Ticha
Senior Member
- Aug 26, 2007
- 135
- 8
Wanachuo wote wa Diploma ya Ualimu wanatarajia kuanza mitihani yao ya mwisho jumatatu hii.Tunawatakia kila la kheri wote waweze kufauru vizuri ili waweze kuajiriwa. Tukumbuke wanachuo hawa wote wamesoma mwaka mmoja chuoni na mwaka wa pili wamefanya mafunzo hayo ya kufundisha kwa miezi sita, kwa hiyo mwaka mmoja chuoni na mwaka wa pili kazini.Baada ya hapo wamerudi chuoni kufanya mtihani wao wa mwisho na atakayefeli hatapata ajira ya serikali. Lakini ikumbukwe wamekaa nje ya chuo mwaka mzima ndipo wanakuja kufanya mtihani huo,sijui kama walikuwa wanasoma huko majumbani na pia wafundishe. Lakini mfumo huo umefutwa baada ya kuona haureti mafanikio kabisa,inaonekani Wizara ilirudisha mtindo wake maarufu kama VODA FASTER. Kwa hiyo mwaka huu wanasoma miaka miwili yote darasani.