ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Tathimini inaonyesha kuwa wanawake wengi wanaoolewa katika miaka hii wanashindwa katiba kuwatosheleza wenzi wao na wengi hujikuta wakiachika au kukosa mapenzi ya dhati kutokana na kujibweteka.
Dr. mmoja aliwahi kueleza kuwa amekuwa akipokea kesi nyingi za wanandoa kushindwa kutimiziana tendo la ndoa na hasa kina dada wengi kutojisikia kufanya mapenzi mara kwa mara na waume zao kwa kisingizio cha kuchoka na mihangaiko ya maisha. Hii imepelekea kuwepo kwa matatizo mengi ya uzazi hasa kuchelewa kwa wananandoa kupata watoto...
Kama umeaoa, tatafiti kwa mwenzio na unaweza kubaini mapungufu fulani.
Wanaume watatu ambao kila mmoja alielezea maisha na mwezi wake wanasema
Huyu alisema : "yaani kila ninaposikia hamu na kumgusa mwenzangua ana ng'aka na kuruka utadhani ameguswa na umemem .., atanguruma hapo kama simba, sitaki asieee mimi sitaki., nimechoka..mbona huelewi...mbona hunionei huruma mwenzio..?"
Mwengine alieleza "..sio tu anasema amechoka, bali anakuambia ..wewe kila saa tu unataka..jana ulifanya, leo tena ..unanichosha bwana...'...
Huyu mwingine anasema: "mimi ilifika wakati ikabidi niombe ushauri nasaha,nilihisi mwanzangu kapata mwanaume mwingine nje....yaani hazisikii kabisa kuwa na mimi...hataki kabisa, kazi imekuwa ndio kisingizio chake..ukimgusa tu...atakupa sababu kibao ambazo zinaweza kukukasirisha usiendelee nae...akiingia kitandani, usingizi mzito utadhani kapiga kilauli... sawa uenda amechoka lakini, kila siku hivyo hivyo?? pengine unajiuliza hivi ndoa ya nini na mtu kama huyu?"
Tathimini inaonyesha pia kuwa japo katika karne tuliypo Mungu ameendelea kutoa viumbe vikali kuliko karne zilizopita, lakini uzuri wa watoto wa kike wanaozaliwa sasa haudumu kwa muda mrefu kutokana na maisha wanayoishi. Hasa ya kupenda starehe, mapombe, vitimoto, kutembea kwenye magari muda mwingi, kushindwa kujishughulisha na kazi za nyumbani kwa kisingizio cha kuchoka hivyo kuajiri mabinti wenzao ili wawafanyie kazi nk. ...