Kilaini: Kikwete bado ni chaguo la Mungu

Nikijaribu kuangalia hii post yako ninahisi kutapika kwani inanuka udini mtupu. ninafikiri in short unataka kuwaambia waislamu wote wasimchague yeyote asiyekuwa muislamu.Udini wako hautatupeleka kokote.Ni lazima tuwaingize madarakani wanamapinduzi wa Pipoooooooooos Pawaaaaaaaaaaaa.
 
KAMA NAKUPATAPATA HALAFU UNANITOKA HV YAANI SIKUELEWIELEWI,
UTAKUWA UNALETA MAMBO YANAYOKATAZWA HAPA EEH!:shut-mouth::shut-mouth:
 
Hili li-article lako hakuna atakayelisoma. Umeliandika ovyo sana. Weka aya, na maandishi makubwa zaidi kidogo.

Wewe ndiyo Shekhe Yahaya wa ukumbi huu ama ndiyo nani? Si useme ukweli tu kuwa kama unataka usifiwe lazima ubandike post za kuisifia Chadema na mgombea wao wa urais. :hand:
 
Jibuni hoja nyiye Wagalatia msiokuwa na akili. Badala ya kama huyu farasi/twigammmmmmmmmmhhhhhh......................
.

udini sasa tumevamiwa.........
hatujali kama raisi ni mwislam au mkristo.........
tunachojali ni kitu kimoja tuu.......
tupate mtu aliyejitolea mhanga kuwaondoa wataanzania hapa walipo na kuwasogeza mbele kidogo tuu hata tufikie theluthi ya MDG's mwaka 2015.
.........aslaani.........
hakuna mwingine zaidi ya DR WILBROAD SLAA.
 
Tanzania ni mfano mzuri. Pamoja na jitihada kubwa sana zinazoendelea usiku na mchana za kumtukuza Mwal. Julius Kambarage Nyerere, Nyerere alikuwa ni mmoja wa viongozi hao. Mwandishi Jan P van Bergen katika kitabu chake Development and religion in Tanzania, amefichua taarifa za kikao cha siri Ikulu ya Dar es Salaam mnamo Agosti 3, 1970 kati ya Rais Julius Nyerere, Padri Robert Rweyemamu na muwakilishi wa Papa, Giovanni Cerrano. Kwa mujibu wa van Bergen, katika kikao hicho Nyerere aliwaeleza viongozi wake wa dini kuwa ameunda idara ya elimu ya siasa katika TANU na amemuweka Padri aiongoze kwa sababu ya imani yake madhubuti. Aliwaeleza pia kuwa katika Kamati kuu ya chama ameweka Mapadri lengo likiwa kulipa Kanisa fursa na uwezo mkubwa hapa Tanzania.

..sasa turudi basi tuhakiki kama in 1970 Kamati Kuu ya Tanu ilikuwa imesheheni Mapadri.

..zaidi, hivi mwandishi ana uhakika kwamba ktk wagombea Uraisi mwenye kashfa ya ngono ni Dr.Slaa peke yake? amesahau sakata ya Lipumba na Georgina?

..mwandishi angejielekeza ktk kuchambua sera na utekelezaji wake, siyo kuandika makala yenye mashambulizi ya udini.

NB:

..mwandishi anaweza vipi kuitambulisha Zanzibar iliyokuwa ikiendesha biashara ya utumwa kama nchi ya Kiislamu?

..kwa uelewa wangu mamlaka iliyohalalisha utumwa haiwezi kutambulishwa na Uislamu wala Ukristo.
 
Duuuuu, anyway acha niseme,Unamaanisha nini unaposema watu fulani wana daraja la kwenda kwa Mungu wao? Waache walivyo maana hata wewe hujui vizuri mambo ya kiroho haya. Kwa namna ingine unasema Uislamu sijui umekwenda je sikuelewi vizuri, lakini? Kwanza kutaja Ukristo na Uiaslamu kwene jukwaa hili umekatazwa, hapa tunaongea kiongozi bora,mtu mwenye utu na nia thabiti ya kumkomboa Mtanzania na umaskini, uonevu na ukiritimba. Kwa hiyo jipange vizuri, ndo uingie kwene jukwaa hili.Umesikia? Usiharibu jukwaa letu au kama hapakufai ingia kwene jukwaa lingine.
 
Mi naona huyu mwandishi tumsamehe bure, ataelewa taratibu mpango mzima wa unavyokwenda. Na hio hasira yake ya udini itaisha tu,manake siku inakuja na siku ipo.(Mwanakijiji ameshasema). Nahisi hajaisoma ile akiisoma sijui atasema ameandika nani.
 
Wewe unajieleza wazi bila kificho kuwa ni mdini. Mapendekezo yako na takwimu zako vinaadhihirisha wazi. Unaleta uchochezi ambao haufai kabisa. Kumbuka kuwa vijana wa leo hawako huko uliko ndo maana unaona hata ndoa za wakristo na waislam zinakuwepo.

Pia watu wa sasa hawazingatii sana hayo unayosema. Tangu uhuru hadi sasa hakujawa na mzozo mkubwa kati ya waislamu na wakristo. Watu wanaishi pamoja na kufanya kazi pamoja shule zinasomesha watoto bila ubaguzi wa dini wala rangi.

