Kyawanjubu
JF-Expert Member
- May 13, 2017
- 2,437
- 2,158
we nae umezidi kama season za kihindi dk 5 unasubiri muendelezo wiki iyayoTUENDELEE,
BALAA LA KWANZA
katika mwambao wa Hilo ziwa hapa kijijini ikola Kuna bandari ndogo ambayo inapokea maboti yalioundwa kwa mbao kwaiyo yakifika hapa ikola yanapakia mizigo ya mazao yanapeleka Congo...Sasa kumbe Hawa watu wanaomiliki haya maboti wanarogana hakuna mfano..boti lako likionekana linafanya kazi Sana linazamishwa kichawi ziwani na upepo maarufu uitwao lukuga.
Sasa Kuna mwamba alipewa laki mbili akachote maji kwenye boti la mfanyabiashara mmoja ili hayo maji yapelekwe kwa mganga...mwamba akachukua dili Hilo huyooo mpaka kwenye boti akachota maji na kuyapeleka kwa aliemuagiza.
Basi baada ya siku mbili yule mwamba alietumwa kuchota maji kwenye boti akaanza kuota kidonda mkononi...baada ya wiki Hali ikawa mbaya...Kijiji hakina huduma ya afya zaidi ya maduka ya dawa tu...ikabidi apelekwe kwa mnganga kufika huko ikaonekana jamaa amerogwa kwa kuchota maji botini...ametibiwa na mnganga ikashindikana Hali yake ikazidi kuwa mbaya..ikabidi ndugu wamtafute mmiliki wa boti wamueze Hali halisi.
Mwenye boti akawaambia kuwa boti lake amelizindika kwa waganga zaidi ya ishirini kutoka kongo...kwaiyo hajui ni dawa za mnganga yupi zimempata ndugu yao..baada ya siku tatu mbele mgonjwa akakata Moto... ITAENDELEA