Mjadala kwa Wanaume: Kwa nini ndoa za mitala zinapigwa vita sana? kasoro yake nini? Tuoe bana kila mtu kwa uwezo wake

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,754
Ndugu zetu Islam na wazee wa Mila wameweza kudumisha ndoa za wenza wengi na kutokana na elimu waliyonayo ni jambo linalowezekana sana na linatibu jamii ambayo infidelity imekuwa order of the day.

Wakristo na Serikali wamejikita kwenye ndoa ya mme mmoja to mke mmoja ambapo ukiangalia ratio ya sensa unaona wazi kabisaa kuna wanawake wanaachwa pembeni kuishi bila ndoa. Jambo hilo hupelekea kuwepo na tatizo la uchepushaji wa mtiririko wa uaminifu wa ndoa.

Mimi nimekuta Babu yangu ambaye alibatizwa Ulutheri akiwa na wake wawili na wote wanatambulika kwenye kanisa hilo na amesalia bibi mmoja anaishi mpaka leo na huduma anapata. Yaani aliyesalia ni bibi mke mdogo. Tukivuta historia ya Baba wa Taifa hakuitwa mtoto haramu ingawa mama yake alikuwa mke wa tisa wa Chifu Burito.

Kipenzi cha Mungu, Mfalme Daudi alikuwa na ndoa zisizoeleweka kabisaa, na yule bwana aliyepewa na Mungu Hekima na Utajiri kuliko wanadamu wote yaani Mfalme Solomon alikuwa na ndoa yenye idadi ya wake pasua kichwa hadi kukinai.

Swali najiuliza; Hii LAZIMA ya mke mmoja ni kitu gani kinasababisha hayo? Hawa wanawake wanaohaha bila ndoa huku wakitamani ndoa wanaionaje pepo ya dunia? Tuchukulie kwamba idadi ya wanaume inapungua kwa kasi kubwa duniani. Je heka heka za kuchepuka zinasuluhishwaje kwa huu utamaduni wa kujifanya tu waaminifu wakati hatuna hata chembe ya kuvumilia ndoa ya mke mmoja?

Tujadili kwa kuelimishana
 
Acha tu ndugu, hapo ndo tulipigwa na kitu chenye ncha kali kichwani mke 1 haifai na hatoshi kabisa!

Ajabu ni pale baadhi ya vijana wa kiume nao wana-left kwenye group (papai) tunazidi kubaki wachache mbaya zaidi tunaambiwa tugawane haki ziwe sawa na wakati huo tanawahi kufa kuliko wao!

Suleman aliifaidi hii dunia kuliko kiumbe ye yote yule
 
Ndoa za mitalaa ikitokea Baba hakuacha misingi mizuri siku akifa au akiteteleka ni Rahisi sana familia kua na mpasuko mkubwa sana asa kama aliacha Mali ila Faida mojawapo ukoo ni Rahisi Sana kuwa mkubwa mfano kwa kipindi cha miaka ya Nyuma Bibi zetu walikua wanauzao mkubwa Sana kwahyo koo zilikua zinakua Sana ila kwa miaka hii sioni Faida ya polgamism zaidi zaidi ni kutafta kisukari tu kilipo wanawake wa kipindi wasaliti kwa kiwango kikubwa sana plus tamaa
 
Monogamy ipo kwenye agano jipya mbona,

Ni kwamba agano jipya liliandikwa kipindi waisraeli wapo chini ya utawala wa warumi, na warumi walikua na sheria ya mke mmoja

Vile vitabu vinne vya injili vimeandikwa na watu ambao hawakua hai kipindi cha yesu, walikua wanaongeza chumvi

Lakini Judaism, ambayo ndo dini ukristo ulipotokea, bado wanaoa wake wengi
 
Monogamy kama monogamy ni social construct, binadamu hawana asili hiyo, ililazimishwa tu

Kadri binadamu alivyozidi kuendelea na kuzaliana ilibidi kuwe na mfumo wa kusambaza rasilimali muhimu

