GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Njmeshazisoma nyuzi kadhaa humu jamvini zinazohamasisha kilimo. Pamoja na kwamba ni nyuzi za kuvutia, kuna watu wameonekana kuwa na mashaka na hata kuwaita MOTIVATIONAL SPEAKERS watoa mada husika. Na wengine, katika kuonesha kutokukubaliana nao, huziita ni kilimo cha kwenye makaratasi.
Lakini ni kweli kilimo hakilipi?
Hivi majuzi nilimtembelea mkulima mmoja nchini Kenya. Yeye anajishughulisha na kilimo cha matunda mbalimbali, yakiwemo matunda yanayodaiwa kuuzwa ghali, DRAGONS. Na inawezekana kwa sababu hata mimi mwenyewe niliyanunua kadhaa humo shambani kwake kwa bei ya shambani , yaani, ya jumla. Niliuziwa tunda moja kwa Ksh 500/=. Nilichukua manne kwa Ksh 2,000/=.
Ingawa eneo lake si kubwa sana, lakini anaonekana kuwa na mafanikio katika shughuli zake hizo. Miundombinu iliyopo kwenye bustani yake, na hata wafanyakazi aliowaajiri, ni uthibitisho kuwa kazi yake inamlipa.
Mfanyakazi aliyepewa jukumu la kunitembeza bustanini, aliniambia kuwa robo eka ya shamba lililopandwa dragon fruits inaweza kuwaingizia hela ya Kenya sh milioni moja kwa mwaka. Ukiibadilisha kwa hela ya Kitanzania, ni zaidi ya million kumi na Sita. Na hiyo ni robo eka tu. Je akiwa na eka 20?
Huyo bwana ameisajili biashara yake ya ukulima wa matunda. Nilipofika bustanini hapo, niliwakuta wageni kadhaa akiwemo mtu wa mahesabu aliyeenda kumsaidia kuandaa ripoti ya masuala ya kodi. Wakati wa kuondoka, alitupeleka kwa gari lake hadi kituo cha mabasi.
Nilipata nafasi ya kubadilishana mawazo na huyo mhasibu ambapo nilipomwuliza kama ana mpango wa kujihusisha na kilimo, alisema anatafuta ardhi. Akipata kuanzia ekari 3, anakuwa mkulima wa "full time". Siyo eka 30, ni eka 3.
Aisee! Watanzania tuna fursa ambayo wengi hawajaijua!!!
Jibu lake, pamoja na nilichokishuhudia kwa huyo mkulima niliyemtembelea, imenifanya nitilie mashaka hoja kuwa kilimo hakilipi.
Ninashawishika kuamini kuwa kilimo kinalipa kikifanywa kwa mujibu wa kanuni zake.
Kama Wakenya wenye uhaba wa ardhi wamefanikiwa sana kwenye kilimo, sisi Watanzania tulio na ardhi tele yatupasa tuwe na mafanikio makubwa zaidi kuwazidi.
Najua kuna baadhi ya Watanzania ambao wameshaonesha kwa vitendo kuwa kilimo kinalipa, lakini bado wengi hawaliamini hilo.
Nihitimishe kwa kusema kuwa SIYO KWAMBA KILIMO HAKILIPI TANZANIA, BALI HAKILIPI KWA MTU YEYOTE ASIYEZINGATIA KANUNI STAHIKI.
Kilimo KINALIPA sana.
Lakini ni kweli kilimo hakilipi?
Hivi majuzi nilimtembelea mkulima mmoja nchini Kenya. Yeye anajishughulisha na kilimo cha matunda mbalimbali, yakiwemo matunda yanayodaiwa kuuzwa ghali, DRAGONS. Na inawezekana kwa sababu hata mimi mwenyewe niliyanunua kadhaa humo shambani kwake kwa bei ya shambani , yaani, ya jumla. Niliuziwa tunda moja kwa Ksh 500/=. Nilichukua manne kwa Ksh 2,000/=.
Ingawa eneo lake si kubwa sana, lakini anaonekana kuwa na mafanikio katika shughuli zake hizo. Miundombinu iliyopo kwenye bustani yake, na hata wafanyakazi aliowaajiri, ni uthibitisho kuwa kazi yake inamlipa.
Mfanyakazi aliyepewa jukumu la kunitembeza bustanini, aliniambia kuwa robo eka ya shamba lililopandwa dragon fruits inaweza kuwaingizia hela ya Kenya sh milioni moja kwa mwaka. Ukiibadilisha kwa hela ya Kitanzania, ni zaidi ya million kumi na Sita. Na hiyo ni robo eka tu. Je akiwa na eka 20?
Huyo bwana ameisajili biashara yake ya ukulima wa matunda. Nilipofika bustanini hapo, niliwakuta wageni kadhaa akiwemo mtu wa mahesabu aliyeenda kumsaidia kuandaa ripoti ya masuala ya kodi. Wakati wa kuondoka, alitupeleka kwa gari lake hadi kituo cha mabasi.
Nilipata nafasi ya kubadilishana mawazo na huyo mhasibu ambapo nilipomwuliza kama ana mpango wa kujihusisha na kilimo, alisema anatafuta ardhi. Akipata kuanzia ekari 3, anakuwa mkulima wa "full time". Siyo eka 30, ni eka 3.
Aisee! Watanzania tuna fursa ambayo wengi hawajaijua!!!
Jibu lake, pamoja na nilichokishuhudia kwa huyo mkulima niliyemtembelea, imenifanya nitilie mashaka hoja kuwa kilimo hakilipi.
Ninashawishika kuamini kuwa kilimo kinalipa kikifanywa kwa mujibu wa kanuni zake.
Kama Wakenya wenye uhaba wa ardhi wamefanikiwa sana kwenye kilimo, sisi Watanzania tulio na ardhi tele yatupasa tuwe na mafanikio makubwa zaidi kuwazidi.
Najua kuna baadhi ya Watanzania ambao wameshaonesha kwa vitendo kuwa kilimo kinalipa, lakini bado wengi hawaliamini hilo.
Nihitimishe kwa kusema kuwa SIYO KWAMBA KILIMO HAKILIPI TANZANIA, BALI HAKILIPI KWA MTU YEYOTE ASIYEZINGATIA KANUNI STAHIKI.
Kilimo KINALIPA sana.