Kauli ya Chagulani dhidi Manyerere (Council Mwanza) ni sahihi kwa afya ya CHADEMA?

“Mimi ninataka niseme ukweli kwa sababu siogopi mtu, mimi ni taasisi inayojitegemea, sina imani na wewe mwenyekiti (Meya wa Jiji la Mwanza), umekuwa hufuati kanuni, utaratibu wako wa kuendesha vikao kila mara unataka kusababisha vurugu, ninataka baada ya hapa nipewe karatasi mimi nitakuwa wa kwanza kuandika jina langu ili nipate idadi ya madiwani 10 wanaoweza kuleta hoja kuomba tukupigie kura ya kutokuwa na imani na wewe,” alisema diwani huyo kijana.

Habari zaidi soma hapa Raia Mwema - CHADEMA yatikisa mashabiki wake

Hii ni kauli ya Chagulani kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani wa Jiji la Mwanza alipowataka Madiwani wapige kura ya kutokuwa na imani na Meya wa Jiji hilo Bw. Josephat Manyerere (CDM). Kwenye orodha ya waliosaini kumpiga chini meya Manyerere jina la Chagulani ni la kwanza, kisha linafuatiwa na mwenzake Matata halafu wanafuata madiwani wa CCM na CUF. Hakuna jina la diwani mwingine wa CDM aliyesaini.

My Take:
1. Ni Kweli Chagulani hakutakiwa kuogopa wala kujali chochote na kwamba yeye ni taasisi inayojitegemea? Hana taasisi (Chama) kilichomu-endorse ambacho alipaswa kuongozwa na katiba, sheria na taratibu zake? Si kwamba, hii ni jeuri kuu ambayo haieleweki ni wapi inatoka?

2. Kwa nukuu hii si kwamba, Bw. Chagulani alikuwa anatekeleza mradi aliotumwa na CCM? Kitendo cha yeye kuanza kwa kujihami kuwa, haogopi mtu na kwamba yeye ni taasisi huru inayojitegemea kinatafsiriwa wazi, alikuwa na maelekezo kichwani kutoka kwa chama chake yaani CDM lakini alikaidi makusudi pengine ni kutokana na yeye kuwa na mradi aliokuwa anautekeleza (Bila shaka kuupata umeya/malipo kutoka CCM)

Tujadili.

Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. Na kwamuungwana ni ngumu nyeusi kuita nyeupe!! Hivi kunamkazi gani wa Mwanza asiyejua madudu yaliyofanywa na aliyekuwa meya. Think Deep CHADEMAS!!! Mbona baada ya kukemewa na CHAGULANI, baadae Meya alioondolewa? Tatizo walitaka eti Meya akaripiwe kwenye vikao vya chama. Hivi huyu Meya si alichaguliwa katika vikao vya madiwani? Kwanini asiwajibike kwao? Stahili hii ya vikao vya chamani kwenye utekelezaji wa taratibu za madiwani, hivi inatofauti na vikao vya ndani vya wabunge wa CCM ambavyo vimekuwa kiini cha kulinda mafisadi bungeni?

MIMI nimeanza kuogopa sasa!! Kwani hapa inaonekana kunya anye kuku akinya bata kaharisha. Tuliiondoa CCM tuwe na taratibu mpya za uedeshaji mambo. Ambapo Tanzania kwanza, Chama baadae.

NDUGU mtoa mada, tafuta ukweli na jiepushe na mlengo, kwani chadema tunaamini katika ukweli. Na ukweli ni kuwa CHADEMA mwanza kuna mgogoro. Issue si Chagulani wala Matata, Tuutafute UKWELI kwa ustawi wa TZ na CHADEMA

 
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. Na kwamuungwana ni ngumu nyeusi kuita nyeupe!! Hivi kunamkazi gani wa Mwanza asiyejua madudu yaliyofanywa na aliyekuwa meya. Think Deep CHADEMAS!!! Mbona baada ya kukemewa na CHAGULANI, baadae Meya alioondolewa? Tatizo walitaka eti Meya akaripiwe kwenye vikao vya chama. Hivi huyu Meya si alichaguliwa katika vikao vya madiwani? Kwanini asiwajibike kwao? Stahili hii ya vikao vya chamani kwenye utekelezaji wa taratibu za madiwani, hivi inatofauti na vikao vya ndani vya wabunge wa CCM ambavyo vimekuwa kiini cha kulinda mafisadi bungeni?

