Kikwete 'awapakazia' viongozi wa dini biashara ya madawa ya kulevya

haya majibu ya kijinga awapelee watoto wa chekechea

Tulitaka rais atusaidie kutaja ili tuwaondoe kwenye huduma ya kanisa wahusika in case sheria ichukue mkondo wake.

Tabia ya Maaskofu kumwalika JK ikome manake ni hawa maaskofu wanaoonesha kujipendekeza kwake.
Maaskofu wawaalike viongozi wanaotumia akili na sio matumbo kufikiria
 
Na haya ndio majibu ya Rais Jakaya Kikwete kwa viongozi wa dini waliompa saa 48 kuwataja viongozi wa dini wanaojihusisha kwa biashara haramu ya dawa za kulevya. Soma, tafakari kisha chukua hatua.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Taarifa za Maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kumpa Rais Jakaya Mrisho Kikwete saa 48 kuwataja kwa majina viongozi wa dini wanaotuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya, ni kauli ya kusikitisha na ambayo haikutegemewa kutoka kwa viongozi hao wa dini.

Viongozi wa dini ni watu wa kutumainiwa sana katika jamii yeyote, lakini ikizingatiwa kuwa wao sio malaika ama watakatifu hapa duniani, kwani nao wanatumbukia katika majaribu na kujikuta katika vitendo au hali isiyo tegemewa kabisa.

Katika Hotuba yake kwenye sikukuu ya kuwekwa wakfu na kusimikwa Mhashamu Askofu John Ndimbo kuwa Askofu wa Jimbo la Mbinga, Rais Kikwete alitoa ombi ambalo si geni kwani alishalitoa katika hafla zingine pia zilizohusisha viongozi wa dini.

Katika sherehe hiyo Rais alitoa ombi la kuwataka viongozi wa dini wajihusishe kwa ukamilifu katika mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya.

Rais Alisema, "Ni tatizo linalozidi kukua pamoja na jitihada za Serikali kupitia vyombo vya usalama kuwabana, kuwawajibisha watumiaji na wafanyabiashara ya dawa za kulevya. Athari zake kwa jamii zinaeleweka hivyo haihitaji kuzirudia" Rais alieleza, "Hata hivyo niruhusuni niseme tu kwamba tusipofanikiwa kulidhibiti tatizo hili, hasara yake ni kubwa mno. Watoto wetu wengi wataharibika, uhalifu, hasa wa wizi na mauaji utaongezeka. Taifa litaharibikiwa." Amesema Rais na kuendelea kueleza kuwa,

"Siku hizi kila siku kuna watu wanaokamatwa kwa kujihusisha na dawa za kulevya. Inaashiria kuimarika kwa vyombo vyetu vya usalama, Lakini inasikitisha sana kuona kuwa biashara hiyo sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu. Huku sasa tunakoelekea kwa kweli ni kubaya sana. Nawaomba mtoe uzito unaostahili kwa tatizo hili. Viongozi wa dini mnasikilizwa, Nawaomba kemeeni, onyeni na elimisheni jamii juu ya madhara ya dawa za kulevya, waelimisheni vijana ambao ndiyo walengwa wakuu, waepuke na waache kujihusisha na biashara na matumizi ya dawa za kulevya". Rais alisema.

Kwa maneno haya, tunategemea viongozi wa dini kuchukua onyo hili la Rais kama ishara (Clue) na kuanza kuifanyia kazi.

Mtu akikuonya kuwa nyumbani kwako kumeonekana nyoka, huanzi kwa kuuliza kama kweli, ni wa rangi gani? Unatakiwa kushtuka na kuweka na kujiandaa kumsaka kwa nia ya kumuondosha nyumbani kwako hata ikibidi umuue ili asije akaleta madhara makubwa kwako na kwa familia yako. Rais ana nia njema sana katika kulielezea jambo hili na mwenye nia njema haumbuki.

