mbutamaseko
JF-Expert Member
- Nov 20, 2018
- 736
- 1,054
Mfukuze tu uache kuishi kwa wasi wasi.Habarini za muda wakuuu.
Najikuta napata hamu ya kumdukua shemeji yenu sasa kila ninavyojaribu kumdukua sikuti mchepuko,sio mara mbili au tatu ni mara kibao nafanya hvyo lakini bado naona sms akichati na marafiki zake tu.
Sasa kuna maneno yanayosemwa kuwa mwanamke hawezi kaa asichepuke,sasa nahisi ananificha huyu mke wangu.ila nakosa ushahidi wapi nimkamatiee.
Sisemi kama namtafutia sababu hapana.lakini sasa yale maneno ya kuwa mwanamke lazima achepuke yameniathiri sana.
Kila nikidukua najikuta natamani nidukue na mengine lakini sikuti kitu nipeni mbinu wakuu..
Nimchunguze vipi haswa haswa ili nijue ukweli.
Mana KUNA PICHA MOJA NILIIONA KWAKE AMEMTUMIA MWANAUME KWENYE WATSAP HUKU ILE PICHA YA KAWA IMEANDIKWA "KILICHOMO NI CHAKO,ONDOA HOFU"
sasa hyo picha kila nikienda watsap kwake kuIchunguza yani nione kama walifanya kuchati naona ile picha imefika lakini sasa jamaa hajibu,kila siku namdukua kuangalia ile namba kama wanawasiliana naoba eboo tu.
Hata katika sms za kawaida sioni kama wanachati aisee.
Sasa najiuliza ilikuwaje akaandika au akamtumia mtu picha ile yenye maneno ya ukakasi tena mwanaume??
Inawezekana akamtumia tu bila kuwa na mahusiano nae pjcha kam hyo wakuuw?