Kauli ya Chagulani dhidi Manyerere (Council Mwanza) ni sahihi kwa afya ya CHADEMA?

Adam wewe kama msomi ulipaswa ujue nini cha kusema na wapi. Nimewahi kuwa kiongozi wa mradi kwa kitaifa unaofanyika kimataifa nijuavyo mimi katibu/mtendaji ndio anashauriana na mwenyekiti kuitisha vikao, mara nyingi ratiba ya vikao huwa inajulikana hivyo mtendaji muda ukikaribia humwalifu mwenyekiti ili waweze kutekeleza ratiba. Ukiona mwenyekiti ndo anakuwa mbele sana, bila mtendaji ujue ni ktk hali ya dharura na ukweli ni migongano ktk uongozi. Mikutano ya kawaida ya h/w inabidi CD/DED atoe taarifa sasa kama taarifa hazipo meya ataitisha kikao ili diwani aje kuchukua posho kisha aaondoke???? kwa hiyo ni muhimu sana CD kuhusika ktk mipango ya vikao, anawasiliana na meya kwa maana ya kufix tarehe na mambo madogomadogo kama yapo;

Zaidi Adam kama uliona meya anapwaya au anafanya vivyo isivyo ulipaswa kumshauri meya kwanza nje ya vikao, ndani ya vikao vya chama, kumshitaki ngazi za juu za chama, na kama hupati msaada wowote na hali inazidi kuwa mbaya ndipo umwage kwenye vikao vya wananchi/baraza la madiwani ambalo ni la wazi.

Ni kuulize swali kama meya anapotoshwa na CD tunafanyaje??? maana umeya sio taalum, CD ndo amempelekea meya asaini huku akijua meya anahitaji baraka za baraza, kwani nini cd asipewe onyo kwa makosa hayo??? tumeona hata kwa rais wa nchi, meya ni rais wa h/jiji la mwanza, iweje mtendaji amtegesheeee huoni hila hizo za KICCM CCM??? CD ni mdhoefu sana wa miaka na miaka wa vikao vya madiwani na mamlaka yake meya ni mgeni kabisaaa, dhamana kubwa hasa mambo ya kisheria ya uendeshaji wa jiji ni CD, kama anampotosha meya apigwe chini.

Kuhusu mtendaji wa kata, kwanza sio vema kwa msomi kuchagua mtu wa kufanya nae kazi, huo nao umeonesha udhaifu. pili kama mwanachadema unajua CCM haina watu hata ukibadilisha vipi, sasa unalalamika kuhusu WEO atatoka wapi??? ni mpaka wananchi wapige chini kabisa CCM ndo mambo yanyoke 100% kwa sasa tunalazimika kufanya nao kazi hivyo hivyo tukisubiri uamuzi wa wananchi 2015. au nawewe unataka uletewe WEO mpenzi wako???? nani amekuhakikisha atakayekuja ni mzuri kuliko aliyepo???

Kwenye siasa fitina ni siasa, unapaswa uzishinde na wala sio kutulalamikia kuwa unafanyiwa zengwe, siasa ni zengwe amini usiamini; maana hata ndani ya chama kunawatu wanataka nafasi yako achilia mbali nje ya chama. na ni haki yao, so kuwa smart kushinda fitina za siasa, acha kukurupuka utanasa kwenye mtego; i mean himili mkiki ya siasa na usilalamike kuhusu zengwe, maana hata wewe unafanya mizengwe kwa upande mwingine. Ukiona unaelemewa unapaza sauti, hakuna wa kukuonea huruma pigana na kuwa smart it will work.

Fumagila nimefika maana nilifanya siasa mwaka 2010, nakuunga mkono daraja hilo lijengwe tena kuwa mwehu kabisa; ila usipoteze sheria za mchezo wa siasa; tumia wananchi daraja litajengwa. Na kwa kutumia forum hii nimtake meya ajenge daraja hilo kwa bajeti ya mwaka huu, kama atapuuzia haya.

Mwisho maana sitaki nikujibu hoja zote, kuwa makini hasa na watu unaunda kundi nao, i repeat kuwa makini; ndani yake wamo vijana wa CCM/serikali; nimekuona nao, nawafahamu siku mingi sana na wananifahamu. Nimewaona kwenye kundi lako tena wanachangia sana hoja. Na hapo ndo wasiwasi wa shughuli zako uliponiijia, wale vijana ni smart guys be careful labda kama nawe wewe ni mmoja wao. JUA KUWA NGUVU YA UMMA inatokana na umma wenye nguvu; Watanzania kwa sasa wamejenga umma wenye nguvu.

kula like yangu mzee.
 
