MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Takriban wiki mbili zilizopita, siku ya Jumatatu, kituo cha habari cha kimataifa, Al Jazeera, kilitangaza kipindi chake cha Witness Special, ambacho ni kawaida kutangazwa siku hiyo kila wiki.
Siku hiyo, kipindi hicho kilichotangazwa kiliitwa MITUMBA, na kilionesha safari ndefu ya fulana ya michezo iliyokuwa ikimilikiwa na mtoto wa nchini Uholanzi - kama sikosei - ambayo ilitolewa kama msaada (donation) pamoja na nguo nyingine zilizotolewa na familia ya mtoto huyo. Huko ulaya, ni kawaida kwa wazungu kutoa nguo kama michango kwa nchi zinazoendelea (?), ambayo inakusanywa na taasisi (?) zinazodai kwamba nguo hizo zinaletwa Afrika kama misaada, kinyume na ukweli kwamba ZINAUZWA. Ndio, hata wazungu nao ni mafisadi pia! Mwashangaa nini?
Kipindi cha Al Jazeera kilifichua ukweli huu, lakini, cha kushangaza, ITV walikatisha kipindi hicho kabla hakijakamilika, kwa kile kilichotafsiriwa kwamba ni aibu kwetu sisi kuonekana tunavaa mitumba. Fulana ya mtoto wa kizungu hatimaye ilikuja kuishia mkoani Iringa, ITV walikatisha kipindi hicho wakati wa awamu ya mwisho ya kipindi hicho, pale yalipokuwa yakifanyika mahojiano kati ya mtangazaji/mwandishi wa kipelelezi, aliyeandaa kipindi hicho, na mfanyabiashara wa mitumba anayeishi mjini Iringa.
Kwa wale ambao walikosa kuona kipindi hicho, tembeleeni YouTube kupitia anuani hii
Asanteni.
Pamoja tutafika!
./Mwana wa Haki
Siku hiyo, kipindi hicho kilichotangazwa kiliitwa MITUMBA, na kilionesha safari ndefu ya fulana ya michezo iliyokuwa ikimilikiwa na mtoto wa nchini Uholanzi - kama sikosei - ambayo ilitolewa kama msaada (donation) pamoja na nguo nyingine zilizotolewa na familia ya mtoto huyo. Huko ulaya, ni kawaida kwa wazungu kutoa nguo kama michango kwa nchi zinazoendelea (?), ambayo inakusanywa na taasisi (?) zinazodai kwamba nguo hizo zinaletwa Afrika kama misaada, kinyume na ukweli kwamba ZINAUZWA. Ndio, hata wazungu nao ni mafisadi pia! Mwashangaa nini?
Kipindi cha Al Jazeera kilifichua ukweli huu, lakini, cha kushangaza, ITV walikatisha kipindi hicho kabla hakijakamilika, kwa kile kilichotafsiriwa kwamba ni aibu kwetu sisi kuonekana tunavaa mitumba. Fulana ya mtoto wa kizungu hatimaye ilikuja kuishia mkoani Iringa, ITV walikatisha kipindi hicho wakati wa awamu ya mwisho ya kipindi hicho, pale yalipokuwa yakifanyika mahojiano kati ya mtangazaji/mwandishi wa kipelelezi, aliyeandaa kipindi hicho, na mfanyabiashara wa mitumba anayeishi mjini Iringa.
Kwa wale ambao walikosa kuona kipindi hicho, tembeleeni YouTube kupitia anuani hii
Asanteni.
Pamoja tutafika!
./Mwana wa Haki
Last edited by a moderator: