Jafari Haruna
JF-Expert Member
- Jun 18, 2017
- 347
- 962
Narudia tena ni Udhalilishaji, Upuuzi, Ushenzi, Uchonganishi na Utapeli.
Nimefika mkoa wa Kigoma Tokea Majuzi nilicho Kikuta huku Sielewi Huku ninchi Nyingine au ni Tanzania hii hii !
Kuna kitu kinaitwa KAMCHAPE, hawa wapuuzi nani kawaleta, Hili kweli nani kalipa Baraka kufanyika karibu mkoa mzima wa Kigoma?
Kinachofanyika Ni Udhalilishaji na Uchonganishi kwa jamii.
Kwanza Wanachangisha Tsh 5,000 kila kaya kwa lazima sio ombi.
Kisha Wanapita kila nyumba Eti wanatoa Uchawi na wachawi! Tena utake usitake lazima.
Wakifika kwako wanasema hapa kuna uchawi Lazima uchapwe kisha unanyolewa Nywele Mbele ya umati wa watu kisha kunyweshwa Kile wanachoKiita Dawa hautakuwa mchawi tena!
Nimefuatilia kinachofanyika pale ni Mazinga Ombwe na Kujipatia Pesa kwa Utapeli!
Wakati Yakifanyika hayo Kijiji Jirani, Nyie mnaanza jiandaa na kama mwenyekiti hata Wakaribisha hao watu au kuchangisha hizo pesha kila kaya naye Anajumuishwa kwenye Kundi moja la Wachawi !
Kuna vitu vya Ajabu sana Vinafanyika mpaka nimeshikwa na Butwaa. Nimeuliza nikaambiwa Serikali Ndio Imeruhusu hili Lifanyike Mkoa mzima kweli?
Mbona Sioni Dodoma na Mbeya Kwanini Kigoma?
Kwasasa zoezi limepamba Moto Vijiji vya Nyarubanda, Kalinzi, Mukigo, Muhinda, Nyaruboza, Rukoma, Igalula, Mgambo, Katumbi, Kalya Nk.
Huko kumechafukwa hali ni mbaya na lisipofanyiwa kazi na kuacha litaleta shida kwa watu
======================
UPDATE: 13/09/2023
Hatimaye Jeshi la Polisi limeingilia Kati jambo Hili
Pia soma
- Mfahamu 'Kamchape' mkamata wachawi na shughuli zake kwa ujumla kutokea hapa Mkoani Kigoma
Nimefika mkoa wa Kigoma Tokea Majuzi nilicho Kikuta huku Sielewi Huku ninchi Nyingine au ni Tanzania hii hii !
Kuna kitu kinaitwa KAMCHAPE, hawa wapuuzi nani kawaleta, Hili kweli nani kalipa Baraka kufanyika karibu mkoa mzima wa Kigoma?
Kinachofanyika Ni Udhalilishaji na Uchonganishi kwa jamii.
Kwanza Wanachangisha Tsh 5,000 kila kaya kwa lazima sio ombi.
Kisha Wanapita kila nyumba Eti wanatoa Uchawi na wachawi! Tena utake usitake lazima.
Wakifika kwako wanasema hapa kuna uchawi Lazima uchapwe kisha unanyolewa Nywele Mbele ya umati wa watu kisha kunyweshwa Kile wanachoKiita Dawa hautakuwa mchawi tena!
Nimefuatilia kinachofanyika pale ni Mazinga Ombwe na Kujipatia Pesa kwa Utapeli!
Wakati Yakifanyika hayo Kijiji Jirani, Nyie mnaanza jiandaa na kama mwenyekiti hata Wakaribisha hao watu au kuchangisha hizo pesha kila kaya naye Anajumuishwa kwenye Kundi moja la Wachawi !
Kuna vitu vya Ajabu sana Vinafanyika mpaka nimeshikwa na Butwaa. Nimeuliza nikaambiwa Serikali Ndio Imeruhusu hili Lifanyike Mkoa mzima kweli?
Mbona Sioni Dodoma na Mbeya Kwanini Kigoma?
Kwasasa zoezi limepamba Moto Vijiji vya Nyarubanda, Kalinzi, Mukigo, Muhinda, Nyaruboza, Rukoma, Igalula, Mgambo, Katumbi, Kalya Nk.
Huko kumechafukwa hali ni mbaya na lisipofanyiwa kazi na kuacha litaleta shida kwa watu
======================
UPDATE: 13/09/2023
Hatimaye Jeshi la Polisi limeingilia Kati jambo Hili
Pia soma
- Mfahamu 'Kamchape' mkamata wachawi na shughuli zake kwa ujumla kutokea hapa Mkoani Kigoma