TUKANA UONE
JF-Expert Member
- Jan 3, 2018
- 1,816
- 5,151
Ukihitaji salamu suburi kwanza nilewe, tofauti na hapo utaambulia chuya!
Kiranga ana asilimia kubwa kuurithi uzima wa milele kuliko watu wengi wanafiki!.
Narudia tena "Kiranga anazo asilimia kubwa za kuurithi uzima wa milele kuliko wanafiki walio wengi"
Kiranga ni nani?
Huyu ni jamaa ambaye JF expert ambaye haamini uwepo wa Mungu kabisa.
Mimi kama Mkristo ninaye muamini Mungu,huwa sichukizwi wala sikerwi na ambacho anakiamini Kiranga
Watu wengi wanaojiita Wakristo kwa Waisilamu huwa wanafanya maigizo ya kuishi namna ya mafundisho ya dini zao zinavyotaka,watu wengi wamekuwa washupavu wa hizi dini huku wakimuona Kiranga na wenzie wasioamini uwepo wa Mungu kama walio na dhambi kupitiliza kuliko wao.
Hata wewe kabla hujamjua Mungu yawezekana ulikuwa kama Kiranga na ndugu zake,kibaya zaidi umemjua Mungu lakini bado Kiranga ana unafuu kuliko wewe!.
Kwanini?
1. Kuna mwanamke/mwanaume anayemuamini Mungu lakini kwenye biashara zake pale Kariakoo, Tandika, Mbezi, Buguruni bado anatumia Ushirikina akimini itavuta wateja wengi! Huyu mtu utamkuta kila Ijumaa, jumapili au Jumamosi anaenda kumuabudu Mungu tena anakuwa wakwanza kutiririsha machozi wakati wa maombi lakini akitoka hapo anaendelea na ushirikina wake lakini huyo Mungu wake anayemfanya alie wakati wa maombi anamuweka mfukoni!.
Kiranga atakuwa na unafuu sana kama atafanya biashara akatumia ushirikina kwasababu aamini uwepo wa Mungu kuliko wewe unayejiita Mkristo na unaendelea kutumia Ushirikina.
2. Endelea kufanya Ngono,Uzinzi na Uasherati sana wakati huo huo unajiita Muisilamu au Mkristo na wakati ukielewa kabisa Mungu amekataa!.
Kiranga atakuwa na unafuu sana kufanya uzinzi na uasherati kwasababu aamini uwepo wa Mungu aliyekataza mambo hayo kuliko wewe unayejifanya kumjua huyo Mungu na bado unaendelea kufanya!.
3. Endeleza Uongo,majungu na Usengenyaji kwa sana huku ukiwa na matumaini ya kuirithi pepo au uzima wa milele kutoka kwenye mbingu ya huyo Mungu wako kuliko
Kiranga akiwa muongo, msengenyaji na mfitinishi hiyo ni haki yake kwasababu haamini uwepo wa Mungu wenu ambaye amaekaza hayo mambo kuliko wewe unayejifanya Msalia mtume wakati ni mnafiki kutwa nzima uongo na kuteta watu.
4. Mkristo au Muisilamu unakuta ni mfiadini kwelikweli lakini ni Mwizi, tapeli na mzurumati(Mzurumaji) mkubwa na hana aibu kabisa na kila siku ya ibada ndo kimbelembele na tumbo lake kwenda kuabudu na akitoka huko aachi tabi hizo.
Kiranga atakuwa na nafuu sana kuwa mwizi, tapeli na mzurumaji kwasababu aamini uwepo wa huyo Mungu aliyezuia mambo hayo kuliko wewe unayejidai unaye Mungu wakati hizo tabia hutaki kuziacha.
Msipobadirika Akianani siwatanii Kiranga huyu huyu mtamkuta peponi(Mbinguni) wakati huo wewe unajidhani unamubudu Mungu moto ukikungoja!.
Kiranga ana asilimia kubwa kuurithi uzima wa milele kuliko watu wengi wanafiki!.
Narudia tena "Kiranga anazo asilimia kubwa za kuurithi uzima wa milele kuliko wanafiki walio wengi"
Kiranga ni nani?
Huyu ni jamaa ambaye JF expert ambaye haamini uwepo wa Mungu kabisa.
Mimi kama Mkristo ninaye muamini Mungu,huwa sichukizwi wala sikerwi na ambacho anakiamini Kiranga
Watu wengi wanaojiita Wakristo kwa Waisilamu huwa wanafanya maigizo ya kuishi namna ya mafundisho ya dini zao zinavyotaka,watu wengi wamekuwa washupavu wa hizi dini huku wakimuona Kiranga na wenzie wasioamini uwepo wa Mungu kama walio na dhambi kupitiliza kuliko wao.
Hata wewe kabla hujamjua Mungu yawezekana ulikuwa kama Kiranga na ndugu zake,kibaya zaidi umemjua Mungu lakini bado Kiranga ana unafuu kuliko wewe!.
Kwanini?
1. Kuna mwanamke/mwanaume anayemuamini Mungu lakini kwenye biashara zake pale Kariakoo, Tandika, Mbezi, Buguruni bado anatumia Ushirikina akimini itavuta wateja wengi! Huyu mtu utamkuta kila Ijumaa, jumapili au Jumamosi anaenda kumuabudu Mungu tena anakuwa wakwanza kutiririsha machozi wakati wa maombi lakini akitoka hapo anaendelea na ushirikina wake lakini huyo Mungu wake anayemfanya alie wakati wa maombi anamuweka mfukoni!.
Kiranga atakuwa na unafuu sana kama atafanya biashara akatumia ushirikina kwasababu aamini uwepo wa Mungu kuliko wewe unayejiita Mkristo na unaendelea kutumia Ushirikina.
2. Endelea kufanya Ngono,Uzinzi na Uasherati sana wakati huo huo unajiita Muisilamu au Mkristo na wakati ukielewa kabisa Mungu amekataa!.
Kiranga atakuwa na unafuu sana kufanya uzinzi na uasherati kwasababu aamini uwepo wa Mungu aliyekataza mambo hayo kuliko wewe unayejifanya kumjua huyo Mungu na bado unaendelea kufanya!.
3. Endeleza Uongo,majungu na Usengenyaji kwa sana huku ukiwa na matumaini ya kuirithi pepo au uzima wa milele kutoka kwenye mbingu ya huyo Mungu wako kuliko
Kiranga akiwa muongo, msengenyaji na mfitinishi hiyo ni haki yake kwasababu haamini uwepo wa Mungu wenu ambaye amaekaza hayo mambo kuliko wewe unayejifanya Msalia mtume wakati ni mnafiki kutwa nzima uongo na kuteta watu.
4. Mkristo au Muisilamu unakuta ni mfiadini kwelikweli lakini ni Mwizi, tapeli na mzurumati(Mzurumaji) mkubwa na hana aibu kabisa na kila siku ya ibada ndo kimbelembele na tumbo lake kwenda kuabudu na akitoka huko aachi tabi hizo.
Kiranga atakuwa na nafuu sana kuwa mwizi, tapeli na mzurumaji kwasababu aamini uwepo wa huyo Mungu aliyezuia mambo hayo kuliko wewe unayejidai unaye Mungu wakati hizo tabia hutaki kuziacha.
Msipobadirika Akianani siwatanii Kiranga huyu huyu mtamkuta peponi(Mbinguni) wakati huo wewe unajidhani unamubudu Mungu moto ukikungoja!.