HAKUNA VITA VYA MSALABA TANZANIA KUNA VITA KATI YA WAILO NA MTIZAMO KIMAMBOLEO NA MTIZAMO WA KALE, WATU WANAOTAKA MABADILIKO YA DHATI NA WAHAFIDHINA YAANI WASIPENDA MABADILIKO.
 
bwana Dabomani kiasi fulani nakuunga mkono.. udini kwenye uchaguzi UPO, na kila kikundi kinavutia upande wake,..
 
Mwandishi anamsifia JK kwa kuwapeleka kina Mramba na Yona mahakamani halafu amewasafisha kwenye kampeni hiyo inaonesha ni usanii mtupu, ni yeye aliyetamka kuwa anawafahamu wezi wa bandarini, wakwepa kodi, wauza madawa lakini hajawashughulikia sasa hapo mafanikio yako wapi jamani. kwanini mnataka kuonyesha uwezo ambao hata yeye haamini kama anao. whyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyy
 
..mwaka huu mwezi mtukufu uliangua wakati wa kipindi cha kampeni za uchaguzi.

..sasa kuna wanasiasa wakawa wanatumia upenyo huo kufuturisha wananchi kwa minajili ya kuomba kura.

..hata kile kitendo cha Masheikh kumuita Raisi Kikwete kuwa mgeni rasmi ktk maulidi ya kitaifa kunaweza kutafsiriwa kama ni kumpigia chapuo kwa Waislamu.

..kuna viongozi wengi tu wastaafu kama, Salim Ahmed Salim, Dr.Salmin Amour, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, ambao wangeweza kuongoza shughuli ya Maulidi ya kitaifa.
 
Kiukweli nimepoteza muda mwingii kusoma then sipata chochote ndani ya hii threand yako mkuu inakuajeeeee...
 
Hili li-article lako hakuna atakayelisoma. Umeliandika ovyo sana. Weka aya, na maandishi makubwa zaidi kidogo.

Jamaniii mimi hapa nilisema watu humu siunajua makutano mi-artcle mingine ina bore!!japo inawezakuwa more useful lakini???watu na mastress ya kukimbiza sh.hawatasoma mwisho wasiku mtu anakimbilia kwenye comment kuona nini watu wamecomment ili apate angalau ka idea mimi nawahasa tafuta maneno yenye vifupisho!!lakini kama utatumia muda wako walikizo ukaandika li-artcle hilo!!!Mhnnnn:blah::A S 112::A S 13::hand:
 
Huyu jamaa mimi sijamuelewa lakini mimi ninaimani kwamba yeye ka copy and paste hivyo hakujishughulisha nakutaipu hange taipu hii thread!!!:blah:
 
Kwa mfano, pamoja na kwamba kule nchini Uingereza hali ya wafanyakazi wengi ilikuwa ni duni sana, jitihada za chama chao cha Labor kushika madaraka ya dola ili kuboresha hali zao za maisha zilikuwa zinakwamishwa na wafanyakazi wenyewe! Makada wa Labor walikuwa wakitukanwa, kubezwa na hata wakati mwingine kupigwa. Hali kwa makada wa Labor waliokuwa wanaendesha 'Operesheni Zinduka' hiyo iliendelea kuwa mbaya hadi mwaka 1914 pale kitabu cha hadithi cha mwandishi Robert Tressel, kinachoitwa 'The Ragged Trousered Philanthropists', yaani, 'Wasamaria wema waliovaa viraka', kwa tafsri isiyo rasmi, kilipochapishwa.
Kwa kifupi kitabu hiki kilikuwa kinawazungumzia wafanyakazi wa Uingereza ambao hali zao za kimaisha zilikuwa duni sana. Kilikuwa kinawaashangaa ni kiasi gani walikuwa HAWAJIONEI au KUWAONEA HURUMA WATOTO WAO kwa kuleta mabadiliko ya kisiasa, ukizingatia kuwa uwezo wa kufanya hivyo walikuwa nao kupitia kura zao.

Too long for a blog.
 
Udini utawaponza Watanzania. Nimekaa muda wa kutosha duniani. Nilichoona ni kuwa watu wanaweza kuwa wasomi wazuri na wenye hoja na usikivu ila linapokuja suala la dini usomi na usikivu huwekwa pembeni na jazba na ubinafsi vinatawala. Mi naamini wanaoleta udini katika siasa wana hukumu kubwa inawangojea kwa kuwa wanatetea dini zao na kuacha kutenda mema. Wako tayari kuzini huku wakijionesha mbele za watu kuwa wanatetea dini. Endeleeni tu, si mnadhani nchi ni yenu pekee Wakristo na Waislamu, endeleeni tu. You just go on. Endeleeni tu!
 
HAKUNA VITA VYA MSALABA TANZANIA KUNA VITA KATI YA WAILO NA MTIZAMO KIMAMBOLEO NA MTIZAMO WA KALE, WATU WANAOTAKA MABADILIKO YA DHATI NA WAHAFIDHINA YAANI WASIPENDA MABADILIKO.
na huu ndio ukweli wenyewe na haupingiki.
 
Rough za CCM zimeanza. Wanajaribu humu kupima maji, then next week mambo yako mtaani mbele kwa mbele. Kweli nimekubali "mtaji wa CCM ni ujinga wa wa-Tanzania!!!"
 
Back
Top Bottom