Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
IPTL Saga, Benjamin Mkapa
Richmond/Dowans saga, Jakaya Kikwete!
Ukirudi kumsoma Brian Cooksey, na varangati zima la IPTL, unabakia kushangaa na kuduwaa.
Nimeisoma ripoti ya Cooksey tena leo ikiwa ni mara ya 20 tangu ripoti hiyo itoke na kila siku inakuwa kama kuna kitu kipya kinafunuka!
Ni jinamizi gani lililowashika Viongozi na Watendaji wa Tanzania?
Ukijumuisha gharama halisi za tangu mwaka 1994 mpaka leo hii za mambo ya umeme, hii ikiwa ni mikataba na makampuni yote ya umeme (IPTL, Songas, Dowans, Artumas nk., halafu gharama za nchi kukosa Umeme tangu 1994 mppaka leo hii, utagundua kuwa Tanzania tumeshatumia karibu Dola Bilioni 2 za Kimarekani kuzungushana kuhusu suala la Umeme tangu 1994.
Fedha hizo zingetosha sana kutujengea Steiglers Gorge, kununua mitambo mikubwa na ya kuaminika na mengine mengi ambayo yasingetuleta hapa.
Sasa kila Shetani na Mbuyu wake, je tunakokwenda ni Ushetani gani na Mbuyu gani utatokea?
Richmond/Dowans saga, Jakaya Kikwete!
Ukirudi kumsoma Brian Cooksey, na varangati zima la IPTL, unabakia kushangaa na kuduwaa.
Nimeisoma ripoti ya Cooksey tena leo ikiwa ni mara ya 20 tangu ripoti hiyo itoke na kila siku inakuwa kama kuna kitu kipya kinafunuka!
Ni jinamizi gani lililowashika Viongozi na Watendaji wa Tanzania?
Ukijumuisha gharama halisi za tangu mwaka 1994 mpaka leo hii za mambo ya umeme, hii ikiwa ni mikataba na makampuni yote ya umeme (IPTL, Songas, Dowans, Artumas nk., halafu gharama za nchi kukosa Umeme tangu 1994 mppaka leo hii, utagundua kuwa Tanzania tumeshatumia karibu Dola Bilioni 2 za Kimarekani kuzungushana kuhusu suala la Umeme tangu 1994.
Fedha hizo zingetosha sana kutujengea Steiglers Gorge, kununua mitambo mikubwa na ya kuaminika na mengine mengi ambayo yasingetuleta hapa.
Sasa kila Shetani na Mbuyu wake, je tunakokwenda ni Ushetani gani na Mbuyu gani utatokea?