Ndio mimi Mfipa. Ila kupata hao watakaopenda bila masharti inakuwa ngumu, kama hawapo vile!
aah mbona rahisi tu kama wewe ni wa huko...chagua umpendaye then rudi waambie wazee wako..yani utamkuta nakusubiri home!
Aaah mdanganye tuu,ameshazoea huyo hata hapo umeshamdanganya kuwa unampenda kaamini,sasa ataacha kuamini hilo kabila lako la uongo,ataamini kuwa humpendi mara tuu utakapo mtosa,hivi hivi hawazi kushtukia!!Naombeni ushauri kutokana na tatizo linalonikumba ktk haya mambo ya kimahusiano. Ni muda mrefu nimekuwa nikikimbiwa na wapenzi, na hii hutokea kila ninapowatajia KABILA langu. Mpenzi wangu wa mwisho niliamua kumueleza nia yangu ya kwenda kujitambulisha kwao, lakini alikataa kwa sababu kuwa hawezi kuolewa na mimi, hata kwao watamshangaa kuolewa na mtu kutoka kabila linalosifika kwa uchawi(sina uhakika na hili) na uhusiano uliishia hapo. Kutokana na umri kuanza kunitupa mkono, nimekuja kwa staili ya kuoa na nimepata binti mmoja ambae bado hajapata details zangu. Kutokana na experience niliyopata kutoka kwa wapenzi wa zamani, nafikiria kumdanganya kuhusu kabila langu ili naye asije akanibwaga.
Naombeni ushauri nikaoe kijijini mtu wa kabila langu au niendelee na mpango wa kumdanganya huyu kuhusu kabila langu!
mmmh!! Wale wamekaa kisharishari.....enewei nitajaribu!
Mkuu GP, dada mmoja wa kabila langu niliwahi kumuapproach akakataa eti akadai mimi ni kaka yake(eti watu wa kabila moja ni ndugu).