Hivi karibuni wapo viongozi wa dini wamekamatwa kwa rushwa, ngono na kutuhumiwa kujihusisha na vitendo mbalimbali ambavyo ni kinyume na maadili yasiyo tegemewa na jamii kwa ujumla, wapo ambao wameshakamatwa na watafikishwa kwenye vyombo vya sheria, wapo wanaochunguzwa, tumeshawashuhudia na bado wataendelea kushuhudiwa. Hili si jambo dogo la kujitetea kwa kauli nyepesi kutoka kwa watu wanaotegemewa na jamii kwa kumpa Rais saa 48.

Anaejishuku ajisalimishe mwenyewe, anaeshukiwa na jamii afichuliwe ili afanyiwe uchunguzi na hatimaye sheria ichukue mkondo wake lakini msisubiri Rais awataje hadharani ndiyo muanze kuchukua hatua.

Mnategemewa muweke mikakati na vipaumbele vya kufanyia kazi changamoto hiyo, na sio kuaihirisha tatizo hili ambalo linazidi kuwa kubwa. Kazi hii ya kupambana na madawa ya kulevya haimhusu Rais peke yake inamhusu kila Mtanzania, popote alipo katika nafasi yake na viongozi wa dini wananafasi kubwa sana kwa sababu wao wanasikilizwa, wanatoa ushauri na wanategemewa kuwa na maelekezo yanayompendeza Mungu.

Mwisho.

Imetolewa na:

Premi Kibanga
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi
Ikulu,
Dar-Es-Salaam.

07 Juni, 2011

Well done Premi ! mie mwenyewe nilishangazwa kuona Mokiwa anataka watajwe , hili si jukumu la Rais kuna vyombo vya usalama ndio kazi zao hizo. Na wengine wameisha kamatwa pia, je Mokiwa hawajui ?. mie hapo ndipo ninapooona uwezo wa viongozi wa dini kufikiri siku hizi unaathiriwa na matashi yao ya kisiasa. Na Mokiwa anajulikana ni mfuasi mkubwa wa Chama Cha Demokaya na Magwanda
 
Alisema kuwa viongozi hao wa dini baadhi yao wamekuwa wakishiriki katika kufanya biashara ya madawa ya kulevya kwa kuwafanyia mipango vijana kuwatafutia hati za kusafiria kwenda nchi za nje kufanya biashara hiyo. source gazeti mwananchi la tarehe 7/6

nakubaliana na mchangia mada hapo juu, kwani anaonekana kuwa na uwezo mkubwa sana wa kuchambua mambo, ukweli ni kwamba, suala hili tusijetuka lipotosha mbele ya umma, kwani Rais alichokisema si kuwa baadhi ya maaskofu au baadhi ya mashekhe bali baadhi ya watumishi wa Mungu. hata hivyo si vibaya kwetu sisi kuona si jambo jema sana kwa mtu kama Rais kutoa tamko la ujumla kiasi kile "a such generic statement", inaonekana naye ni sehemu tu ya watu wengi wanao lalamika ili watu wengine waweze kujibu hayo wanayo yaona kuwa hawatendewi haki. kwa Rais hili si sawa kabisa, yeye ana uwezo mkubwa wa ku-identify wale wahusika na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria na si-kulalamika kama mwanchi wa kawaida tu.......hii inaonesha udhaifu wa hali ya juu ya utendaji wake kwa ujumla.

watu wanahitaji utekelezaji wa sheria bila kuonea watu wa tabaka lolote na si kuwa sawasawa na watu wa vijiweni ambao hukaa na kuzungumza mambo bila kuya fanyia utafiti yakinifu.
 
majib hayaridhishi, tunasubiri atutajie majina ya hao watumishi, hatutaki bla bla hapa! Kama ana majina ayataje ili arahisishe kazi ya kuwakamata.
 