Adam wewe kama msomi ulipaswa ujue nini cha kusema na wapi. Nimewahi kuwa kiongozi wa mradi kwa kitaifa unaofanyika kimataifa nijuavyo mimi katibu/mtendaji ndio anashauriana na mwenyekiti kuitisha vikao, mara nyingi ratiba ya vikao huwa inajulikana hivyo mtendaji muda ukikaribia humwalifu mwenyekiti ili waweze kutekeleza ratiba. Ukiona mwenyekiti ndo anakuwa mbele sana, bila mtendaji ujue ni ktk hali ya dharura na ukweli ni migongano ktk uongozi. Mikutano ya kawaida ya h/w inabidi CD/DED atoe taarifa sasa kama taarifa hazipo meya ataitisha kikao ili diwani aje kuchukua posho kisha aaondoke???? kwa hiyo ni muhimu sana CD kuhusika ktk mipango ya vikao, anawasiliana na meya kwa maana ya kufix tarehe na mambo madogomadogo kama yapo;

Zaidi Adam kama uliona meya anapwaya au anafanya vivyo isivyo ulipaswa kumshauri meya kwanza nje ya vikao, ndani ya vikao vya chama, kumshitaki ngazi za juu za chama, na kama hupati msaada wowote na hali inazidi kuwa mbaya ndipo umwage kwenye vikao vya wananchi/baraza la madiwani ambalo ni la wazi.

Ni kuulize swali kama meya anapotoshwa na CD tunafanyaje??? maana umeya sio taalum, CD ndo amempelekea meya asaini huku akijua meya anahitaji baraka za baraza, kwani nini cd asipewe onyo kwa makosa hayo??? tumeona hata kwa rais wa nchi, meya ni rais wa h/jiji la mwanza, iweje mtendaji amtegesheeee huoni hila hizo za KICCM CCM??? CD ni mdhoefu sana wa miaka na miaka wa vikao vya madiwani na mamlaka yake meya ni mgeni kabisaaa, dhamana kubwa hasa mambo ya kisheria ya uendeshaji wa jiji ni CD, kama anampotosha meya apigwe chini.

Kuhusu mtendaji wa kata, kwanza sio vema kwa msomi kuchagua mtu wa kufanya nae kazi, huo nao umeonesha udhaifu. pili kama mwanachadema unajua CCM haina watu hata ukibadilisha vipi, sasa unalalamika kuhusu WEO atatoka wapi??? ni mpaka wananchi wapige chini kabisa CCM ndo mambo yanyoke 100% kwa sasa tunalazimika kufanya nao kazi hivyo hivyo tukisubiri uamuzi wa wananchi 2015. au nawewe unataka uletewe WEO mpenzi wako???? nani amekuhakikisha atakayekuja ni mzuri kuliko aliyepo???

Kwenye siasa fitina ni siasa, unapaswa uzishinde na wala sio kutulalamikia kuwa unafanyiwa zengwe, siasa ni zengwe amini usiamini; maana hata ndani ya chama kunawatu wanataka nafasi yako achilia mbali nje ya chama. na ni haki yao, so kuwa smart kushinda fitina za siasa, acha kukurupuka utanasa kwenye mtego; i mean himili mkiki ya siasa na usilalamike kuhusu zengwe, maana hata wewe unafanya mizengwe kwa upande mwingine. Ukiona unaelemewa unapaza sauti, hakuna wa kukuonea huruma pigana na kuwa smart it will work.

Fumagila nimefika maana nilifanya siasa mwaka 2010, nakuunga mkono daraja hilo lijengwe tena kuwa mwehu kabisa; ila usipoteze sheria za mchezo wa siasa; tumia wananchi daraja litajengwa. Na kwa kutumia forum hii nimtake meya ajenge daraja hilo kwa bajeti ya mwaka huu, kama atapuuzia haya.

Mwisho maana sitaki nikujibu hoja zote, kuwa makini hasa na watu unaunda kundi nao, i repeat kuwa makini; ndani yake wamo vijana wa CCM/serikali; nimekuona nao, nawafahamu siku mingi sana na wananifahamu. Nimewaona kwenye kundi lako tena wanachangia sana hoja. Na hapo ndo wasiwasi wa shughuli zako uliponiijia, wale vijana ni smart guys be careful labda kama nawe wewe ni mmoja wao. JUA KUWA NGUVU YA UMMA inatokana na umma wenye nguvu; Watanzania kwa sasa wamejenga umma wenye nguvu.

kula 'like' yangu mzee, hayo ndo nilitaka ni mweleze pia, asifanye papara atumie vikao vya chama na viongoz wa chadema taifa, kabla ya kukurupuka kuileza audience tofaut yake na wenje, meya, CHONDE MSITUHARIBIE CHAMA KWA BIFU ZISIZO NA TIJA.
 
