mzee wa nguna
Senior Member
- Dec 5, 2012
- 132
- 113
Ndugu yangu wa karibu ameniomba nimsaidie ushauri,nami nimelileta hapa jamvini tusaidiane kumshauri...............''Jamani hebu nisaidieni mwenzenu. Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 31. Nina mpenzi ambae ninaishi nae na tumezaa mtoto mmoja,tatizo lake ni serial cheater,ukimkamata leo na huyu kesho kaishahamia kwa mwingine na haachi na mara nyingine mambo hadharani kama meseji za kupongezana jinsi gemu lilivyonoga n.k ni kawaida kukuta kwenye simu yake. Sasa tatizo ni kwamba nilikutana nae nikiwa na watoto wawili tayari bali baba zao tulishaachana kabisa hata mawasiliano nao sina na niliamua kuachana na mahusiano yote kabisa ndipo nikaanza mahusiano mapya na hatimaye kufuata taratibu za kimila na kuanza kuishi naye. Kila Nikithubutu hata kumuuliza hao anaotembea nao ni kina nani au kwa nini ananifanyia hivi ananigeuzia kibao mimi kwamba sina usafi wowote wa kumuuliza ningekuwa msafi nisingekuwa na watoto wawili kila mmoja na baba yake. Ukweli jambo hili linaniuma nashindwa la kufanya maana yeye ni mpekupeku akikuta hata nasalimiana na mtu anashuku vibaya na kutoa matishio kibao,nipo lonely vibaya maana namuogopa na ninajisikia kuteseka sana rohoni. Nifanyeje ili kumfanya walau aone anayofanya ni mabaya na kwamba mimi pamoja na historia iliyopo ni mtu mwema wala si entertain masuala ya kukosa uaminifu?? Kumuacha ni ngumu maana nachelea kutengeneza historia ya kutisha kwa jamii na kumnyima mwanangu mdogo haki ya kukua na baba yake.'' Haya,wale wenye neno hebu tupia hapa,lakini msilete mzaha