Boss la DP World
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 1,997
- 7,552
Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda okoa mstakabali wa maisha ya binti huyu.
"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.
Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo. Nimeumia Kiukweli naomba nisaidie kwa wahusika binti apate haki yake, Mimi sina kipato kikubwa lakini kwa shule ya serikali nitamsomesha, lakini anapataje haki yake maana mimi kumpeleka shule binafsi uwezo sina.
Shule aliyomalizia Form Four ni MKOMBOZI SECONDARY SCHOOL ipo Hedaru Wilaya Ya Same. Shule aliyopangiwa aripoti Form Five Inaitwa NAMWAI HIGH SCHOOL Ipo Mkoa wa Kilimanjaro Sanya Juu,
Na Mchepuo aliopangiwa ni PCM
Namba yake ya Mtihani ni S.P. 0708/0136
Naomba Nisaidie Huyu Mtoto apate haki Yake Arudi shule Mimi nilitaka mfanyakazi ndo nimeletewa Huyo na Moyo wangu Umekosa Amani Nafasi yake Imeuzwa Kisa Alichelewa Kurepoti shule Wazazi wake Hawana Msaada Tena Maana Baba yake ni masini kabisa, na Mama Yake mzazi kwa sasa ni Mgojwa. Naomba Nisaidie apate hake yake Mimi Nitamsomesha Kwa hikihili kipato changu kidogo Nilichojaliwa".
Nimeitoa kwa Yericko Nyerere
=====
UPDATES;
======
Napenda kutoa shukrani za dhati kwa Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na Watoto, Mh Doroth Gwajima kwa kuchukua hatua kwa haraka baada ya taarifa ya binti anayehitaji msaada wa kuendelea na masomo kitato cha tano baada ya mgogoro wa nafasi yake na shule aliyochaguliwa kujiunga.
Pia nimshukuru Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda ambae amechukua jukumu la kuwasiliana nami, na kuahidi kuwa Wizara imelichukua na ufumbuzi utapatikana haraka iwezekanavyo.
Lakini niwashukuru wadau kwa mamna mlivyolipokea na Wengine wameguswa hadi kufikia hatua ya kuwa tayari kumsomesha binti huyu kwa namna wawezavyo. Ni hatua muhimu sana ya kizalendo na ya kusaidiana kama Watanzania.
Kwasasa suala hili liko chini y Wizara hizi mbili, Tuziache zishughulikie na kutafuta ukweli wa mgogoro huu, na Haki ya mabinti hawa wawili (aliyechukua nafasi ya SIFIKA DANIEL RUBEN, na SIFIKA mwenyewe) wapate haki yao ya msingi ya kupata elimu bila kujalisha nani alifaulu au hakufaulu.
Lakini pia Viongozi wa Shule za Mkombozi Secondary na Namwai High School, Viongozi wa Elimu Wilaya na Mkoa, toeni ushirikiani kwa mamlaka bila kujalisha nyinyi ni walalamikiwa wa jambo hili. Muhimu zaidi ni mabinti hawa wapate elimu zao.
Na Yericko Nyerere.
Pia soma: Taarifa kutoka shule ya Sekondari Mkombozi alikosoma Sifika Danieli Rubeni.
"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.
Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo. Nimeumia Kiukweli naomba nisaidie kwa wahusika binti apate haki yake, Mimi sina kipato kikubwa lakini kwa shule ya serikali nitamsomesha, lakini anapataje haki yake maana mimi kumpeleka shule binafsi uwezo sina.
Shule aliyomalizia Form Four ni MKOMBOZI SECONDARY SCHOOL ipo Hedaru Wilaya Ya Same. Shule aliyopangiwa aripoti Form Five Inaitwa NAMWAI HIGH SCHOOL Ipo Mkoa wa Kilimanjaro Sanya Juu,
Na Mchepuo aliopangiwa ni PCM
Namba yake ya Mtihani ni S.P. 0708/0136
Naomba Nisaidie Huyu Mtoto apate haki Yake Arudi shule Mimi nilitaka mfanyakazi ndo nimeletewa Huyo na Moyo wangu Umekosa Amani Nafasi yake Imeuzwa Kisa Alichelewa Kurepoti shule Wazazi wake Hawana Msaada Tena Maana Baba yake ni masini kabisa, na Mama Yake mzazi kwa sasa ni Mgojwa. Naomba Nisaidie apate hake yake Mimi Nitamsomesha Kwa hikihili kipato changu kidogo Nilichojaliwa".
Nimeitoa kwa Yericko Nyerere
=====
UPDATES;
======
Napenda kutoa shukrani za dhati kwa Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na Watoto, Mh Doroth Gwajima kwa kuchukua hatua kwa haraka baada ya taarifa ya binti anayehitaji msaada wa kuendelea na masomo kitato cha tano baada ya mgogoro wa nafasi yake na shule aliyochaguliwa kujiunga.
Pia nimshukuru Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda ambae amechukua jukumu la kuwasiliana nami, na kuahidi kuwa Wizara imelichukua na ufumbuzi utapatikana haraka iwezekanavyo.
Lakini niwashukuru wadau kwa mamna mlivyolipokea na Wengine wameguswa hadi kufikia hatua ya kuwa tayari kumsomesha binti huyu kwa namna wawezavyo. Ni hatua muhimu sana ya kizalendo na ya kusaidiana kama Watanzania.
Kwasasa suala hili liko chini y Wizara hizi mbili, Tuziache zishughulikie na kutafuta ukweli wa mgogoro huu, na Haki ya mabinti hawa wawili (aliyechukua nafasi ya SIFIKA DANIEL RUBEN, na SIFIKA mwenyewe) wapate haki yao ya msingi ya kupata elimu bila kujalisha nani alifaulu au hakufaulu.
Lakini pia Viongozi wa Shule za Mkombozi Secondary na Namwai High School, Viongozi wa Elimu Wilaya na Mkoa, toeni ushirikiani kwa mamlaka bila kujalisha nyinyi ni walalamikiwa wa jambo hili. Muhimu zaidi ni mabinti hawa wapate elimu zao.
Na Yericko Nyerere.
Pia soma: Taarifa kutoka shule ya Sekondari Mkombozi alikosoma Sifika Danieli Rubeni.