Mtu ambaye ataweza kuivuruga CDM kwanza lazima awe na uwezo wa kuwavuruga watanzania wote (community trust is more powerful than hooliganism). Huyo mtu hayupo hapa duniani labda mbinguni; So be careful when you say somethings to the general public. Kwa hali ilivyo sasa ni point of no return, ukombozi lazima. Ni kama tu hali ilivyokuwa wakati wa uhuru, mzungu hakuamini lakini ndo ilivyotokea, Kama CCM hawaamini wala wasihangaike kula mti shamba na sindano za kuondoa maumivu, wawapigie waingereza Prince Charles, Richard Tanbull, Queen Elizabeth etc. watawapa full mkanda.
 
Chagulani Adam Taarifa yako tumeisoma kwa tafakuri zito hapa jamvini, MODS did well kuziunga hizi thread ili kuweka sawaia majibu yako kama ni afya au kansa kwa chama. Kama mwana jamvi imenihitaji umakini wa hali ya juu kuisoma taarifa yako ambayo imejaa malalamiko mazito na shutuma ambazo pia bado ni hatari sana kwa afya ya chama. Kama ningekuwa katika viatu vyako: 1. Maelezo yako yalikuwa silaha nzuri katika vikao vya chama kwa kuongeza ufanisi katika utendaji wa kiongozi mmoja mmoja kwa masilahi ya Umma na afya ya CDM. 2. Maelezo haya ningemwasilishia mnadhimu wa Chama, Katibu,Naibu Katibu, na Mwenyekiti wa chama kwa hatua madhubuti za utekelezaji katika vikao stahiki vya CDM, hasa baada ya kulega kwa imani yako kwa uongozi wa mkoa. 3. Uchaguzi ni awamu na mchakato, huna haja ya kutaka kushindwa ama kushinda nje ya jukwaa. Ukichafuka katika game itakuchukua muda kujipanga mpaka ueleweke. Kwa nini usijipange ukashindana katika mchakato wa uchaguzi.
4. Kama utetezi huu ni taarifa kwa umma sina shaka hatua ya pili tutakuona pale Star TV tuongee asubuhi Jumapili kwenye siasa au Ijumaa na Yahya, Tafakari hatua zako na upate mashauri ya kina ya kisiasa yatakayoinusuru hali ilivyo kutoka hapa mpaka hitimisho la kadhia hii.
ADIOS
 
Kwanza nimpongeze Diwani wangu na mdogo wangu Adam Chagulani(Tete)kwa Hoja yake yenye mashiko,ukweli nikwamba huyu Meyor ni mzigo na janga ndani ya Chama na Jiji la mwanza hana jipya haiwezekani kabisa Jiji linaloingiza/toa mapato makubwa sana lakini barabara zake tena za katikati ya Jiji mf.Pamba road karibia na keep left karibu na Stanbic barabara ni mbovu sana siku nyingi lakini mayor katulia tu nakuridhika kabisa...je utasema kweli anasimamia vyema utendaji wa Halmashauri ya jiji pamoja na matumizi yake yanayotokana na kodi zetu.Ukweli nikwamba mayor huyu amefail na niwakati muafaka kwa madiwani wa Mwanza kuchukua hatua kabla mambo hayajaharibika zaidi.
 
Leo tulikuwa kwenye mkutano wa hadhara Igoma, mkutano ulioitishwa na diwani Igoma (CHADEMA) Mh. Adam Chagulani kuelezea juu ya mchakato wa kukusanya kura za kutokuwa na imani na meya wa jiji la Mwanza Mh. Manyerere.

Kwa mujibu wa maelezo ya Chagulani juu sababu ya kutokuwa na imani na meya nimegundua kuwa Chagulani hana jipya na anatumiwa sana na CCM. Amezungumza siri nyingi sana za CHADEMA bila aibu mbele umati wa watu waliokuepo kwenye ule mkutano na kila mtu ametoka pale akilalamika na kumlaumu Chagulani. Na amemshutumu sana Mh. Wenje - mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) bila kufuata taratibu za kichama. Kiujumla ni kwamba Chagulani hana jipya, hana ushirikiano na mahusiano mazuri na viongozi wa CHADEMA Mwanza!

