyuma na akashindwa shindwa baadaye mtu ambaye hana uwezo hata kidogo..mawazo yake yeye ni NGONO masaa 24..
SIKU WATANZANIA WAKIIJUA CHADEMA HALISI NDIO MWISHO WA UPINZANI NCHINI
 
Ni wazo zuri lakini kwa vile SISIEMU na serikali yake bado ni 'wababe', kuwawekea kila kitu hadharani officially vitu vinaweza ku-'back-fire' maana CCM hawachelewi 'kuchakachua' wacha tuendelee 'kuwastukiza na nguvu ya umma' .

Hivyo 'nguvu ya umma' kupitia JF ndiyo mojawapo ya source ya mawasiliano kwa sasa, maana kwa njia hii ya 'ushirikishwaji wa nguvu za umma' katika kueneza sera na habari za CHADEMA, chama kina uhakika kuwa huu moyo wa kujitolea kutoa habari za matukio toka mashinani ni dalili tosha CHADEMA inakubalika na 'kikishaeleweka' baadaye ktk KATIBA MPYA YA TANZANIA basi mambo yatakuwa more official. kwa sasa acha nguvu ya umma iburuzane na SISIEMU iwe maandamano, forums n.k

Mtindo wa mpaka 'katibu mkuu ofisi ndogo ya CCM Lumumba' kuwa njia pekee ya kutoa habari ni sawa na kupora haki za 'nguvu ya umma' kuwasiliana wenyewe kwa wenyewe bila kutegemea mfumo rasmi.

Mkuu, ama akili yangu ni ndogo sana sijaweza kukuelewa ama wewe hujaelewa mada vema
 
ndugu yangu CHADEMA kinakuwa tu kwa nguvu za mungu..wala hakuna kitengo idara wala hata dawati la mawasiliano ya umma...kuna idara ya habari na uenezi ambayo wamemuweka jamaa mmoja aliyewahi kuwa mbunge wa kisesa miaka ya nyuma na akashindwa shindwa baadaye mtu ambaye hana uwezo hata kidogo..mawazo yake yeye ni NGONO masaa 24..
SIKU WATANZANIA WAKIIJUA CHADEMA HALISI NDIO MWISHO WA UPINZANI NCHINI

Kama hayo ndiyo matatizo, kwa nini wasishutuke watu wanapolalamika tangu wakati wa kampeni za uchaguzi hadi leo? Kuna mada nyingine ilikuwa hapa wiki iliyopita mzemaji mmoja akasema kama chadema inashindwa kusikiliza kilio cha wananchi juu ya hili kwa muda wote huu basi haina tofauti na ccm
 
Hatukujua leo wana ratiba gani hadi Regia alipotuambia wanatembelea nyumbani kwa Nyerere. Hatujui kesho watakuwa wapi wala siku zingine wiki ijayo watakuwa wapi
 
Na website ya CDM haiko updated Ina habari za siku nyingi sana. Nadhani tukubali hiki kitengo kina matatizo na kinahitaji kurekebushwa Haraka iwezekanavyo tafadhari wanahusika tunaomba ili lifanyiwe kazi Haraka....sitaki kuamini kwamba chama hakina Uwezo wa Kuendesha kitengo hiki kwa Kisasa zaidi.....ni Kama kimekufa kwa sasa......PLZ TUNAWAOMBA JAMANI TUACHE KURIDHIKA!!
 
Tusiwalaumu CDM kwa hili kwani chama kimepanuka kwa haraka mno katika kipindi cha kuelekea na baada ya uchaguzi 2010. Hizi zinaitwa growing challenges na taasisi zote zinazokuwa huyapitia haya. Matarajio ya watu kwa Cdm ni makubwa na kuyatimiza ni changamoto kubwa. Naamini wahusika wameyaona maoni yenu na muda si mrefu tutaona mabadiliko.
 
Tusiwalaumu CDM kwa hili kwani chama kimepanuka kwa haraka mno katika kipindi cha kuelekea na baada ya uchaguzi 2010. Hizi zinaitwa growing challenges na taasisi zote zinazokuwa huyapitia haya. Matarajio ya watu kwa Cdm ni makubwa na kuyatimiza ni changamoto kubwa. Naamini wahusika wameyaona maoni yenu na muda si mrefu tutaona mabadiliko.

Mkuu sidhani kama kukua ni tatizo. watu wanazungumzia umuhimu wa kitengo cha mawasilianao kwa umma na ushauri huu umetolewa tangu wakati wa uchaguzi walipoluwa wanapata michango yetu mingi sana kupitia friendsofslaa na sasa wana ruzuku. Propaganda na mawasilianao kwa chama chochote cha siasa ni lazima. Ilitakiwa washindwe kufanya lingine lolote lakini wahakikishe mawasiliano kwa umma ni imara na ya kisasa kabisa
 
Back
Top Bottom