Kilimanjaro: Naomba tumsaidie Mwanafunzi Sifika Daniely Ruben apate haki yake na arudi shule

Hakikisha na yeye hajakudanganya.
Sio tunasumbua watu kumbe mtoto hataki shule ama alifeli.
Nilisema hapa
Screenshot_20230926-081009_Instagram.jpg
 
Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

Amani ya Simu "TAMISEMI DODOMA Simu Nu: +255 26 2321667 Nus: +255 26 2322116 Barua pepe game..

Mi wa Sekalun

Maa TAMISEM SLP 1823

TAARIFA KWA UMMA

Ofisi ya Rais -TAMISEMI imma taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikinahusisha mwanafunzi SIFIKA DANIEL RUBEN aliyesoma Shule ya Sekondari ya Mkombozi iliyoka Wilaya ya Samani Kilimanjaro na kupangwa kidato cha tano kwenye shule ya Sekondari Nawa nafasi yake amepewa mwanafunzi mwingine hivyo yeye kukosa haki ya kuendelea na m

Ofisi ya Rais-TAMISEMI imefuatilia taarifa hizo kwa kina kutoka Mlambon Sekondari alikosema mwanafunzi huyo (O'level) mpaka shule ya Sekondari Namwai diyoko Scha mkoani Kilimanjaro alikopangiwa mwanafuzi baryo kuendelea na masomo ya kidato cha tano

Imebainika kuwa binti anayelalamika mitandoni anaitwa Sifaeli Tawel Elirehoma na aliona shule moja

Sika Daniel Rubern. Hata hivyo binti huyo namba yake ya Mtihani ilikuwa ni 8.850/135 alipata

Dis IV: 34 (Zero) na ama masomo ya Sanaa ilihali Sifika Daniel Raben umba yake ya mtihani ni

5.850/136 alisoma masomo ya Sayani na umepata Division 1.10.

Binti anayelalamika mitandaoni alifikishwa shuleni hapo na Wazazi Waler kompoti akiwa hata viambatanisho vyovyote (Result Slip) na alipohojiwa ilibainika kuwa amewadanganya wale wake a jina mpaka matokeo yake na kwa sababu walezi hao walimchukua kama mundi wa nyumbani hawakufahamu ukweli wa tarifa waliopewa na binti huyo

Kufuatia taarifa hii tunapenda kumjulisha umma kuwa hakuna mwanafizi aliyunyang'anywa haki yake ya kuendelea na masomo ya kidato cha tano na taarifa zilizotolewa na binti huyo ni za songo na zipurwe na mwanafunzi Sifika Daniel Ruben codes na masomo yake Nawai Sekondari.

Aidha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Mohamed O. Mchengerwa amewataka Wazazi Walezi na wanaharakati kutokusambaza taarifa ambazo hawajajiridhisha na usahihi wake il kepuka kuna haki kwenye jami

Imetolewa na:

Nteghenjwa Hosseah

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais-TAMISEMI 25.09.2023
Screenshots_2023-09-26-08-42-49.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu nafasi yake inauzwa afu anaenda kuwa hausigel,hayuko serious huyo

Hataki shule
Siyo hayuko siriaz umeshaambiwa Baba yake ni maskini sana na mama yake ni mgonjwa unadhani kwa umri huo angeenda wapi kulalamika?

Hii nchi kila mahali ili jambo lisogee ushikwe mkono au uwe na kitu mkononi sasa hivyo vyote hakuwa navyo angetoboa vipi?ila nichukue nafasi hii kumpongeza mama Gwajima anajitahidi sana kuwa active kwa mambo ya msingi ya kijamii (of course huko ccm naona wote wapiga debe na kujipendekeza lakini huyu mama kiasi anaujua wajibu wake ipasavyo)
 
Siyo hayuko siriaz umeshaambiwa Baba yake ni maskini sana na mama yake ni mgonjwa unadhani kwa umri huo angeenda wapi kulalamika?

