Kikwete atunukiwa tuzo ya demokrasia Afrika

Ikulu ya Dar es salaam imetangaza kuwa Rais Kikwete ametunukiwa tuzo ya kimataifa ya Gwiji wa demokrasia barani Afrika kwa mwaka 2014.

Ikulu imepokea tuzo hiyo iliyotolewa na Jarida la The Voice na iliwahi kutolewa pia kwa Rais mstaafu wa Zambia Kenneth Kaunda.

=========

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Rais Kikwete atunukiwa Tuzo jingine la kimataifa


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa mara nyingine ametunukiwa tuzo la kimataifa – zamu hii kwa kuwa mshindi waTuzo la Nyota wa Demokrasia Afrika 2014 – Icon of Democracy Award Winner for 2014 in Africa.

Kwa mujibu wa barua aliyoandikiwa Rais Kikwete na kupokelewa Ikulu, Dar Es Salaam, Rais Kikwete amekuwa mshindi wa kwanza, na kwa mbali kabisa, katika mchuano na marais watatu wa Afrika ambao walifikia mwisho mwa mchuano wa kuwania tuzo hilo.

Katika barua hiyo, Mchapishaji na Mhariri Mkuu wa Jarida hilo, Pastor Elvis Iruh, akizungumza kwa niaba ya Kamati ya Tuzo 2014, amesema kuwa uongozi wa Rais Kikwete umekuwa ni hadithi ya kusifiwa ya mafanikio katika Bara ambako hadithi za namna hiyo siyo nyingi.

Tuzo hilo hutolewa na Jarida la The Voice na mwaka jana mshindi alikuwa ni Rais Bai Koroma wa Sierra Leone ambaye alikuwa ni mshindi wa pili wa Tuzo hiyo ambalo ilitolewa kwa mara ya kwanza kwa Rais wa Kwanza wa Zambia, Mzee Kenneth Kaunda.

Sherehe maalum ya kukabidhi tuzo hiyo imepangwa kufanyika Oktoba 17, mwaka huu, 2014, katika Hoteli ya Van der Valk, iliyoko Almere, Uholanzi.

Miongoni mwa sifa nyingine, Rais Kikwete anatunukiwa Tuzo hiyo kwa sababu ya kuwa msimamizi mzuri na wa kweli wa demokrasia, kuendelea kuhakikisha kuwa amani, utulivu na maendeleo vinaendelea kupatikana katika eneo la Afrika ambalo limepitia vipindi vingi vya migogoro na matatizo.

Aidha, gazeti hilo linasema kuwa Rais Kikwete amekuwa kiongozi wa mfano, kimataifa na kikanda, na linatoa mfano wa mchango wake katika kusuluhisha mgogoro mkubwa wa kisiasa nchini Kenya kufuatia uchaguzi mkuu wa 2007.

Rais Kikwete pia anasifiwa kwa mchango wake katika kusimamia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbali mbali – kilimo, elimu, miundombinu, maendeleo ya viwanda, utalii na pia mchango wake katika kuendeleza vijana na kutoa nafasi nyingi kwa akinamama kushika nafasi nyingi za uongozi.

Jarida la The Voice pia limempongeza Rais Kikwete kwa kuimarisha Umoja na Muungano wa Tanzania na kutoa nafasi kwa wananchi kujadili na kukubaliana kuhusu Katiba Mpya ya Tanzania.

Aprili mwaka huu, Rais Kikwete alitunukiwa tuzo la kuwa kiongozi mwenye mchango mkubwa zaidi katika maendeleo ya Afrika kwa mwaka 2013 – The Most Impactful Leader in Africa 2013.


Imetolewa na:


Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
30 Julai, 2014

Hawa watu wa Ulaya wanatudharau sana?? au wana agenda wanayoisukuma nyuma ya pazia??
Hawa wa Ulaya walikuja wakatufundisha democracy na utawala wa sheria, sijui yaliyotokea kwa Mwangosi, Mabomu mikutano ya wapinzani, kuwabambika wapinzani kesi na kusweka ndani ndio utawala wa sheria na democracy??

Huu ni muuendelezo wa dhihaka na dharau za Wamagharibi dhidi yetu. Wanataka kutuaminisha kuwa wao wanaweza kuchukua maji alafu wakaweka kwenye dumu (jerycan) alafu wakatuambia haya ni mafuta tena petrol safi kabisa na sisi tukaamini.

