Kibanda afanyiwa upasuaji, atolewa jicho moja!

Du.!! Kabla hujafa hujaumbika..walaaniwe wote walio fanya unyama huu.
 
Looh, OMG!

Jicho la plastic? The enemy is wining ... we must do smthing ...!!
...."Weep not my child,
Weep not my darling,
the ravening clouds shall not be victorious,
They shall no longer posses the sky"...by Ngugi.
 
bilashaka kuchapisha makala ndefu iliyohusika na kuwepo chuo cha ugaidi huko ukerewe ndiko kumekuletea huu msiba. Pole sana bwana kibanda, hii ndio gharama ya kulinda na kutetea mstakabali wa nchi yako na watu wake.
 
so sad...tunaishi na magaidi nchi hii.Watanzania tumezidi kuwa wapole ipo siku na mimi nitaamka na panga langu niingie barabarani..this z too much now!!!
Mungu awe nawe Kibanda,u'll get well soon
 
Kibanda amefanyiwa upasuaji chini ya madaktari bibwa watatu, kati ya maktari hao wawili wakiwa ni wataalam wa kichwa na mmoja ni mtaalamu wa macho,

katika upasuaji huo madaktari hao wamegundua kuharibika vibaya kwa jicho la mwanahabari kibanda kiasi cha kulazimika kuliondoa nahivyo wanaangalia namna ya kumwekea la plastiki.

eatv
Maana ya Breaking news imeshakosa maana kwa baadhi ya watu humu.


  • [h=6]LinkBack[/h]
  • [h=6]Topic Tools[/h]
  • [h=6]Search Topic[/h]
  • [h=6]Rate This Topic[/h]


user-offline.png
Manyerere Jackton

Yesterday 16:37
#1
Senior Member
verified.png
Array


Join Date : 11th December 2012
Posts : 151
Rep Power : 343
Likes Received178
Likes Given6



[h=2]
icon1.png
Kibanda aingizwa Theater[/h] Taarifa kutoka South Africa, kupitia Jukwaa la Wahariri Tanzania

1.
Kibanda leo ameingizwa theater ili kuanza kufanyiwa upasuaji na kujengwa sura baada ya kupungua kwa majeraha na uvimbe vilivyokuwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake, hususan kichwani na usoni.

2. Upasuaji huo unazingatia matokeo ya uchunguzi ulifanywa kwa zaidi ya saa 48 na jopo la madaktari na kubaini kwamba mbali na madhara ya awali, Kibanda pia aliumizwa taya lake la kushoto.

3. Kuhusu jicho lake la kushoto ambalo pia lilijeruhiwa, madaktari walisema wangetoa uamuzi kuhusu aina ya upasuaji ambao wangeufanya baada ya kubaini hali halisi wakati watakapokuwa wakijenga sura yake ambayo iliharibiwa kwa majeraha.

4. Wakati akipelekwa theater ambako alikuwa akifanyia upasuaji ambao uliotarajiwa kuchukua saa zaidi ya nne, alikuwa akilalamikia maumivu kutokana na kidonda kilichopo kwenye mguu wake wa kushoto. Kidonda hicho pia ni matokeo ya unyama aliyofayiwa.

5. Jana Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana ambao wako Afrika Kusini kikazi, walimtembelea Kibanda hosipitalini kumjulia hali. Rais Kikwete alisema Serikali inajitahidi kuwasaka wahusika wa tukio la utesaji wa Kibanda na kwamba wakikamatwa watafikishwa mahakamani.

Tutaendelea kufahamishana kila hatua ya tiba ya Mwenyekiti wetu, na tunaomba tuendelee kumwombea ili apone haraka.

--

Neville C. Meena,
Secretary General,
Tanzania Editors Forum - TEF,
Dar es Salaam - Tanzania.
Cell: +255 - 787 - 675555
+255 - 753 - 555556

============
UP DATE
============

quote_icon.png
By Manyerere Jackton
Wapendwa, habari za uhakika zilizofika sasa hivi kutoka hospitalini Afrika Kusini alikolazwa Kibanda ni kwamba ameshatolewa jicho moja ambalo liliharibiwa kabisa na wavamizi. Tayari ameshatoka Theater.Tutaendelea kujuzana.




