Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Status
Not open for further replies.
Mhariri Mtendaji wa gazeti la Tanzania Daima bwana Kibanda ameandika makala kwenye gazeti la Tanzania Daima kumshutumu Zitto Kabwe kugombea uenyekiti Chadema.Kibanda anafanya kazi chini ya gazeti la Mbowe,swali Mwalimu Nyerere alipewa Uenyekiti wa Tanu akiwa chini ya miaka 30,

Chadema ni Chama cha demokrasia kwanini Kibanda aogope Chadema watimize kauli yao ya Demokrasia kwa Vitendo? kama Kigezo ni Umri Marekani wangempa John MC CAIN kwa vile ni mtu mzima ana mvi kichwa chote. Tanzania Daima la leo lina habari mbili zote za Zitto Kabwe.....

Fungukeni yetu macho
 
sikujua kumbe nafasi ya makamu mwenyekiti wa CDM ilikuwa na ushindani namna hii.

"Wakati uamuzi huo ukiashiria mpambano mkali baina ya wawili hao, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu amechukua fomu kuwania nafasi ya makamu mwenyekiti."
 
Huyu mhariri mada zake nazo hazina mshiko. Ni kweli zito ni pandikizi la ccm lakini si waingie ulingoni?
 
si mara ya kwanza si hii kitu na mara zote sioni pa kuweka mashaka km hii si mojawapo ya article zinazomkaanga mikononi kwa waliokuwa waking'ata vidole kwa hasira kabla hajaingia line.mtendaji husahau ila mtemeewa mh..

Hii ilimmaliza sana mafuta ZITTO WAKATI ANAJIPANGA TENA KUJIFANYA SUPERMAN FROM THE HELL.Kabla Ben saa 8 kumalizia little toka kwa wazee wa jehanum walioahidi wan wana Ccm na factions zake kuwa wata establish utawala wa shetani kwa nguvu na harama yoyote.Hao wazee wa kuzimu ndio zito kala nao kiapo kwa kiasi aliamini kuwa ataua hadi panya na si kuchomoa mkono km wa mudhihiri.

Makala nyingine aliyozhdi waudhi devided magamba ni ile ya kinana..kama nilivyowahi sema tena ccm huwezi appease mtu bila udhi kambi binafsi ya upande mwingine.HUYU JAMAA KWA FIKRA ZA CDM ALIDHANI BUSNESS AS USUAL.
 
Tunashukuru kusikia mawazo toka kwa mtanzania mwenzetu, ingawa mimi hushangazwa sana na jamii hii ya watanzania kwani sina hakika kama wanafahamu maana halisi ya neno demokrasia, siku zote wanataka tuwape viongozi wetu vyeo kirahisi tuu, kwa kuwa mboye ni mwenyekiti basi aendelee kuwa mwenyekiti mpaka atakapo choka mmh sidhani kama hili ndilo tunalo taka wanachadema.

Naimani kuwa tunataka kuwafunza ccm nini maana ya demokrasia na uchaguzi unatakiwa kuwa vipi, si kutumia mlungula tuu so zitto na wengine wemgi wanaojisikia kuchukua fomu wachukue mwisho wa siku kura ndio zitatupa kiongozi.

otherwise kibanda ni muandishi tuu so mara nyingine hukosa la kureport kwa bosi wake then ili aonekane anafanya kazi basi huona aandike lolote, kibanda acha demokrasia ifanyike ili iwemfano kwa chama tawala, na wala chadema siyo sehemu ya utawala wa kifalme mpaka mtu achoke ndio tuweke wengine au kama ccm wanavijana lakini mpaka muwaite vikongwe waje kusaidia kutawala wakati mnavijana
 
hapa kaamdika utumbo wa ajabu , kwa sababu aliajiriwa na mbowe...............ameingia kambi ya lowassa kaanza kuwakandia chadema...na kuwasifia mabwana zake

yet mtu huyu mnamwona hero?? ambaye ataandika lolote kujaza choo? sijajua kwa nn hakufa

wanafiki wabaya sana hawa
 
Nafikiri Zitto wanampamba tu lakini hajawa na uwezo na uzoefu wa kuongoza CHADEMA kama mwenyekiti wa taifa! Uongozi siyo issue ya kuwa DEGREES tu, it is more than that. Hebu yeye mwenyewe au wapambe wake akina CHRISS LUKOSI, ZeMarcopolo and others watueleze ameisidiaje CHADEMA kukua katika Mkoa wa Kigoma na mikoa jirani? Tuelezeni amefanya juhudi gani kuongeza idadi ya wabunge, madiwani, wenyeviti wa vijiji/mitaa, n.k.? Imekuwa ni ''craps'' ambazo tunasikia mara Zitto anataka kupewa sumu mara ooh Zitto hapendwi kwa sababu siyo Mchagga na utumbo mwingine kama huo!

