WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Kitchen party ni biashara kubwa sana kadri miaka inavyoenda.Nielewavyo mimi KP ( kufundwa bi harusi) huko nyuma,makabila mbalimbali yalitumia siku chache kabla y aharusi kukaa na bi harusi mtarajiwa kumshauri kuhusu majukumu atakayoenda kukutana nayo kama mke na hata mama.Alipewa mawaidha mbalimbali yanayohusu usafi wake binafsi, usafi wa nyumbani kwake, umuhimu wa kuwa mchapakazi na siyo mvivu, kumheshimu na kumpenda mume wake; kuwajali ndugu wa mume, kukaa na marafiki/mashoga na hatari ya kuwavuta karibu na mumewe; na mengine mengi.
Katika kabila langu mimi jukumu hili lilibebwa na wanawake walioko kwenye ndoa tu na walioheshimika kwenye jamii na si vinginevyo.Shughuli hii ilikuwa private na haikuhusisha watu wengi sana na wala haikuhitaji gharama kubwa sana.Mfundaji hakulipwa ujira au malipo ya pesa, sana sana aliweza kutunukiwa zawadi ndogondogo kadri mtu alivyoona inafaa.Wanaume hawakuhusishwa kwa namna yoyote ile maana na wao walikuwa na utaratibu wao wa kuandaa bwana harusi.( Makabila yanatofautiana na hapa ndipo nitaomba michango yenu)
Katika ustaarabu wa wenzetu wazungu kuna kitu kinaitwa bridal shower ambacho asili yake ni nchi za Ulaya ukasambaa na kukomaa na kudumu nchi za America ya kaskazini.Bridal Shower ilikuwa ni tafrija iliyoandaliwa mahususi na wale wasichana wa kusimamia harusi - Bridesmaids( marafiki na ndugu wa bi harusi mtarajiwa) kumzawadia bibi harusi wiki chache kabla ya siku yenyewe ya harusi.Vilevile kufuatana na historia hii ilikuwa siku maalum pia "kumfunda" mtarajiwa kuhusu majukumu yake kama mke na mama.
Kwa Tanzania shughuli hii imeendelea kukua siku hadi siku na kuongezeka ukubwa na gharama na hata maudhui na mpangilio wake.Inaunganisha watu wa marika tofauti, makabila na dini mbalimbali.Inaanza na kukusanya michango, kununua sare, kuandaa vyakula na vinywaji,anakuwepo mshereheshaji mwenye kutumia kipaza sauti ( hakuna siri tena), wapiga picha za mnato na video na muziki ambao mara nyingi ni wanaume ( wanaume wameanza kuingia kwenye KP!!) na pia utoaji mada na nasaha .Muziki unakuwa mchanganyiko lakini mara nyingi ni rusha roho na vijembe vya hapa na pale.Shughuli haifanyiki nyumbani ( kitchen)tena kama huko nyuma - sasa imehamia kwenye kumbi na kumbi nyingi unakutana kuna wanaume .
Kwenye maudhui watu hutoafautiana katika KP nilizowahi kuhudhuria.Kuna wale wenye kutoa mada zilizoandaliwa kitaalam kulenga kumpa mawaidha mema yenye staha ( nimeona wakinukuu hata vitabu vya dini) na kuna wale wenye kumwaga radhi - kuongea maneno makali yasiyo na staha, kuonyesha kwa vitendo namna ya kumfurahisha mume na wakati mwingi ni aibu tupu kuona wanawake wenye umri wa kutosha wakisimulia mambo ya chumbani bila haya wala soni kwenye kadamnasi yenye watu wa marika mbalimbali.Niliwahi kuona KP moja vijana wa kiume wakiona aibu na kucheka kiaibuaibu maana walitakiwa kukoleza hayo mawaidha kwa kibwagizo maalum kilichochaguliwa na huyo MC! - ILILKUWA AIBU KUBWA.
Kwa kifupi kwa maoni yangu nimeona kuwa KP hizi ni mchanganyiko usioleweka - kuna elements za Bridal shower ya kizungu, kuna mambo ya Pwani ya kurushana roho, kuna mambo ya kidini kwa maana ya mawaidha ya dini, alimradi ni vurugu tupu.Sijawahi kusikia utafiti wowote uliofanyika kutathmini kama KP zinasaidia kudumisha ndoa au la, au kuona kama mafunzo yanayotolewa kwenye KP yanatumika na walioolewa ili kudumisha ndoa zao.Kama kunautafiti huo, naomba tuhabarishane na kupeana rejea ili tuusake tujisomee wenyewe.
Ukipiga hesabu ya gharama inayotumika, muda, na kinachotokana na hiyo KP nadhani kwa wale wachumi watasema ni kutupa pesa kwenye shimo.Lakini kwa wanajamii watasema hapana.Hii ni fursa ya akina mama kutandaa ( networking), kujirusha na kuondoa stress - hata kama kinachopatikana hapo kwa maana ya kudumisha ndoa ya mtarajiwa ni nil.
