Kipimo cha mkojo kinaonyesha hivi:.numerous pus cells

Slave

JF-Expert Member
Dec 6, 2010
5,314
2,635
Nasikia maumivu wakati wa kukoja nimeenda kupima majibu ndo hayo: numerous pus cell urine :seem no ova no parasite. Je? Hilo gonjwa gani? Na nini dawa yake.
 
Uwezekano mkubwa ni kwamba una urinary tract infection (UTI) kwa sababu ya hiyo pus cells na maumivu wakati wa kukojoa. Hivyo waweza kutumia dawa inayopatikana kirahisi kama Ciprofloxacin 500mg 12hrly for 10 days na pia waweza kuongeza na aina fulani ya solution (nimesahau generic name yake) ila Tz ipo kibiashara inaitwa Cital solution 15mls 12hrly for 5 days.
N:B Si mara zote ukiwa na pus cells kwenye mkojo basi una UTI. unashauriwa kufanya urine culture. Ukiwa na sterile pyuria inawezekana ukawa na TB.
 
Uwezekano mkubwa ni kwamba una urinary tract infection (UTI) kwa sababu ya hiyo pus cells na maumivu wakati wa kukojoa. Hivyo waweza kutumia dawa inayopatikana kirahisi kama Ciprofloxacin 500mg 12hrly for 10 days na pia waweza kuongeza na aina fulani ya solution (nimesahau generic name yake) ila Tz ipo kibiashara inaitwa Cital solution 15mls 12hrly for 5 days.
N:B Si mara zote ukiwa na pus cells kwenye mkojo basi una UTI. unashauriwa kufanya urine culture. Ukiwa na sterile pyuria inawezekana ukawa na TB.

ops!! Hapo uwezekano wa kuwa na TB.nimeshtuka kidogo maana ni kama miaka mitano tu nimetoka kwenye huo ugonjwa wa tb ya mapafu.naanza kupata hofu inawezekana imerudi.kuhusu kutumia hizo dawa nilitumia cpro+fragn+dawa flani hivi ipo covered.nilipata nafuu ya wiki moja tu na baadae ugonjwa ukarudi tena. Mwanzo nilizani gonjwa linalotokana na kujamiiana.
 
Sasa mtumwa, unaonaje ukipata majibu ya maabara ukamuonesha dr hapo hapo akupe ushauri? Manake haya matibabu ya mtandaoni yanatakiwa kukuelewesha tu kile ambacho dr hajakuelewesha uzuri, kama sio kukushauri pa kuanzia
 
Sasa mtumwa, unaonaje ukipata majibu ya maabara ukamuonesha dr hapo hapo akupe ushauri? Manake haya matibabu ya mtandaoni yanatakiwa kukuelewesha tu kile ambacho dr hajakuelewesha uzuri, kama sio kukushauri pa kuanzia

king'ast jana nilikuwa najaribu kuku pm kwa bahati mbaya simu niliyokuwa natumia ilikuwa haina chaji hivyo ikawa inazima.ngoja niwashe pc then niku pm.
 
Uwezekano mkubwa ni kwamba una urinary tract infection (UTI) kwa sababu ya hiyo pus cells na maumivu wakati wa kukojoa. Hivyo waweza kutumia dawa inayopatikana kirahisi kama Ciprofloxacin 500mg 12hrly for 10 days na pia waweza kuongeza na aina fulani ya solution (nimesahau generic name yake) ila Tz ipo kibiashara inaitwa Cital solution 15mls 12hrly for 5 days.
N:B Si mara zote ukiwa na pus cells kwenye mkojo basi una UTI. unashauriwa kufanya urine culture. Ukiwa na sterile pyuria inawezekana ukawa na TB.[/

Usitumie dawa yoyote bila kuonana na dr dawa za kuandikiwa hasa kwenye mtandao zinaweza kukuletea madhara zaidi, mf. huyo anaekuandikia atajuaje kama una allergy na hiyo dawa anayokuandikia? Inawezekana dawa hiyo ilishawahi kumsaidia mwingi lakin haina maana na ww itakusaidia.
Kingine ni kuwa kuna haja ya kuongea na dr ana kwa ana ili akupe ushauri na kujua kwa nini tatzo linajirudia, ni bora pia ufanye vipimo vingne km utakavyoshauriwa na dr.
 