MIMI nimeanza kuogopa sasa!! Kwani hapa inaonekana kunya anye kuku akinya bata kaharisha. Tuliiondoa CCM tuwe na taratibu mpya za uedeshaji mambo. Ambapo Tanzania kwanza, Chama baadae.

NDUGU mtoa mada, tafuta ukweli na jiepushe na mlengo, kwani chadema tunaamini katika ukweli. Na ukweli ni kuwa CHADEMA mwanza kuna mgogoro. Issue si Chagulani wala Matata, Tuutafute UKWELI kwa ustawi wa TZ na CHADEMA


well said mkuu
 
Binafsi sipendezwi na hukumu ya mwisho kuwa ni kufukuzana kwenye chama.haya ni maamuzi ambayo kwa namna moja au nyingine lazima yanakiathiri chama,penda usipende.kuna watakaosema ni ubabe,umwamba na matumizi ya nguvu kubwa kwa kitu kidogo.huyu sheikh chagulani na mwenzake wangeweza kupewa onyo kali na wakajirekebisha chama kikabaki na heshma yake kama kawaida
 
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. Na kwamuungwana ni ngumu nyeusi kuita nyeupe!! Hivi kunamkazi gani wa Mwanza asiyejua madudu yaliyofanywa na aliyekuwa meya. Think Deep CHADEMAS!!! Mbona baada ya kukemewa na CHAGULANI, baadae Meya alioondolewa? Tatizo walitaka eti Meya akaripiwe kwenye vikao vya chama. Hivi huyu Meya si alichaguliwa katika vikao vya madiwani? Kwanini asiwajibike kwao? Stahili hii ya vikao vya chamani kwenye utekelezaji wa taratibu za madiwani, hivi inatofauti na vikao vya ndani vya wabunge wa CCM ambavyo vimekuwa kiini cha kulinda mafisadi bungeni?

MIMI nimeanza kuogopa sasa!! Kwani hapa inaonekana kunya anye kuku akinya bata kaharisha. Tuliiondoa CCM tuwe na taratibu mpya za uedeshaji mambo. Ambapo Tanzania kwanza, Chama baadae.

NDUGU mtoa mada, tafuta ukweli na jiepushe na mlengo, kwani chadema tunaamini katika ukweli. Na ukweli ni kuwa CHADEMA mwanza kuna mgogoro. Issue si Chagulani wala Matata, Tuutafute UKWELI kwa ustawi wa TZ na CHADEMA


Mkuu Mkata Ufuta; kuna tofauti kubwa sana kati ya vikao vya Wabunge wa CCM wawapo Dodoma na hiki kilichomkuta Chagulani.

Mimi si muumini wa siasa za kufukuzana lakini naamini katika Collective Responsibility (Maana kama haukubaliani na msimamo wa wengi unatakiwa uwe kimya/uwe passive na si reactionary as far as bado unaamini itikadi ya hao wengi), kufuata Katiba,Sheria na Kanuni zinazoongoza taasisi zilizo chini yetu na kwa hili ni chama chako cha Siasa.

Sasa hoja kwamba, Meya alionesha uwezo mdogo katika kuongoza ni issue nyingine. Tatizo linalojitokeza kwa Chagulani pamoja na ukweli unaoweza kuwepo kuwa Meya alikuwa incompetence ni kile alichokionesha mwanzo kabisa kuutaka Umeya wa jiji la Mwanza. Na hata alipotak
iwa kuondoa jina kwenye kinyang'anyiro cha Umeya ili kumuachia mwenzake Josephat Manyerere hakuacha kuendelea kuwinda kiti hicho pamoja na nafasi hiyo ya umeya kuwa mikononi mwa Chama chake. Kwake yeye (Chagulani) kilio na hitaji lake ni kuupata umeya. Ndiyo maana baada ya kuondoa jina kwenye uchaguzi huo wa meya arirudi msituni na kujipanga upya kwa njia za panya (Zisizo na baraka za Chama chake ) akishirikiana na vyama visivyo na mlengo mmoja na chama chake ili kumuondoa meya Manyerere.