Ninayo mengi ya kuongea lakini nisimalize uhondo - nawaachia na wengine watoe maoni yao.
Je- KP hizi zina tija na mwelekeo unafaa?
Katika kabila langu mimi jukumu hili lilibebwa na wanawake walioko kwenye ndoa tu na walioheshimika kwenye jamii na si vinginevyo.Shughuli hii ilikuwa private na haikuhusisha watu wengi sana na wala haikuhitaji gharama kubwa sana.Mfundaji hakulipwa ujira au malipo ya pesa, sana sana aliweza kutunukiwa zawadi ndogondogo kadri mtu alivyoona inafaa.Wanaume hawakuhusishwa kwa namna yoyote ile maana na wao walikuwa na utaratibu wao wa kuandaa bwana harusi.( Makabila yanatofautiana na hapa ndipo nitaomba michango yenu)
Katika ustaarabu wa wenzetu wazungu kuna kitu kinaitwa bridal shower ambacho asili yake ni nchi za Ulaya ukasambaa na kukomaa na kudumu nchi za America ya kaskazini.Bridal Shower ilikuwa ni tafrija iliyoandaliwa mahususi na wale wasichana wa kusimamia harusi - Bridesmaids( marafiki na ndugu wa bi harusi mtarajiwa) kumzawadia bibi harusi wiki chache kabla ya siku yenyewe ya harusi.Vilevile kufuatana na historia hii ilikuwa siku maalum pia "kumfunda" mtarajiwa kuhusu majukumu yake kama mke na mama.
Kwa Tanzania shughuli hii imeendelea kukua siku hadi siku na kuongezeka ukubwa na gharama na hata maudhui na mpangilio wake.Inaunganisha watu wa marika tofauti, makabila na dini mbalimbali.Inaanza na kukusanya michango, kununua sare, kuandaa vyakula na vinywaji,anakuwepo mshereheshaji mwenye kutumia kipaza sauti ( hakuna siri tena), wapiga picha za mnato na video na muziki ambao mara nyingi ni wanaume ( wanaume wameanza kuingia kwenye KP!!) na pia utoaji mada na nasaha .Muziki unakuwa mchanganyiko lakini mara nyingi ni rusha roho na vijembe vya hapa na pale.Shughuli haifanyiki nyumbani ( kitchen)tena kama huko nyuma - sasa imehamia kwenye kumbi na kumbi nyingi unakutana kuna wanaume .
Kwenye maudhui watu hutoafautiana katika KP nilizowahi kuhudhuria.Kuna wale wenye kutoa mada zilizoandaliwa kitaalam kulenga kumpa mawaidha mema yenye staha ( nimeona wakinukuu hata vitabu vya dini) na kuna wale wenye kumwaga radhi - kuongea maneno makali yasiyo na staha, kuonyesha kwa vitendo namna ya kumfurahisha mume na wakati mwingi ni aibu tupu kuona wanawake wenye umri wa kutosha wakisimulia mambo ya chumbani bila haya wala soni kwenye kadamnasi yenye watu wa marika mbalimbali.Niliwahi kuona KP moja vijana wa kiume wakiona aibu na kucheka kiaibuaibu maana walitakiwa kukoleza hayo mawaidha kwa kibwagizo maalum kilichochaguliwa na huyo MC! - ILILKUWA AIBU KUBWA.
Kwa kifupi kwa maoni yangu nimeona kuwa KP hizi ni mchanganyiko usioleweka - kuna elements za Bridal shower ya kizungu, kuna mambo ya Pwani ya kurushana roho, kuna mambo ya kidini kwa maana ya mawaidha ya dini, alimradi ni vurugu tupu.Sijawahi kusikia utafiti wowote uliofanyika kutathmini kama KP zinasaidia kudumisha ndoa au la, au kuona kama mafunzo yanayotolewa kwenye KP yanatumika na walioolewa ili kudumisha ndoa zao.Kama kunautafiti huo, naomba tuhabarishane na kupeana rejea ili tuusake tujisomee wenyewe.
Ukipiga hesabu ya gharama inayotumika, muda, na kinachotokana na hiyo KP nadhani kwa wale wachumi watasema ni kutupa pesa kwenye shimo.Lakini kwa wanajamii watasema hapana.Hii ni fursa ya akina mama kutandaa ( networking), kujirusha na kuondoa stress - hata kama kinachopatikana hapo kwa maana ya kudumisha ndoa ya mtarajiwa ni nil.
Ninayo mengi ya kuongea lakini nisimalize uhondo - nawaachia na wengine watoe maoni yao.
Je- KP hizi zina tija na mwelekeo unafaa?