Uwezekano mkubwa ni kwamba una urinary tract infection (UTI) kwa sababu ya hiyo pus cells na maumivu wakati wa kukojoa. Hivyo waweza kutumia dawa inayopatikana kirahisi kama Ciprofloxacin 500mg 12hrly for 10 days na pia waweza kuongeza na aina fulani ya solution (nimesahau generic name yake) ila Tz ipo kibiashara inaitwa Cital solution 15mls 12hrly for 5 days.
N:B Si mara zote ukiwa na pus cells kwenye mkojo basi una UTI. unashauriwa kufanya urine culture. Ukiwa na sterile pyuria inawezekana ukawa na TB.[/

Usitumie dawa yoyote bila kuonana na dr dawa za kuandikiwa hasa kwenye mtandao zinaweza kukuletea madhara zaidi, mf. huyo anaekuandikia atajuaje kama una allergy na hiyo dawa anayokuandikia? Inawezekana dawa hiyo ilishawahi kumsaidia mwingi lakin haina maana na ww itakusaidia.
Kingine ni kuwa kuna haja ya kuongea na dr ana kwa ana ili akupe ushauri na kujua kwa nini tatzo linajirudia, ni bora pia ufanye vipimo vingne km utakavyoshauriwa na dr.
 
haya kaka, nakusubiria ngoja nitandike jamvi kabisaa!
ila uende kwa dr banaa, wenzenu watakula wapi jamani?kha!
king'ast jana nilikuwa najaribu kuku pm kwa bahati mbaya simu niliyokuwa natumia ilikuwa haina chaji hivyo ikawa inazima.ngoja niwashe pc then niku pm.
 
haya kaka, nakusubiria ngoja nitandike jamvi kabisaa!
ila uende kwa dr banaa, wenzenu watakula wapi jamani?kha!

ok umesomeka vyema.kuhusu hao wenzetu watakula walipo peleka mbogo.au unaonaje?
 
Usitumie dawa yoyote bila kuonana na dr dawa za kuandikiwa hasa kwenye mtandao zinaweza kukuletea madhara zaidi, mf. huyo anaekuandikia atajuaje kama una allergy na hiyo dawa anayokuandikia? Inawezekana dawa hiyo ilishawahi kumsaidia mwingi lakin haina maana na ww itakusaidia.
Kingine ni kuwa kuna haja ya kuongea na dr ana kwa ana ili akupe ushauri na kujua kwa nini tatzo linajirudia, ni bora pia ufanye vipimo vingne km utakavyoshauriwa na dr.

Ni kweli tunashauri mgonjwa asitumie dawa bila kupata ushauri wa daktari ila hatusemi usitumie dawa bila kumuona daktari usoni. Kuona ni bora kuliko kusikia, lakini kusikia pia hutosha kwa baadhi ya magonjwa ambayo yamkini hata kama ungekuwa na mgonjwa mbele yako usingefanya chochote zaidi ya kuchukua history tu. Hapa, ndio maana hata mtandao waweza kuwa tosha ilimradi uwe na taarifa zote za muhimu kama majibu ya maabara, picha za vipimo n.k. Nadhani sasa tulishaingia ulimwengu wa Telemedicine. Kusema hivyo hata mtu akiwa ana allergy ya dawa fulani si kwamba ukimuona usoni ndio utajua ana allergy ya dawa husika, kwani atakupa historia ya allergy kwa simulizi au kwa kuona mwenyewe baada ya kuanza kutumia dawa. Lakini tuna magonjwa mengi ambayo unahitaji ufanye physical examination kabla ya kufika kwenye jibu (mfano mdogo rahisi ni magonjwa ya ngozi), lakini bado tuna magonjwa ambayo unaweza ukatoa consultation kwa simu tu na ikatosha kabisa.
Nasikia maumivu wakati wa kukoja nimeenda kupima majibu ndo hayo: numerous pus cell urine :seem no ova no parasite. Je? Hilo gonjwa gani? Na nini dawa yake.
Tukirudi kwa mgonjwa wetu, unaweza ukafanya vipimo vizuri kama urinalysis nzuri, sio ya kutumia dip sticks tu halafu pia mfanyaji awe mzuri katika matumizi ya darubini ili kuleta majibu ya uhakika kama ya casts, protein na vitu vingine muhimu. Urine culture ni muhimu sana pamoja na cystoscope. Usifikirie TB tu kwa kuwa niliandika (kuna magonjwa mengi ambayo ilikuwa ngumu kuandika kwa simu) maana wengine huwa na Interstitial Cystitis, Prostatitis, na Urethritis ambazo huwa na dalili hizohizo pia ambapo moja wa sababu yake huwa ni magonjwa ya zinaa kama gono n.k. (Sio kwa Interstitial Cystitis). Kama imekuwa chronic ni vizuri ukipata ushauri toka kwa urologist na internal medicine specialist.
Mkuu pima na HIV maana nyemelezi tayari
Mimi sipendi daktari akimbilie kupima HIV mara anapokutana na mgonjwa ambaye hajafikia diagnosis. Madaktari wengi wakishajua unaumwa HIV uwezo wao wa kufikiria hukomea hapo (huganda) na hivyo hata kama una ugonjwa nyemelezi au sio nyemelezi wanaishia kutoufahamu na hivyo kutotoa tiba sahihi kwa kuwa kila kitu kwa wao kitaelezewa na HIV wakati sio sahihi. Tibu ugonjwa unaomsumbua mgonjwa kwanza kwa muda husika kama kuna umuhimu wa kumpima HIV fanya hivyo, ila usijifiche kwenye mgongo wa HIV.
 