Yaani Rais wetu kila siku ni mtu wa kujiteteaaa tuuuuuuuuuuu!!!!! na kauli zake zenye utata!!!! MPAKA AIBU KWA KWELI...........
 
mi napata mashaka na utashi wa wasaidizi wa rais!
Msaidizi mahususi wa Raisi hawezi kusema anayejishuku ajisalimishe....naona kama vile ni kama mipasho flani hivi niliyowahi kusikia kwenye taarabu na akina mama wa mtaani wakisema kama limekukugusa/ukijishuku basi ni wewe!! Nadhani mimi wametumia style hii toka Kwa Hadija Kopa kwani si Mwana CCM pia??
 
Lakini, inasikitisha sana kuona kuwa biashara hiyo sasa inawavutia hata baadhi ya watumishi wa Mungu. Huku sasa tunakoelekea kwa kweli ni kubaya sana. Nawaomba mtoe uzito unaOstahili kwa tatizo hili.

Kwenye red ina maana ni pamoja na maaskofu

Si vema kutufanya wengine hatuchambui mambo, Hebu chukua tena muda wako usome hii ili angalau uone umejikwaa wapi katika uchambuzi wako;

haya karibu;
Rais Jakaya Kikwete, ametangaza kuwa ataunda chombo maalum cha kupambana na ongezeko kubwa la tatizo kubwa la biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini.

Aidha, Rais Kikwete amewaomba viongozi wa dini na taasisi za dini nchini kusaidiana na Serikali katika kupambana na tatizo hilo lenye madhara makubwa kwa jamii, na hasa miongoni mwa vijana ambao wanaunda asilimia 60 hadi 80 ya Watanzania wanaotumia dawa za kulevya ambazo zinaharibu mwili na akili ya mtumiaji.


Vile vile, Rais amesema kuwa wakati ni kweli kuwa mikoa yote ya Tanzania inakabiliwa na tatizo hilo, lakini ni mikoa saba inayoongoza kwa kuwa na tatizo kubwa zaidi ikiwa ni Dar es Salaam, Mwanza, Mjini Magharibi – Zanzibar, Arusha, Tanga, Mbeya na Dodoma.

Rais Kikwete alitangaza kusudio lake la kuunda chombo maalum cha kupambana na dawa za kulevya jana wakati wa sherehe za kusimikwa kwa Askofu Mteule Albert Jella Randa wa Kanisa la Mennonite, Tanzania, kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mwanza ambako alikuwa mgeni.


Sherehe hizo zilifanyika kwenye makao ya Dayosisi hiyo Nyakato, mjini Mwanza.


Akihutubia mamia ya waumini wa Kanisa hilo pamoja na wananchi wengine waliohudhuria sherehe hizo, Rais Kikwete amewaomba viongozi wa dini, madhehebu ya dini mbali mbali nchini kuongeza juhudi za kupambana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya.


Akisema kuwa pamoja na kwamba matunda ya juhudi za Serikali katika kupambana na tatizo hilo yameanza kuonekana bado kazi iliyoko mbele ya jamii ya Tanzania ni "kubwa sana".


"Mwaka jana, 2010, watu 12,119 walikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya. Katika kipindi hicho, dawa za kulevya zilizokamatwa ni heroine kilo 190 na gramu 780, cocaine kilo 65, morphine kilo 11, bangi kilo 279,520 na mirungi kilo 10,317. Takwimu zinaonyesha kuwa mkoani Mwanza tatizo linakua kwa kasi sana," amesema Rais Kikwete na kuongeza:


"Dawa za kulevya zina madhara makubwa kwa watumiaji na kwa jamii. Kwa watumiaji hatima yake ni mtu kuharibikiwa kimwili na kiakili. Watu huwa mazezeta na hivyo kushindwa kutokuwa na manufaa kwa jamii. Hii ni hasara kwa familia, jamii na taifa. Bahati mbaya sana waathirika wengi ni vijana. Tafiti zilizopo zinaonyesha kwamba asilimia 60-80 ya watu wanaotumia dawa hizo ni vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 30, alisema."


