Kazi za Kiongozi Mkuu wa ACT-Tanzania

Kama chadema walivyompa uenyekiti DJ MBOWE

Pamoja na kwamba Mbowe hajawahi kuwa Dj bali mmiliki wa ukumbi,nina kurudisha kwa mmoja wa marais bora wa Marekanr Regan alikuwa muigizaji wa filamu, Sanaa haimzuii mtu kuwa kiongozi mzuri. Rekebisha mindset yako!
 
Wow...Sasa ni nini faida ya umiliki kama huna hata mamlaka ya kuteua mjumbe wa halmshauri ya kata? Mtei ni muasisi na mwanzilishi wa Chadema na kwa mujibu wa katiba ya CDM, muasisi hana nguvu yoyote ya kupindisha functions of katiba. Anaweza kutoa ushauri tu kwa chama na si lazima ushauri huo ufuatwe kama vile Mwl. Nyerere alipogomea kufuata ushauri wa Mtei (Chanzo cha kujiuzuru ugavana).
 
ACT ni Tishio kubwa kwa uhai wa CHADEMA.

kamati kuu ya ccm isipompitisha Lowassa km mgombea wake wa urais wallahi huo ndio utakuwa mwisho wa ccm ktk ramani ya kisiasa duniani,Leo asubuhi ktk kipindi cha watoto ITV,mmoja wa watoto waliohudhuria kipindi kile anaulizwa unafikiri nani atakuwa rais wa 5 wa JMT confidently anajibu Lowassa,napenda kukumbusha kuwa mpaka dakika hii lowasa 2 ccm 0 mbaya zaidi ni dakika ya 89 na kwa jinsi mlivyozidiwa hamna uwezekano wa kurudisha hizo goli mlizokwisha fungwa.
 
Mkuu mimi siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini kwa muda nimekuwa nikiona michango yako haswa jukwaa hili imekaa ki nafiki nafiki sana, ndiyo zzk anamazuri yake lakini ana mabaya pia na kama huu ni mpango wake sasa demokrasia aliyokuwa anatuaminisha nayo imeishia wapi, angaza zaidi ya bavicha na chadema mkuu, vyote hivi vinamwisho si Tanzania

Unapoteza muda wako. Watu aina ya huyo wameshashupaa wala hawashauriki, ila jaribu bahati yako labda utafanikiwa. Mi nimeshakata nao tamaa.
 
shikamoo zitto kabwe kama hadi hapa watu wasipokujua wewe ni msaka tonge na madaraka kwa pamoja basi watakuwa ni vipofu wa kuamini zaidi ya thomaso
 
Hahaha Dah.. asingepewa uongozi wowote bado kuna watu wangesema aliepewa uenyekiti kawekwa kama pazia ZZK ndo atakuwa anatoa amri. Jamani wanachama wa ACT wameamua, waachieni chama chao turudi kuongea siku likibuma.
 
PakavuNateleza weka majukumu ya mwenyekiti

Majukumu ya mwenyekiti wa ACT ni haya yafuatayo. Mods naomba mpandishe hii post Juu.

/*l) Kazi za Mwenyekiti wa Chama Taifa :*/
i)Atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa kiongozi mkuu wa ACT-Tanzania
ii) Atakuwa mlinzi mkuu wa sera zilizopendekezwa na kupitishwa au jambo
lolote litakaloamliwa na kupitishwa na vikao cya chama na kuhakikisha
kuwa ngazi zote za chama zinatekeleza maamuzi yaliyotolewa
na
kuhakikisha kuwa ngazi zote zinafanya kazi ndani ya mipaka ya katiba,
kanuni, sera na maamuzi yoyote yaliyoagizwa na vikao vikuu vya chama
iii) Atakuwa mwenyekiti wa mikutano yote ya chama ya kitaifa isipokuwa
vikao vya utendaji
iv)
Atafanya shughuli nyingine za Chama kama atakavyoelekezwa na
Kiongozi Mkuu wa Chama
v) Katika mikutano anayoiongoza zaidi ya kuwa na kura yake ya kawaida
atakuwa pia na kura ya uamuzi endapo kura ya wajumbe wanaoafiki na
wasioafika zitalingana

Kama ulivyoona mwenyekiti anaripoti kwa ayatollah ZZK
 
Last edited by a moderator:
Majukumu ya mwenyekiti wa ACT ni haya yafuatayo. Mods naomba mpandishe hii post Juu.