Ozzie nimependa ushauri wako kuhusu HIV. Of recently tumepoteza ndugu yetu kwa kile nilichokiona kuwa madaktari hawakujishughulisha kisa ni muathirika. Alikuwa kwenye ARV lkn wakakomalia kuwa hatumii vizuri. Mgonjwa hakuwa serious wakati anaenda hospt lkn akadevelop aneimia akiwa hapo na kufariki after 10 days. FBP ilionesha platelets zimepungua, hakuwa na kifua wala pnemonia. It is so sad hizi hospital zetu. Yaani ukiwa na HIV madaktari wenyewe ni kama wanakuandikia death sentence!
 
Ozzie;

Ni kwa nini mabinti wa siku hizi wanapata sana UTI?
Kuna mtu aliniambia wasichana hawapendi kunywa maji hivyo ni rahisi sana kwa wao kupata UTI
Na wasichana wanasema hawapendi kunywa maji kwa sababu hawapendi kukojoa mara kwa mara cz wanaogopa kupata UTI kutoka public toilets.
So wats ur advice on this?
 
untitled.JPG majibu ya jana hayo wataaram.
 

Attachments

  • BUZ 011.jpg
    BUZ 011.jpg
    164.3 KB · Views: 148
... Mkuu Slave,labda walikupima then hawajakupa majibu mengine:
inaonyesha
>ulipimwa mkojo majibu kama hayo
>ukapimwa na kaswende [majibu ni negativu]
> na hiyo hapo chini
'Sero- negative'ndo kipimo cha HIV... So ur HIV negative kulingana na aliekupima.

mkuu fafanua.au unamaanisha kwamba nikienda kupimwa mahala pengine majibu yanaweza kubadilika? Kama ndivyo basi watakuwa hawatutendei haki.binafs nimepima zaidi ya 4 times na sehemu tofauti.
 
mkuu fafanua.au unamaanisha kwamba nikienda kupimwa mahala pengine majibu yanaweza kubadilika? Kama ndivyo basi watakuwa hawatutendei haki.binafs nimepima zaidi ya 4 times na sehemu tofauti.

.... Teh teh teh ! Kuwa na imani Mkuu! Majibu yatakuwa hayo hayo kwa misingi ifuatayo:
>>Kwa vipimo tunavyotumia zaidi Bioline SD au determine majibu hurudiwa kupimwa baada ya miezi 3 toka kipimo cha awali.
,Reason behind ni kwamba, huwa vinasoma positive wiki 6 au zaidi baada ya maambukizo. Kwa mfano,kama mtu alipima ilhali siku chache nyuma ndo alipata maambukizi havitaonyesha hadi baada ya muda huo. So kama bado una hofu subiri baada ya miezi 3 ukacheki tena. Na katika kipindi hiki unatakiwa kufanya protective sex ili usipate maambukizi hapa katikati. Huu ni ushauri wa kukuondolea hofu,lakini mimi ningekuwa wewe kwa vipimo vyote hivi vi4 nisingehangaika tena,labda kama ningekuwa nimejichafua kwa mtu nisiyemwamini hapa katikati.
>>>Japo kwa sasa pia kwenye Health Facilities chache kuna kipimo kinachoweza kutoa majibu sahihi within 2weeks kutoka siku unayohofia kupata maambukizo,jina lake limenitoka kidogo,ila kama sikosei,kinacheki RNA/DNA ya HIV kama ipo au la.
......SATISFIED MKUU?!
 
mkuu fafanua.au unamaanisha kwamba nikienda kupimwa mahala pengine majibu yanaweza kubadilika? Kama ndivyo basi watakuwa hawatutendei haki.binafs nimepima zaidi ya 4 times na sehemu tofauti.


... Sorry for later reply,nilikuwa nje ya mtandao.

>>> Naomba uamini majibu uliyopewa mkuu. Labda lugha niliotumia [neno "kwa mujibu"],limekutoa nje ya mstali... Let say nimelitumia kimakosa kwa bahati mbaya. Na nimefanya hivyo,kwa kuwa siyo mimi niliekupima !
Bahati mbaya zaidi TZ,watu wengi wanaopima,hasa HIV na Typhoid,wakipewa majibu ya negative huwa hawaamini,hadi wapime mara 2 au zaidi, sehemu tofauti...UWONGO ?!
 
Back
Top Bottom