Kikwete-visits-TEF-chairman.jpg
 
...."Weep not my child,
Weep not my darling,
the ravening clouds shall not be victorious,
They shall no longer posses the sky"...by Ngugi.

Indeed ... ! The enemy must be crushed and made to evaporate to become non victorious clouds!
 
...."Weep not my child,
Weep not my darling,
the ravening clouds shall not be victorious,
They shall no longer posses the sky"...by Ngugi.

Hivi lile la FRONT LINE mtunzi wake alikuwa nani? Pole kwa wanafamilia.
 
Mungu amuafu.....wakati huo huo nafikiria kama tukio hili lingemtokea mtu wa kawaida (kipato cha chini) nadhani angefia pale muhimbili. Hosp[itali zetu tusipoziboresha kukawa na wataalamu wanaoweza kufanya upasuaji wa aina zote.......wa pangu pakavu hatuna uhakika wa tiba.
 
Hii Tanzania inaelekea kubaya. Something must be done soon and very soon
 
anayeyafanya haya mabaya chini ya muhimili wa shetani mungu anamjua, siku mungu atakamilisha ukuu wake na kujibu maombi ya wengi .... atajulikana tuu ... uawezi kutesa wana wa mungu hapa duniani namna hii .... na mungu akitujuza basi atajichagulia adhabu yeye mwenyewe
 
.......Ninamuombea MUNGU amsaidie na nina walaani wote walioanya kitendo hiki kilichosababisha haya yote.....
 
[QUOTE
quote_icon.png
By Manyerere Jackton
Wapendwa, habari za uhakika zilizofika sasa hivi kutoka hospitalini Afrika Kusini alikolazwa Kibanda ni kwamba ameshatolewa jicho moja ambalo liliharibiwa kabisa na wavamizi. Tayari ameshatoka Theater.Tutaendelea kujuzana.




Kikwete-visits-TEF-chairman.jpg
[/QUOTE]

Unaelewa nini kwa wanaomjalia hali.

Somo "Usiamini hata siku mmoja maadui zako kaa mbali nao". Mara nyingi wao hukumbuka makosa uliyowatendea na siyo mema unayofanya sasa. HAWATAKUSAMEHE.
 
I love Manyerere Jackton, he is a reall son-of-a-gun. Manyerere Jackton is a Dedicted Journalist who wants right on every side, his and mine too. Lakini Manyerere Jacton is a New-Generation young man who does not know and cannot truely comprehend why (for example) Mwalimu Nyerere was known to have 'kionambali". Ukimwambia Mtemi Fundikira kuhusu kionambali atakwambia anataka wenye nacho ndiyo wamwongoze. Manyerere anataka kiongozi mwenye bashasha, mcheshi, mbunifu n.k. Lakini Manyerere, hii ni Dunia ya Mungu na inaongozwa na Mungu Mwenyewe. Matakwa ya Mungu katika wabadamu hujulikana kwa wenye hivyo unavyoita vionambali. Hao huambiwa kesho kutakuwa na dhoruba, na keshokutwa ukame. Usidanywe na Idd Amini mwenye ndoto za mwendawazimu, waulize wazee wako kama kuna mwenye kionambali katika nchi. Mkimficha wote mnajitafutia majanga, wewe na wazee wako na hili wazee wengi sana huwa hawalitaki kwa sabau ni majanga ya kujitakia. Msimamo wa Manyerere Jackton kama kijana na mwana habari ni kutuingiza vichochoro vya kutoelewa nini maana ya kionambali kwa sababu tu vijana wamepata kusema bila kusahihishwa na wazee.Uhuru wa kuongea hata Masai aliukataa kwa Morani, siyo ujinga, ndiyo ujanja wenyewe wa kujua makubwa ya Mungu. Manyerere, tumwombee ndungu yetu Kibanda apone na arudi salama lakini meno matatu na jicho moja hana. Usidhani nafurahia hali hii ya Kibanda, nasikitikia sana pia na hali ya Dr. Ulimboka ambao sasa hivi nina hakika wataishia kuwa "Siri ya Taifa" kama mnavyowaita. Kinachonikera ni kuwepo akina Manyerere Jackton na kalamu zao wakitamba kila mahali bila kuona hatari wanazoziparamia. Sasa hivi Watz tumegeuka waganga majeraha baada ya kuangukia mikenge badala ya kuikwepa tukaenda salama. Mara mitihani, mara Padri kauwawa, mara Ulimboka katekwa. Tume za kuchunguza haya ni kipofu kusaka sindano gizani ambapo hata Kikwete mwenye macho haioni. Manyerere amka kutoka ujingani, tutakwisha huku tukionana wakati tunahudhuria misiba ya waliotutangulia.