Kwahiyo ilibidi kila me awe na ke mmoja, wajenge familia

Hapo inakua rahisi kutunza paternity(mtoto kuwa wako kihalali) na ke anapata ulinzi na rasilimali, vitu atakavyoshindwa kujipatia akiwa mjamzito na kulea

Na vile watoto wa binadamu ni atricial(wanazaliwa wakiwa hawajakamilika) mfumo huu unasaidia kuongeza survival rate ya binadamu

Nadharia ni nyingi ila hii ndo inaeleweka na hata hizo zingine zinabeba hii ndani....
 
Monogamy kama monogamy ni social construct, binadamu hawana asili hiyo, ililazimishwa tu

Kadri binadamu alivyozidi kuendelea na kuzaliana ilibidi kuwe na mfumo wa kusambaza rasilimali muhimu

Kwahiyo ilibidi kila me awe na ke mmoja, wajenge familia

Hapo inakua rahisi kutunza paternity(mtoto kuwa wako kihalali) na ke anapata ulinzi na rasilimali, vitu atakavyoshindwa kujipatia akiwa mjamzito na kulea

Na vile watoto wa binadamu ni atricial(wanazaliwa wakiwa hawajakamilika) mfumo huu unasaidia kuongeza survival rate ya binadamu

Nadharia ni nyingi ila hii ndo inaeleweka na hata hizo zingine zinabeba hii ndani....
Mimi ninadhani hizi theorem zimewekwa makusudi na mababa wa Nadharia ili kutukoga akili tusiweze kufurukuta nje ya utamaduni wao. Utamaduni wa Wagiriki ulirithiwa na Warumi na ukatawala dunia zama hizo na Warumi waliamua kujificha nyuma ya Ukristo ili waendelee kuitawala dunia kama ambavyo US na NATO wanavyojificha nyuma ya Demokrasia ili kuhakikisha ajenda za utamaduni wao zinafunika dunia nzima.

Afrika tuna la kujifunza kwenye hizi nadharia zinazotawala ulimwengu. Ingawa kitabu ya Ufunuo wa Yohana 22:18-19 anaelezea kufunga Neno la Mungu kwamba mtu asiongeze wala kupunguza maneno ya Unabii wa kitabu cha Mungu.... Lakini practically tunashuhudia walioasisi Biblia wakiipindua chini juu.

Nahisi labda hata eneo la ndoa limepindulia kufit hitaji lao
 
Mimi ninadhani hizi theorem zimewekwa makusudi na mababa wa Nadharia ili kutukoga akili tusiweze kufurukuta nje ya utamaduni wao. Utamaduni wa Wagiriki ulirithiwa na Warumi na ukatawala dunia zama hizo na Warumi waliamua kujificha nyuma ya Ukristo ili waendelee kuitawala dunia kama ambavyo US na NATO wanavyojificha nyuma ya Demokrasia ili kuhakikisha ajenda za utamaduni wao zinafunika dunia nzima.

Afrika tuna la kujifunza kwenye hizi nadharia zinazotawala ulimwengu. Ingawa kitabu ya Ufunuo wa Yohana 22:18-19 anaelezea kufunga Neno la Mungu kwamba mtu asiongeze wala kupunguza maneno ya Unabii wa kitabu cha Mungu.... Lakini practically tunashuhudia walioasisi Biblia wakiipindua chini juu.

Nahisi labda hata eneo la ndoa limepindulia kufit hitaji lao
Wao wenyewe wanafuata monogamy.

Monogamy imeshakua romanticized kwenye filamu na miziki, watoto wanalelewa hivyo, kila mtu anadhani kuna 'mwenzie' aliyeumbwa kwa ajili yake.

Hama dini tu, kubadili mfumo kutachukua muda sana.
 
Ngoja waje...

unnamed-1.jpg
unnamed.jpg


Cc: Mahondaw
 
Back
Top Bottom