Nafikri kuna haja ya kuwepo na chombo cha kutathimi hizi awards (Tuzo) kabla ya viongozi wetu kuzipokea ili kujua kama ni sahihi au dharau ilojificha???
 
Bawacha hata mkimuna vipi ndiyo basi tena jk anasonga mbele tu kathubutu,kaweza na sasa anasonga mbele twende jk wetu na tanzania yetu.
...maskini bagamoyo na kigamboni tunaexchange kwa recognition tu,kweli kal peters treaty bado zipo mpaka leo...
 
yeye anazipenda na kuzifurahia kweli. kwani hamwoni yeye na wapambe wake wanavyokomaa na kumwita 'dk. kikwete' wakati msingi wake ni usanii tu kama wa hizi tuzo zisizojulikana. siku si nyingi mkewe naye atatunikiwa doctorate ya heshima kwa kuwa tu ni mke wa 'dk. kikwete'.
 
Sifa zenyewe wanaotoa ni wazungu!!! Kama si kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa ni nini?!
 
Mkuu usihangaishwe na
hao wazungu,vigezo wanavyo vitumia nijinsi unavyokua laini kwa wazungu,
wakati wote ukiwapa wanachotaka lazima wakupambe tu,hakuna kigezo
kingine.

acha unafki hiyo tuzo angepewa baba yako kagame ungetamka maneno hayo.?
 
Nikweli,nakumbuka kiomgozi mmoja afrika alisema wakati wote ukifanya mambo kwa masilahi ya wananchi utaitwa dickteta lakini ukiyafanya kwa masilahi ya wazungu utaitwa mwanademokrasia.

Umeona eh!Halafu tunadhani hawa watu weupe ni wajomba zetu.
 
Hii ni ile Kama kawa ya mizaha ya Wazungu!

Kwamba Kiwete amepewa Tuzo ya Nyota wa Demokrasia Afrika. Huu ni mzaha au kebehi kwa Watanzania. Sielewi hawa Gazeti la The Voice wametumia Vigezo gani mpaka kumpa ushindi huu!!

Nafikiri ni watu waliokaa mezani huko Uholanzi na kuamua kumpa ushindi kwa maslahi wanayojua wao. Maana kiuhalisia ni kitu gani cha mno kuhusu DEMOKRASIA alichofanya huyu Kiwete???Rais ambaye ameshindwa kuvumilia MAONI YA WATANZANIA waliotaka Serikali TATU katika Tume ya Jaji Warioba na yeye kusema ANATAKA SERIKALI 2 huku akiwatishia Watanzania kuwa iwapo Katiba ya Serikali TATU itapitishwa Jeshi litachukua nchi????

Hawa jamaa wa The Voice lazima watakuwa na sababu zao zingine. Juzi jui tu hapa Gazeti la The Daily Mail lilimshambulia Rais Kikwete kuwa ameshindwa kuzuia mauaji ya Wanyama kutokana na Ujangili!!!!! Leo The Voice wanatuambia hakuna Rais mwenye kusimamia Demokrasia kama Kikwete?????Huu ni usanii ulio wazi kabisa.

Inawezekanaje Rais ambaye ameshindwa kusimamia Mchakato wa Kupata Katiba Mpya kwa ajili ya Watanzania kulingana na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mpya leo ndiye anatajwa kinara wa DEMOKRASIA Afrika???

Ifikie Watanzania tujitambue na tukatae hii mizaha na usanii wa Wazungu! Hii inawezekana kabisa hawa waliompa Ushindi huu wanalenga Raslimali zetu. Hivi huyu Kiwete atakapoenda huko Uholanzi kupewa hiyo zawadi feki na baada ya hapo haohao Waholanzi wakamwingia na gia ya kuja kuwekeza kwenye Madini, Gasi, Mbuga za Wanyama au Kujenga miundo mbinu kwa mikataba ya kifisadi, atakuwa na ubavu wa kuwakatalia?? Jibu ni big NO!!!!

Kilichotakiwa hapa ni Watanzania kupinga kwa nguvu zote uteuzi huu kwa maandamano na kutumia media kuonyesha kuwa hatukubaliani na huu usanii wa kumpa Rais Kiwete ushindi wa nyota wa Demorasia Afrika. Mimi ningekubaliana na hawa Waholanzi kama Katiba Mpya ya Tanzania ingelikuwa tayari imekamilika April,2014 kama Kiwete alivyokuwa amewaahidi Watanzania. Lakini kwa sasa huu ni uongo,unafiki na udhallilishaji kwa Watanzania wote.