Hata asiponyang'anywa kadi ni wazi kuwa 2015 hana chake tena Igoma.

- JACADUOGO (Mwenyekiti wa WANARORYA WOTE popote walipo)!

Mdau hujajibu Hoja ya msingi...kama kuna mgongano ndani ya chama ni kazi ya uongozi wa chama ngazi zinazohusika kuutatua...Hapa hoja nikuhusu Mayor ambae ndiye anaidhinisha matumizi ya jiji katika shughuli mbalimbali je wewe kama mkazi wa Mwanza unaridhika!!Hapo kinachoonekana Chagulani anatimiza wajibu wake yawezekana kabisa madiwani katika vikao vyao wanaazimia Mipango mizuri lakini linapokuja swala lausimamizi mayor anashindwa kusimamia utekelezaji wa hiyo mipango na hapo ndipo madiwani wote wanaonekana ovyo Wananchi wanahuzunika na kulalamika so kwa diwani makini lazima aongee kwa manufaa ya wananchi,yeye binafsi na Chama kwa ujumla.kuhusu swala la chagulani kutokuwa na chake 2015 nadhani umekuwa bias zaidi na ni mawazo yako binafsi si yawakazi wa Igoma mi nikiwa mmojawapo.
 
Wenje (Mbunge) v/s Adam chagulani (Diwani)
Sababu "ukabila + kambi"
"meya wa mwanza hatufai ang'oke na wenje si msukuma hajali maendeleo yetu_Adam"
Adam ni mzushi na mkabila ni zao la Zitto Z Kabwe_ Wenje"
WENJE ANAJENGA KAMBI YA MBOWE, CHAGULANI KAMBI YA ZITTO.


Shibuda (mbunge) v/s John Heche (Mkt BAVICHA)
Sababu "ukanda + kambi”
"Shibuda ni mamluki, hatumuhitaji arudi CCM_Heche"
"heche aniombe radhi na asitumie BAVICHA kwa maslahi yake, ninayajua mengi CHADEMA msinilazimishe niyamwage hadharani_Shibuda"
HECHE ANATAJWA KATIKA WALINZI SHUPAVU WA “UNTOUCHABLE DOMINANCE” KTK CHAMA.


Mbowe v/s Sugu - kuhusu clouds
Sababu "self-interest"
“Clouds wazushi na wanaibeba CCM na wanadhaminiwa na JK _ Joseph Mbilinyi aka Sugu.
“Clouds ni chombo chetu sote, tunaweza kukitumia _ Mbowe.."


Mwenyekiti BAVICHA v/s Makamu Mwenyekiti BAVICHA.`
Sababu “power factor”
“Tamko la Heche ni tamko lake, mimi sikushirikishwa wala hakukuwa na kikao cha kuidhinisha kauli hiyo, ana sababu binafsi na BAVICHA halihusiani nazo _ Makamu Mwenyekiti”
“Tamko la mwenyekiti ni tamko la BARAZA _ Mwenyekiti”


Dr. Slaa V/S Lema
Sababu " Uongo wa Lema"
" Kauli ya lema juu ya Vigogo wa CCM kuhamia chadema si kauli ya Chama ni yake mwenyewe kwa kuwa sisi kama chama hatuna taarifa rasmi juu ya hilo *_ Dr. Slaa ”

My take;
Katika kipindi cha miaka michache hapo nyuma tulishuhudia kasi kubwa ya kukua kwa chama hiki na watanzania walio wengi hasa vijana wakionesha kukikubali na kukipenda. Ni chama ambacho kiliweza kutoa fursa kwa kila mmoja kushiriki shughuli za chama, kuchagua na kugombea. Tuliweza kuona vijana wengi wakipata nafasi kama madiwani na wabunge na hili lilihamasisha wengine kukiamini na kuwatumia vijana hawa kama mifano hai.

Imani imeanza kupotea:
Kulingana na matukio mbalimbali ndani ya chama hasa migongano na mifarakano ambayo imekuwa ikiendelea na kufikia baadhi ya watu kutishiwa ama kufukuzwa kabisa uanachama ktk chama.
Akihojiwa juzi katika radio ya Clouds Mhe. Mbowe alidai kuwa “mifarakano hii si jambo la msingi na mwenye akili hapaswi kujadili hili” kauli hii kutoka kwa mwenyekiti wa Chama imeshtua wengi, kwani mifarakano hiyo ambayo haina msingi wa kuimarisha chama na haina misingi ya kikatiba wala kisera katika chama bali ni matakwa ya watu na hulka binafsi ni vitu vinavyotishia uhai na makuzi ya Chama, hivyo ni vya kujadiliwa tena kwenye kamati ya maadili na kutolewa karipio kali.

