Kitendo hiki unakizungumziaje kinapotokea katika taasisi ya elimu ya juu?

StricklyBiz

New Member
Jan 4, 2015
4
0
Binafsi sijafurahishwa na sijui kitu gani kingine cha kufanya katika nafasi niliyonayo kama mwanafunzi kuzuia jambo hili kutokea tena zaidi ya kuandika hapa. Leo nimeshuhudia Lecturer wa hapa chuoni akimshushia kichapo kikali ikiwemo ngumi na vibao mwanafunzi mwenzangu hapa chuoni (DIT).

Chanzo kikubwa ni kuwa, Lecturer huyo alikua akifundisha lecture room jirani, wakati ambapo kulikuwa na discussion ya darasa zima ikiendelea katika lecture room tuliyokuwemo. Alituomba kuondoka maana discussion yetu ilionekana kuleta kelele na kumsumbua wakati akiendelea na kipindi chake. Tulitii na wakati watu wakiendelea kutoka nje kuna baadhi waliendelea kufungasha vitu vyao ikiwemo laptops na vitu vingine kama madaftari, mmoja wao akiwa muhusika ninaye mzungumzia katika thread hii. Mwalimu kuona kuna watu bado wanafungasha vitu sijui alikua ana mawwazo gani siku ya leo, maana moja kwa moja alianza kumrushia maneno ya fedheha. Baada ya hapo kilichofata zilikua ni ngumi na vibao akimsukuma kuelekea nje, Lecturer alionekana mwenye hasira na sababu pekee niliyofikiri kwa muda huo ilikuwa ni kuchelewa kwa wanafunzi kutoka nje ya hiyo lecture room. sijapenda kuona mwanafunzi akidharirishwa namna hiyo bila kufanya kosa lolote la msingi, na hata kama angekuwa na kosa sidhani kama lecturer ama mtu yoyote ana mamlaka kisheria ya kumpiga mtu mwingine namna hiyo. Leo imetokea kwa rafiki yangu, na ameamua kutochukua hatua zozote ukizingatia lecturer huyo huyo anatufundisha semister hii, kesho inaweza kutokea kwangu ama kwako.

kama titile inavyojieleza karibu.
 
Huyo aliyepigwa ni "me" or "ke"??? Bcoz ma lecturer wanapenda sana mademu wakareee
 
ni "Me" na wala hana hata izo ishu za mademu. Ni dogo ambaye ukimuona huwezi fikiria mara mbili kuwa ameonewa.
 
Unajuaje labda uyo mwanafunz alitoa jbu baya kwa lecture! tatizo madogo na nyie mkifka chuo mnaona ka mmemaliza kila kitu.. Na kama siyo ivo bas atakuwa alilewa na bang au amepitia police anatimza kaul ya mh pinda
 
Kama unao ushahidi wa kutosha peleka sehemu inayohusika.yeye kuwafundisha semester hii isiwatie hofu kuwa atawafelisha.na hofu hiyo ndio mara nyingi hufanya wanafunzi wengi vyuoni kunyanyaswa na walimu wao kwa kuhofia kupewa alama za chini za ufaulu katika mitihani yao.na hata huku uraiani pia wananchi ni waoga kudai au kutoa taarifa pale wanaponyanyaswa au kuonewa mfn..askari polisi,mwanajeshi,diwani,mbunge n.k.mimi nilipambana na askari mmoja mtaani kwetu hakuamini kama nilimhenyesha kiasi kile.na nilienda ofisi za nssf mwanza nako waliniletea za kuleta tukapambana kwa hoja na kisheria mpk kikaeleweka.ninayo mifano mingi sana.so ndg acha uwoga jiamini hasa pale unapojua una haki juu ya jambo fulani.
 
Kiukweli kitendo hichi kimeniuma😥 sana mim kama mwanataasisi., na kama classmate., nashauri aende DITSO najua Lumola atalifanyia kazi..
 
Binafsi sijafurahishwa na sijui kitu gani kingine cha kufanya katika nafasi niliyonayo kama mwanafunzi kuzuia jambo hili kutokea tena zaidi ya kuandika hapa. Leo nimeshuhudia Lecturer wa hapa chuoni akimshushia kichapo kikali ikiwemo ngumi na vibao mwanafunzi mwenzangu hapa chuoni (DIT).

Chanzo kikubwa ni kuwa, Lecturer huyo alikua akifundisha lecture room jirani, wakati ambapo kulikuwa na discussion ya darasa zima ikiendelea katika lecture room tuliyokuwemo. Alituomba kuondoka maana discussion yetu ilionekana kuleta kelele na kumsumbua wakati akiendelea na kipindi chake. Tulitii na wakati watu wakiendelea kutoka nje kuna baadhi waliendelea kufungasha vitu vyao ikiwemo laptops na vitu vingine kama madaftari, mmoja wao akiwa muhusika ninaye mzungumzia katika thread hii. Mwalimu kuona kuna watu bado wanafungasha vitu sijui alikua ana mawwazo gani siku ya leo, maana moja kwa moja alianza kumrushia maneno ya fedheha. Baada ya hapo kilichofata zilikua ni ngumi na vibao akimsukuma kuelekea nje, Lecturer alionekana mwenye hasira na sababu pekee niliyofikiri kwa muda huo ilikuwa ni kuchelewa kwa wanafunzi kutoka nje ya hiyo lecture room. sijapenda kuona mwanafunzi akidharirishwa namna hiyo bila kufanya kosa lolote la msingi, na hata kama angekuwa na kosa sidhani kama lecturer ama mtu yoyote ana mamlaka kisheria ya kumpiga mtu mwingine namna hiyo. Leo imetokea kwa rafiki yangu, na ameamua kutochukua hatua zozote ukizingatia lecturer huyo huyo anatufundisha semister hii, kesho inaweza kutokea kwangu ama kwako.

kama titile inavyojieleza karibu.

Walimu kama hao wanatafuta kukunjwa na kupigwa ngumi.

Tuliwatandika vibao enzi zetu Tambaza mpaka kukawa na heshima.

Vijana inabidi mpige vyuma, kuna miili hata lecture akiwa na hasira akiiangalia anapata kusuasua tashtiti.
 
Wanafunzi wa vyuo vya siku hizi ni bora watandikwe tu viboko na hata ikiwezekana viboko viwekwe mavyuoni
 
Back
Top Bottom