Hii nchi kila mahali ili jambo lisogee ushikwe mkono au uwe na kitu mkononi sasa hivyo vyote hakuwa navyo angetoboa vipi?ila nichukue nafasi hii kumpongeza mama Gwajima anajitahidi sana kuwa active kwa mambo ya msingi ya kijamii (of course huko ccm naona wote wapiga debe na kujipendekeza lakini huyu mama kiasi anaujua wajibu wake ipasavyo)
Kwa hiyo bado unamini dogo kadhulumiwa haki yake?
 
Michezo hii ilikuwepo sana zamani...hadi waziri mmoja alishafanya na alishajitetea sana hapa ...
Mtoto huyu anahitaji msaada zaidi ya huo wa kurudishwa shule maana anatokea familia masikini sana..
Alafu badaye huyo aliyeuziwa jina
Anakuja kuwa kiongozi fulani wa nchi

Ova
 
Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda okoa mstakabali wa maisha ya binti huyu.

"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.

Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo. Nimeumia Kiukweli naomba nisaidie kwa wahusika binti apate haki yake, Mimi sina kipato kikubwa lakini kwa shule ya serikali nitamsomesha, lakini anapataje haki yake maana mimi kumpeleka shule binafsi uwezo sina.

Shule aliyomalizia Form Four ni MKOMBOZI SECONDARY SCHOOL ipo Hedaru Wilaya Ya Same. Shule aliyopangiwa aripoti Form Five Inaitwa NAMWAI HIGH SCHOOL Ipo Mkoa wa Kilimanjaro Sanya Juu,
Na Mchepuo aliopangiwa ni PCM
Namba yake ya Mtihani ni S.P. 0708/0136

Naomba Nisaidie Huyu Mtoto apate haki Yake Arudi shule Mimi nilitaka mfanyakazi ndo nimeletewa Huyo na Moyo wangu Umekosa Amani Nafasi yake Imeuzwa Kisa Alichelewa Kurepoti shule Wazazi wake Hawana Msaada Tena Maana Baba yake ni masini kabisa, na Mama Yake mzazi kwa sasa ni Mgojwa. Naomba Nisaidie apate hake yake Mimi Nitamsomesha Kwa hikihili kipato changu kidogo Nilichojaliwa".

Nimeitoa kwa Yericko Nyerere

View attachment 2761440View attachment 2761442


=====

UPDATES;

======
Napenda kutoa shukrani za dhati kwa Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na Watoto, Mh Doroth Gwajima kwa kuchukua hatua kwa haraka baada ya taarifa ya binti anayehitaji msaada wa kuendelea na masomo kitato cha tano baada ya mgogoro wa nafasi yake na shule aliyochaguliwa kujiunga.

Pia nimshukuru Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda ambae amechukua jukumu la kuwasiliana nami, na kuahidi kuwa Wizara imelichukua na ufumbuzi utapatikana haraka iwezekanavyo.

Lakini niwashukuru wadau kwa mamna mlivyolipokea na Wengine wameguswa hadi kufikia hatua ya kuwa tayari kumsomesha binti huyu kwa namna wawezavyo. Ni hatua muhimu sana ya kizalendo na ya kusaidiana kama Watanzania.

Kwasasa suala hili liko chini y Wizara hizi mbili, Tuziache zishughulikie na kutafuta ukweli wa mgogoro huu, na Haki ya mabinti hawa wawili (aliyechukua nafasi ya SIFIKA DANIEL RUBEN, na SIFIKA mwenyewe) wapate haki yao ya msingi ya kupata elimu bila kujalisha nani alifaulu au hakufaulu.

Lakini pia Viongozi wa Shule za Mkombozi Secondary na Namwai High School, Viongozi wa Elimu Wilaya na Mkoa, toeni ushirikiani kwa mamlaka bila kujalisha nyinyi ni walalamikiwa wa jambo hili. Muhimu zaidi ni mabinti hawa wapate elimu zao.

Na Yericko Nyerere.

Pia soma: Taarifa kutoka shule ya Sekondari Mkombozi alikosoma Sifika Danieli Rubeni.
 

Attachments

  • IMG-20230926-WA0070.jpg
    IMG-20230926-WA0070.jpg
    44.6 KB · Views: 4
Back
Top Bottom