Jogoo la shamba, nimesoma waraka wako. Umetoa changamoto kubwa, si kwangu tu, bali kwetu sote tunaopenda kuiona Tanzania ile iliyodhamiriwa kujengwa na wazee wetu. Kuna makala nimendika kuhusu Kibanda. Nisingependa isomwe kabla ya Jumanne-siku ambayo JAMHURI linakuwa mikononi mwa wasomaji. Kwa ufupi ni kwamba Watanzania wote, bila kujali rika, jinsi, hali, imani au aina yoyote ya tofauti zetu kama binadamu, tunapaswa kuungana kuifanya Tanzania kuwa mahali pazuri pa kila mmoja wetu kuweza kuishi. Miaka kadhaa iliyopita Tanzania ya aina hiyo ilionekana kupatikana, lakini kadri siku zinavyokwenda, sifa hiyo ya uungwana inapotea. Wajibu huu wa kuifanya Tanzania kuwa mahali pazuri ni wa wanahabari, madaktari, madereva, wachuuzi, walimu, wanasiasa, wafanyabiashara, waliooa na wasiooa, vilema na wazima, wazee, vijana na kila mmoja miongoni mwetu. Matukio ya kuvamiwa kwa KIbanda na wanahabari wengine, aidha, tukio la kuawa kwa Mwangosi na Watanzania wengine, ni mengi. Kama Taifa tunapaswa kusema "IMETOSHA". Naamini kabisa, kwa umoja wetu, na kwa mapenzi ya Mungu, tunaweza kurejea kwenye umoja, mshikamano na udugu wetu.
 
Jogoo la shamba, nimesoma waraka wako. Umetoa changamoto kubwa, si kwangu tu, bali kwetu sote tunaopenda kuiona Tanzania ile iliyodhamiriwa kujengwa na wazee wetu. Kuna makala nimendika kuhusu Kibanda. Nisingependa isomwe kabla ya Jumanne-siku ambayo JAMHURI linakuwa mikononi mwa wasomaji. Kwa ufupi ni kwamba Watanzania wote, bila kujali rika, jinsi, hali, imani au aina yoyote ya tofauti zetu kama binadamu, tunapaswa kuungana kuifanya Tanzania kuwa mahali pazuri pa kila mmoja wetu kuweza kuishi. Miaka kadhaa iliyopita Tanzania ya aina hiyo ilionekana kupatikana, lakini kadri siku zinavyokwenda, sifa hiyo ya uungwana inapotea. Wajibu huu wa kuifanya Tanzania kuwa mahali pazuri ni wa wanahabari, madaktari, madereva, wachuuzi, walimu, wanasiasa, wafanyabiashara, waliooa na wasiooa, vilema na wazima, wazee, vijana na kila mmoja miongoni mwetu. Matukio ya kuvamiwa kwa KIbanda na wanahabari wengine, aidha, tukio la kuawa kwa Mwangosi na Watanzania wengine, ni mengi. Kama Taifa tunapaswa kusema "IMETOSHA". Naamini kabisa, kwa umoja wetu, na kwa mapenzi ya Mungu, tunaweza kurejea kwenye umoja, mshikamano na udugu wetu.
Hivi wewe ni pacha na Mzee wa Kwembe kati?
 
bilashaka kuchapisha makala ndefu iliyohusika na kuwepo chuo cha ugaidi huko ukerewe ndiko kumekuletea huu msiba. Pole sana bwana kibanda, hii ndio gharama ya kulinda na kutetea mstakabali wa nchi yako na watu wake.

kama ndo hivyo basi isiwe mwisho wa harakati zake kama dr. Ulimboka kwani watajitangazia ushindi kama walivyojitangazia kwa huyu dr.
 
Back
Top Bottom