Aliongeza: "Hii ni hasara kubwa kwani vijana ndio nguvukazi ya leo na kesho. Ndiyo roho ya taifa na warithi wa familia, jamii na taifa. Wakiharibikiwa taifa letu litaangamia. Tusikubali. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kulichukia tatizo hili na kulikemea kwa nguvu zake zote ili kuokoa taifa letu. Nawaomba viongozi wa dini kushirikiana na Serikali na watu wote wenye mapenzi wa nchi yetu kupambana mpaka tufanikiwe kudhibiti na hatimaye kulitokomeza tatizo hili."


Sherehe za leo za kusimikwa Askofu Randa (50) kuwa Askofu wa Kanisa Mennonite, Jimbo la Mwanza, pia zilihudhuriwa na mamia kwa mamia ya waumini wa Kanisa hilo na wananchi wengine.


Kwenye sherehe hizo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Mennonite Tanzania (KMT), Mhashamu Severin Watson Mang'ana amemkabidhi askofu huyo mpya nguvu kuu ishara za mamlaka na madaraka ya uaskofu ikiwamo Biblia, Katiba ya KMT, Cheti cha Uaskofu na vitabu vya taratibu ya kuendesha ibada za Kanisa hilo na nyimbo.

Kanisa la Mennonite lililoanzishwa duniani mwaka 525 na Mchungaji Menno Simon mjini Zurich, Uswisi, liliingia nchini miaka 77 iliyopita mwaka 1934 na liko katika maeneo yote ya Tanzania isipokuwa Zanzibar, Ruvuma na Pwani. Kanisa hilo lina makao yake mkoani Mara.

Source: Maganga One.: VIONGOZI WA DINI NA TAASISI SAIDIENI SERIKALI KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA - JAKAYA KIKWETE
 
Yap huyu mtetezi kanunuliwa hawa watu cjui kwa nn? wanakuwa wajinga kiasi hiki,ACHA YAMDODEDEE TU! anauzi sana tuige nchi za wenzetu kwanza kwa cheo cha JK mwenyewe kingekuwa mashakani pia kama wapo Rais kwa nn? awe anaumauma maneno.AIBUUUUUUUUUUUU! :majani7:TUPO PEMBENI TUNAKULA JARAMBA!
 
Acha kujipendekeza kwa maskofu kikwete,mbona kwenye mabalaza ya IDDY na maulidi hatumuoni ila kusimikwa kwa maskofu hakosekani,mwache wamwite muongo mana hana cha kuwafanya,amekalia kutudanganya waislamu,tumemshtukia hana msaada wowote
 
Jamani ukiona Rais ametamka hivyo, huwezi kujua makubwa yaliyopo nyuma. Huenda anawajua wanaojihusisha lakini hakuna ushahidi wa kuwashtaki mahakamani. Ni sawa na hizi kesi zingine za ufisadi. Wapo wanaoshutumiwa lakini hawajachukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa hakuna ushahidi wa kutosha. Hilo liwe onyo kwa watumishi wa Mungu wanaotumia utumishi wao kupitisha madawa ya kulevya. Nina uhakika vyombo vinavyohusika vikiwa na ushahidi wa kutosha wanaohusika watashtakiwa.
 
Msaidizi mahususi wa Raisi hawezi kusema anayejishuku ajisalimishe....naona kama vile ni kama mipasho flani hivi niliyowahi kusikia kwenye taarabu na akina mama wa mtaani wakisema kama limekukugusa/ukijishuku basi ni wewe!! Nadhani mimi wametumia style hii toka Kwa Hadija Kopa kwani si Mwana CCM pia??

ndo maama nasema Kikwete kazungukwa na watetezi wajinga ! Wasiojua thamani ya Ikulu na hadhi ya matamko ya Ikulu.
 
Back
Top Bottom