Watu wanaotoka ukanda huo(Ziwa Tanganyika) na jirani zake hawajaona huo umuhimu wa Zitto unahubiriwa na wapambe wake! Labda sasa mtueleze kwa kina mchango wake kwa CHADEMA ni hasa ni upi? CHADEMA ilikuwa maarufu kabla ya Zitto na itaendelea hata bila yeye!! The guy is just too pompasy and greedy, I don't think he deserves the position
 
Umesema kweli mkuu ni kibaraka wa watu analengo la kusambaratisha wenzake.katumwa yule cdm kwa agenda hiyo vitendo na maneno yake vinajipambanua wazi.muendekezeni awavuruge kabla ya 2015.NAPITA TU.
 
Kwa Mwandishi makini na unayeheshimiwa na uliyekomaa kisiasa ni AIBU kuwa upande wa mtu fulani. Nakushauri usubiri wakati wa Kampeini ukifika.
 
Zitto ni mwanasiasa mzuri na mahili ila kuwa mwenyekiti wa CDM na kugombea uraisi kwa tiketi ya CDM bado sana mpaka atakapokuwa ana msimamo thabiti katika kupigania chama yuko kimaslahi yake zaidi anarubunika kirahisi mtu gani kuna wakati alitaka kuanzisha chama chake wakati anajua yeye ni tegemeo CHADEMA.
 
Umri hata siku moja hutakuwa mizani ya kuangalia kama mtu anauwezo wa kuongoza ama la. Hii article ni kama propaganda fulani na pengine Kabwe akisoma inaweza kumpa nguvu zaidi katika nia yake ya kugombea uenyekiti wa chama chake. Si haja kwa kweli ya kutoa mifano ya viongozi ambao hili swala la umri lilitolewa kama kisingizio cha kuwafanya "eti hawapo tayari kuongoza", hivi karibuni tu, Obama wa Marekani, Joseph Kabila wa Democatic Republic of Congo na wengine wengi. Wote hawa wanafanya kazi ya uongozi vema kabisa ....

Cha msingi tu ni yeye (Kabwe) kuwa na stratejia ya kupambana na wapinzani wake kwenye hicho kiti na kufanya kampeni maradufu, kama wananchi wa constituency ya Kigoma North walivyompa kura na kumchagua kuwa Mbunge, ndivyo atakavyoweza kuchaguliwa na wanaCHADEMA kuwa mwenyekiti. Godspeed!

argument nzuri mkuu Sungu,

lakini mwendelezo wa siasa za ndani ya chadema zinaakisi alichochambua Kibanda miaka minne iliyopita, uchambuzi ambao ni tofauti sana na hoja zako. Na hii ndio sababu hasa ya kufuatilia ili kuona mwendelezo wa msigano huu wa kisiasa
 
Hao wite mnao wasifia kuwa wameongoza wakiwa wadogo waliongoza Taifa ambalo lilikuwa halijitambui kwa sasa Taifa linajitambua ndugu sio wakati wa kufanya majaribio.na pia wote mnao watolea mifano wameli mpaka wanatamani kukimbia nchi ndio maana wenye akili timamu wameamua kuwatenga wakiamini wanawapotezea muda tu
 
Zitto ni mwanasiasa mzuri na mahili ila kuwa mwenyekiti wa CDM na kugombea uraisi kwa tiketi ya CDM bado sana mpaka atakapokuwa ana msimamo thabiti katika kupigania chama yuko kimaslahi yake zaidi anarubunika kirahisi mtu gani kuna wakati alitaka kuanzisha chama chake wakati anajua yeye ni tegemeo CHADEMA.

A pragamatist yes! anaweza kuwa politician mzuri lakini sio Zitto Zuberi Kabwe; an Edward Snowden incarnate!!! a seasoned opportunist and Hypocrite, Zitto sio future ya Tanzania wala CDM; labda kama tunazungumzia kubadilisha a Green fisadi with Red/Blue fisadi; then go with Zitto!!
 
KIBANDA SHAKIMOOOOOO!!!!!!!!!!!!! Hakika maandishi hayapotei!!, mazingira dalili na mafindofindo ni yaleyale!! Kama anaakili huyu dogo akae mbali... aache tamaa za kijinga, bado anaumri mdogo kama kuwa atakuwa tu.... Hivi hajiulizi kwanini CCM wanamtafuta kwa udi na uvumba...?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom