nderingosha
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 4,281
- 3,243
- Kama tulivyotabiri baada ya uteuzi wa mchovu Philip Marmo kuwa balozi china
.tayari dalili za udhaifu wake kama balozi wa TZ uchina zimeshaanza kujitokeza kwa kasi ya ajabu
..China..nchi yenye uchumi imara na wa kasi zaidi duniani
.nchi yenye watu wajanja wajanja ambao wanatumia sana udhaifu wa wengine kujinufaisha
iwe kiuchumi kama nchi au hata kibinfsi
kila mtu kwa nafasi yake
Kwa muktadha huu
wengi walitegemea balozi wetu kule uchina awe mtu makini na aweze kulinda interests za TZ na watu wake kule uchina
.jambo ambalo linaonekana kuwa bado ni kitendawili kwa muda mfupi tu huyu jamaa aliokaa kule china
Nasema hivi kwani watu makini lazima wafatilie nyendo za utendaji wa ubalozi wetu kule china
.hasa ikizingatiwa kuwa kwasasa TZ imekuwa inafanya deals nyingi za kimagumashi kule china
rejea mikataba tata
.manunuzi tata
.biashara tata
.etc etc ..Mambo (indicators) machache yanayonifanya nianze kuhoji utendaji wa huyu balozi kule uchina ni kama ifuatavyo
- Tangu amefika uchina balozi Marmo mpaka sasa hajakutana wala angalau na watanzania walioko uchina .wawe wanafunzi au wafanya biashara ..sasa huyu anamsubiri rais JK aende uchina ndio akutane na watanzania au vipi???...yeye balozi anawakilisha interests za nani uchina kama mpaka sasa ameshindwa hata angalau kuitisha mkutano na watanzania????....nina taarifa kuwa kuna jitihada za wanafunzi kule uchina za kukutana na balozi lakini hakuna initiative yoyote toka kwa balozi mwenyewe ya kukutana na wanafunzi ..haswa ikizingitiwa kuwa yeye ni mgeni china na labda kuna mengi ya msingi ya kuisaidia TZ na pia kusaidia utendaji wake angeweza kujifunza toka kwa wanfunzi ambao ndio msingi mkubwa wa maendeleo ya TZ ..China ina wanafunzi wengi saana watanzania kuliko sehemu yoyote duniani ..hawa ni nguvu kazi ya kuangalia sana na ni hili ni jukumu la balozi
- Tayari kuna taarifa(hazijathibiishwa)kuwa kuna wafanyabiashara wamepigwa vibaya na wachina hivi majuzi kule Guanzhou mji ambao watanzania wengi wafanyabiashara hushukia na kuchukua mzigo .biashara kubwa kule kariakoo hutoka uchina haswa katika mji huu wa Guanzhou ..sasa kama kuna taarifa ya wafanyabiashara kupigwa kule hii si nzuri na tungetegemea kusikia tamko la ubalozi wa TZ kule uchina lakini kinyume chake tunasikia habari hizi kwenye magazeti..tena ya udaku .wakati kuna uwezekano kweli kuwa watanzania hawa wemepigwa ..soma habari hii (pamoja na kuwa yaweza kuwa udaku): WABONGO WALA KICHAPO CHINA - Global Publishers
- Kuna taarifa za wanafunzi wa kitanzania uchina kupata shida kubwa ku access mtandao wa bodi ya mikopo TZ..yaani OLAS .jambo lililopelekea wanafunzi kulalamika sana na hata kutuma habari bodi ya mikopo moja kwa moja .mpaka ikabidi wanafunzi wasaidiane wao kwa wao kwa kumtumia mwenzao ambaye ana direct contact na bodi ya mikopo haya yoote yamefanyika wakati ubalozi wa TZ kule uchina upo .Sasa ubalozi wa TZ unawakilisha interests za nani???kama jambo kama hili nalo wanafunzi wameona ubalozi ni helpless mpaka wakachukua jukumu wenyewe (kwa contacts zao)kuweza kusaidiana!!.......Kama balozi angekuwa ameonana na wanafunzi jambo hili angekuwa ameabiwa na kulifanyia kazi kwa wakati kwani halijatokea mara moja kwa wanafunzi hawa .na matokeo yake siku zote ni kwa wanafunzi hawa kucheleweshewa fedha zao za mikopo toka bodi ..
Kwa hizi indicators chache nilizotaja nashawishika kusema kuwa balozi Marmo bado amelala .na ni wakati sasa kwake kuamka na kuchapa kazi aliyotumwa..kwa kuanza na kushughulikia kero kadhaa zilizopo pamoja na kulinda maslahi ya TZ na watanzania kule uchina ..vinginevyo hatutamwamini kuwa anawakilisha interests za TZ uchina ..nawasilisha