Tufikie mahali tukatae upuuzi huu.
 
Tuzo inatolewa na gazeti serikali inaitangaza????? mungu ibariki tanzania!!!
 
Hii ni ile Kama kawa ya mizaha ya Wazungu!

Kwamba Kiwete amepewa Tuzo ya Nyota wa Demokrasia Afrika. Huu ni mzaha au kebehi kwa Watanzania. Sielewi hawa Gazeti la The Voice wametumia Vigezo gani mpaka kumpa ushindi huu!!

Nafikiri ni watu waliokaa mezani huko Uholanzi na kuamua kumpa ushindi kwa maslahi wanayojua wao. Maana kiuhalisia ni kitu gani cha mno kuhusu DEMOKRASIA alichofanya huyu Kiwete???Rais ambaye ameshindwa kuvumilia MAONI YA WATANZANIA waliotaka Serikali TATU katika Tume ya Jaji Warioba na yeye kusema ANATAKA SERIKALI 2 huku akiwatishia Watanzania kuwa iwapo Katiba ya Serikali TATU itapitishwa Jeshi litachukua nchi????

Hawa jamaa wa The Voice lazima watakuwa na sababu zao zingine. Juzi jui tu hapa Gazeti la The Daily Mail lilimshambulia Rais Kikwete kuwa ameshindwa kuzuia mauaji ya Wanyama kutokana na Ujangili!!!!! Leo The Voice wanatuambia hakuna Rais mwenye kusimamia Demokrasia kama Kikwete?????Huu ni usanii ulio wazi kabisa.

Inawezekanaje Rais ambaye ameshindwa kusimamia Mchakato wa Kupata Katiba Mpya kwa ajili ya Watanzania kulingana na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mpya leo ndiye anatajwa kinara wa DEMOKRASIA Afrika???

Ifikie Watanzania tujitambue na tukatae hii mizaha na usanii wa Wazungu! Hii inawezekana kabisa hawa waliompa Ushindi huu wanalenga Raslimali zetu. Hivi huyu Kiwete atakapoenda huko Uholanzi kupewa hiyo zawadi feki na baada ya hapo haohao Waholanzi wakamwingia na gia ya kuja kuwekeza kwenye Madini, Gasi, Mbuga za Wanyama au Kujenga miundo mbinu kwa mikataba ya kifisadi, atakuwa na ubavu wa kuwakatalia?? Jibu ni big NO!!!!

Kilichotakiwa hapa ni Watanzania kupinga kwa nguvu zote uteuzi huu kwa maandamano na kutumia media kuonyesha kuwa hatukubaliani na huu usanii wa kumpa Rais Kiwete ushindi wa nyota wa Demorasia Afrika. Mimi ningekubaliana na hawa Waholanzi kama Katiba Mpya ya Tanzania ingelikuwa tayari imekamilika April,2014 kama Kiwete alivyokuwa amewaahidi Watanzania. Lakini kwa sasa huu ni uongo,unafiki na udhallilishaji kwa Watanzania wote.

Tufikie mahali tukatae upuuzi huu.

kaka usitumie nguvu nyingi hicho kigazeti ni nani hadi roho ikutoke? upuuz mtupu eti tuzo ya gazeti na serikali inatangaza?
 
wacha roho mbaya...unakua kama mtutsi? au huoni anayofanya jk tukakupime miwani!



Labda nina matatizo ya macho....kuna nini cha maana alichofanya Kikwete toka aingie madarakani? Ile ahadi ahadi ya ari mpya na nguvu mpya, maisha bora kwa kila mtanzania aliitimiza?
 
Wazungu ni wazuri kwa satire/sarcasm/irony. Kwakuwa jamaa yetu M.k.w.e.r.e na jamaa zake ikulu wako slow ku-decern subtle messages kama hizi toka kwa Wazungu basi wataendelea kuchezewa sana na kufanywa vituko vya ulimwengu.
 
Ni sawa kabisa unachoongea ila ujue kua hakuna kiongozi anayeweza kusimama peke yake.ubaya ni kwamba anaangushwa na viongozi wenzake ambao ndio waliompa hicho kiti cha uraisi.hebu jaribu kukazia mambo mazuri aliofanya halafu tuone
 
Back
Top Bottom