/*l) Kazi za Mwenyekiti wa Chama Taifa :*/
i)Atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa kiongozi mkuu wa ACT-Tanzania
ii) Atakuwa mlinzi mkuu wa sera zilizopendekezwa na kupitishwa au jambo
lolote litakaloamliwa na kupitishwa na vikao cya chama na kuhakikisha
kuwa ngazi zote za chama zinatekeleza maamuzi yaliyotolewa
na
kuhakikisha kuwa ngazi zote zinafanya kazi ndani ya mipaka ya katiba,
kanuni, sera na maamuzi yoyote yaliyoagizwa na vikao vikuu vya chama
iii) Atakuwa mwenyekiti wa mikutano yote ya chama ya kitaifa isipokuwa
vikao vya utendaji
iv)
Atafanya shughuli nyingine za Chama kama atakavyoelekezwa na
Kiongozi Mkuu wa Chama
v) Katika mikutano anayoiongoza zaidi ya kuwa na kura yake ya kawaida
atakuwa pia na kura ya uamuzi endapo kura ya wajumbe wanaoafiki na
wasioafika zitalingana

Kama ulivyoona mwenyekiti anaripoti kwa ayatollah ZZK

kweli hiki ni chma cha Ayatollat Zitto
 
Kwa mujibu wa Katiba ya ACT ZZK atakuwa na madaraka yafuatato

"Kazi za Kiongozi Mkuu wa ACT-Tanzania

i) Atakuwa kiongozi mkuu wa chama kwenye mikutano mikuu ya chama Taifa, mkutano mkuu, Halmashauri Kuu na Kamati Kuu.

ii) Atakuwa mkuu wa siasa, mshauri na mwelekezaji kwa viongozi wote na maafisa wa ACT-Tanzania

iii) Kuteua wajumbe watano wa Kamati Kuu kwa mujibu wa Katiba hii

iv) Atakuwa ndiye mtoa tamko rasmi kuhusu masuala ya sera na mtazamo wa chama

v) Atakuwa mtoa habari mahususi kwenye mkutano mkuu, Halmashauri Kuu na Kamati Kuu kuhusu hali ya kisiasa nchini na masuala mengine ya kitaifa na kimataifa.

vi) Atasimamia, kufunza na kutoa maelekezo kuhusu shughuli zote za ACT-Tanzania

vii) Iwapo kiongozi wa ACT-Tanzania hayupo kwa sababu yoyote ile basi Mwenyekiti wa chama Taifa atakuwa Kaimu kiongozi mkuu wa Chama.

viii) Iwapo kiti cha kiongozi mkuu wa Chama kitakuwa wazi kwa sababu ya kujiuzulu, kuondoka katika Chama, kuvuliwa uongozi au uanachama, maradhi yenye kuondoa uwezo wa kufanya kazi au kifo, utaratibu ulioelezwa katika

(vi) ya ibara ndogo hii utatumika kwa sharti kwamba Mkutano Mkuu Maalumu wa Taifa utaitishwa katika muda usiozidi miezi sita tangu kuwa wazi kwa kiti hicho kwa ajili ya kuchagua Kiongozi Mkuu wa Chama mwingine.

ix) Ataweza kuondolewa kwenye madaraka baada ya mapendekezo ya Halmashauri Kuu ya Taifa kwa azimio la Mkutano Mkuu wa Taifa
litakaloungwa mkono na theluthi mbili ya kura za wajumbe halali waliohudhuria na kupiga kura.

x) Atakuwa ni nuru na taswira ya ACT-Tanzania"

Jamaa anauchungu n pessa zake
 
Back
Top Bottom