Hapa utagundua mambo makuu matatu
1. Kwa Chagulani kazi aliyokuwa nayo ni kuwinda zaidi madhaifu ya meya Manyerere kuliko mazuri yake ili apate upenyo wa kumdondosha na hatimaye agombee. Ndiyo maana alipofanikisha mradi wake huo ili kuficha uchu wake wa madaraka na pia kuogopa kunyooshewa vidole alikimbilia haraka kutangaza kuwa, hatagombea nafasi hiyo. Alijua alichokuwa anafanya na pengine muda wa uchaguzi ungefika tungeona sura yake halisi zaidi
2. Kwa Chagulani anapotafuta madaraka/cheo chama si lolote ndiyo maana alikuwa tayari kushirikiana na 'maadui' wa chama chake (CCM na CUF) ili kummaliza Meya anayetoka katika chama chake. Hili linajionesha zaidi katika nukuu yake anaposema "Mimi siogopi mtu na ni taasisi inayojitegemea'.
3. Chagulani ameonesha ama kulikuwa na nguvu ya fedha (Aliyopewa) au ahadi fulani aliyokuwa nayo kama angefanikisha mradi wake huo.
4. Ama Chagulani hakujua matokeo ya hiki alichokuwa anapigania kutokana na kusukumwa na Siasa za 'kitoto' zinazotokana na mihemuko na harakati za vyuoni tu pasipokusoma mazingira halisi ya siasa za ushindani hapa nchini au alikuwa anajua hilo alitendalo na hakika alijua mwisho wake ni upi na ni kitu gani atapata.
 
Huyu **** alikuwa anapima upepo ati Lol!!imekula kwako kilaza kumbe hata chuo hajamliza na ulifukuzwa kwa ujinga wako kama huu huu ulofanya kama sikosei sasa imekula kwako na waliokutuma ss wanakucheka.Hivi kwa nini usisome alama za nyakati hujaona wala kusikia wale mafala wengine wa Arusha ushaona sasa hawana chao wanatapatapa na kuota kuwa huenda wakarudishwa chamani lol wajinga ndio waliwao.kaka imekula kwako

Mkuu kwenye hizi Siasa kuna wanaoangalia masilahi peke yake, wanaona umbali usiozidi urefu wa pua zao. Kama huyo Chagulani alipewa pesa kidogo huenda akajiona ameshinda, hii inaleta maana sana kwake hasa ukichukulia kwamba hakuwahi kushika pesa nzuri tangu amalize shule. Kuna udhaifu mkubwa upande huu kwahiyo CDM wanapaswa kuwasoma viongozi wao kwa umakini zaidi kidogo.
 
Inasemekana kuwa Adam Chagulani huenda akahamia CCM ili kuendeleze azima yake ya kuidhorotesha CHADEMA Mwanza.
 
wanafiki huwa hawana maisha marefu...nasikia walikua na mpango wa kumuweka Stan Mabula ili awe Meya CDM wakawashtukia mapema..pia wananchi huku wamechoka na swaga zake za migogoro
 
Huyu amefungua kesi mahakamani kupinga kuenguliwa kwake ktk uongozi? akihama kesi yake itakuwaje mahakama inaweza kumtaka aendelee kuwa diwani wa jmbo la mahakama kupitia CDM
 
Binafsi sipendezwi na hukumu ya mwisho kuwa ni kufukuzana kwenye chama.haya ni maamuzi ambayo kwa namna moja au nyingine lazima yanakiathiri chama,penda usipende.kuna watakaosema ni ubabe,umwamba na matumizi ya nguvu kubwa kwa kitu kidogo.huyu sheikh chagulani na mwenzake wangeweza kupewa onyo kali na wakajirekebisha chama kikabaki na heshma yake kama kawaida

Wewe ni kati ya wale wasioamini mfumo wa kuwajibika na uzingatiaji wa katiba/sheria/kanuni na pengine hujui kwamba kulembuliana macho na kuoneana haya ndiko kumelifikisha taifa letu kwenye lindi hili la ufukara. Kwa sasa tunahitaji sana mfumo wa utawala wenye kuwajibika na hata kuwajibishana kama ikibidi.

Suala hapa la kuangalia ni Je taratibu zimefuatwa katika kuwajibisha? Sasa kwa Chagulani ni wazi ukifuatilia sakata lake ni kwamba, CDM ilimvumilia vya kutosha na ilishampa muda wa kujitetea tena mara mbili na baadaye baada ya kuona hajirekebishi alipewa muda wa mwaka mmoja kuwa kwenye uchunguzi maalum. Hakuna sababu ya kulea maovu eti kwa kigezo kuwa huyu ni mwenzetu,kufanya hivyo ni kukaribisha kifo cha taasisi/chama.
 
Mjadala wa msingi unatakiwa kuangalia kama utendaji wa meya ulikuwa na ufanisi au ulikuwa legelege. Kitendo cha CHADEMA kukasirishwa na meya legelege kuondolewa ni ujumbe kwa wenye akili...
 
Chadema hakuna demokrasia. Ukitofautiana na slaa wewe basi au bwana mtei wewe kwisha. Ndo maana zito kabwe ni mkiwa ndani ya chadema. Labda watwaambie wao demokrasia ninini??
 
kuna watu wanacheka huku wanalia ndani ya CHADEMAi mtoke si mtoke tu??. Angalieni historia za viongozi woote wa CHADEMA wakiwa vijana naona wanamatukio yanayofanana. Ndo maana walitaka kuvuruga Sensa kwa mikutano ya kampeni za kulazimisha.
 
kuna watu wanacheka huku wanalia ndani ya CHADEMAi mtoke si mtoke tu??. Angalieni historia za viongozi woote wa CHADEMA wakiwa vijana naona wanamatukio yanayofanana. Ndo maana walitaka kuvuruga Sensa kwa mikutano ya kampeni za kulazimisha.
Bangi mbaya
 
kuna watu wanacheka huku wanalia ndani ya CHADEMAi mtoke si mtoke tu??. Angalieni historia za viongozi woote wa CHADEMA wakiwa vijana naona wanamatukio yanayofanana. Ndo maana walitaka kuvuruga Sensa kwa mikutano ya kampeni za kulazimisha.
Huyu amefungua kesi mahakamani kupinga kuenguliwa kwake ktk uongozi? akihama kesi yake itakuwaje mahakama inaweza kumtaka aendelee kuwa diwani wa jmbo la mahakama kupitia CDM
Chadema hakuna demokrasia. Ukitofautiana na slaa wewe basi au bwana mtei wewe kwisha. Ndo maana zito kabwe ni mkiwa ndani ya chadema. Labda watwaambie wao demokrasia ninini??
nilibahatika kuangalia kipindi cha Malumbano ya Hoja ITV juzi na mchangiaji mmoja ali-emphasis katika kitu kinaitwa ITIKADI (Ideology??). Hili ni tatizo kubwa na linafanya watu wapoteze muda wao kwa kutoelewa ni kwa nini wapo hapa duniani na hasa ukichukulia muda wa maisha ulivyo mfupi!
Mtu anajiunga cdm kabla hata ya kushika wadhifa wowote wa juu au kukitumikia chama katika wakati wa shida anatangaza kujitoa kwa visingizio kuwa "ni chama kisicho na dira", "...ni cha kidini", "...ni cha wachagga" nk nk. Sasa unajiuliza uliingiaje bila kufanya hata uchunguzi na kujua hayo!!???? Haraka unaweza kugundua kuwa "alifanya maamuzi bila kufikiri". Kibaya zaidi utamsikia akirejea CCM (ref. Sambwee Shitambala), ni bora watu kama hawa wangelienda CUF, TLP, UMD nk kwa maana matatizo ya nchi hii kila mtu anayajua na walio wengi wameanza kuelewa chanzo cha matatizo haya ....kuwa yamesababishwa na CCM! Hivyo kurudi huko ni sawa sawa na kuukataa ukweli ambao kila mtu tayari anaujua.

Kama kweli anarudi CCM basi na aende lakini mfano wake ni sawa na mtu ambaye katika vizazi kadhaa vya jamii yake hawakuwahi kupata elimu hata ya msingi na leo amepelekwa shule kwa bidii za watu kutoka jamii nyingine alafu anapofika Form II anajiona amepata elimu ya kutosha na kuamua kurudi kwenye jamii alikotoka huku akijiona yuko huru zaidi na msomi!

Kuna haja ya mtu kuelewa vision ya chama kabla ya kujiunga ili hukombeleni ikamsaidia kuepukana na mawazoya kubakia madarakani na 'ushindi ni lazima' tu kama njia ya existence




 
Mwacheni Chagulani aende salama kwa Baba ya wa UFISADI Tanzania.

Lakini kubwa zaidi ni kwamba asisahau pia kuhama huo mji maana nako huenda kusikalike kwake ki-urahisa sana kulingana na jinsi ambavyo vijana CHADEMA wanavyoendelea kutafakari matendo yake ya ki-hujuma jijini Mwanza.

Inasemekana kuwa Adam Chagulani huenda akahamia CCM ili kuendeleze azima yake ya kuidhorotesha CHADEMA Mwanza.
 
Back
Top Bottom