Ni nani hasa “UNTOUCHABLE DOMINANCE” katika CHADEMA…?
Ukifuatilia kwa undani mifarakano hii katika Chama inayo sababu zinazoshabihiana sana na mfanano wa hali ya juu, yote kwa pamoja yanatokana na kuwepo kwa kundi hili la “untouchable dominance” ambalo Mbowe anatajwa kuwa ni kinara wake na ndio maana anajaribu kuweka namna ya kutojadiliwa mifarakano hiyo. Tangu kuasisiwa kwake Chadema kumekuwepo na dhana hii ya kuwepo watu rasmi kuandaliwa kwa nafasi Fulani ya juu ya chama hicho. Mnamo mwaka 2004 katika mchakato wa kumpata mgombea urais, alinukuliwa muasisi wa chama hiko Mzee Mtei akieleza kauli inayofafanua hili linaloendelea leo katika Chama, alisema kwa kutumia lugha ya kigeni “.. We can’t give this position to anyone ..”Wenje (Mbunge) v/s Adam chagulani (Diwani)
Sababu "ukabila + kambi"
"meya wa mwanza hatufai ang'oke na wenje si msukuma hajali maendeleo yetu_Adam"
Adam ni mzushi na mkabila ni zao la Zitto Z Kabwe_ Wenje"
WENJE ANAJENGA KAMBI YA MBOWE, CHAGULANI KAMBI YA ZITTO.


Shibuda (mbunge) v/s John Heche (Mkt BAVICHA)
Sababu "ukanda + kambi”
"Shibuda ni mamluki, hatumuhitaji arudi CCM_Heche"
"heche aniombe radhi na asitumie BAVICHA kwa maslahi yake, ninayajua mengi CHADEMA msinilazimishe niyamwage hadharani_Shibuda"
HECHE ANATAJWA KATIKA WALINZI SHUPAVU WA “UNTOUCHABLE DOMINANCE” KTK CHAMA.


Mbowe v/s Sugu - kuhusu clouds
Sababu "self-interest"
“Clouds wazushi na wanaibeba CCM na wanadhaminiwa na JK _ Joseph Mbilinyi aka Sugu.
“Clouds ni chombo chetu sote, tunaweza kukitumia _ Mbowe.."


Mwenyekiti BAVICHA v/s Makamu Mwenyekiti BAVICHA.`
Sababu “power factor”
“Tamko la Heche ni tamko lake, mimi sikushirikishwa wala hakukuwa na kikao cha kuidhinisha kauli hiyo, ana sababu binafsi na BAVICHA halihusiani nazo _ Makamu Mwenyekiti”
“Tamko la mwenyekiti ni tamko la BARAZA _ Mwenyekiti”


Dr. Slaa V/S Lema
Sababu " Uongo wa Lema"
" Kauli ya lema juu ya Vigogo wa CCM kuhamia chadema si kauli ya Chama ni yake mwenyewe kwa kuwa sisi kama chama hatuna taarifa rasmi juu ya hilo *_ Dr. Slaa ”

My take;
Katika kipindi cha miaka michache hapo nyuma tulishuhudia kasi kubwa ya kukua kwa chama hiki na watanzania walio wengi hasa vijana wakionesha kukikubali na kukipenda. Ni chama ambacho kiliweza kutoa fursa kwa kila mmoja kushiriki shughuli za chama, kuchagua na kugombea. Tuliweza kuona vijana wengi wakipata nafasi kama madiwani na wabunge na hili lilihamasisha wengine kukiamini na kuwatumia vijana hawa kama mifano hai.

Imani imeanza kupotea:
Kulingana na matukio mbalimbali ndani ya chama hasa migongano na mifarakano ambayo imekuwa ikiendelea na kufikia baadhi ya watu kutishiwa ama kufukuzwa kabisa uanachama ktk chama.
Akihojiwa juzi katika radio ya Clouds Mhe. Mbowe alidai kuwa “mifarakano hii si jambo la msingi na mwenye akili hapaswi kujadili hili” kauli hii kutoka kwa mwenyekiti wa Chama imeshtua wengi, kwani mifarakano hiyo ambayo haina msingi wa kuimarisha chama na haina misingi ya kikatiba wala kisera katika chama bali ni matakwa ya watu na hulka binafsi ni vitu vinavyotishia uhai na makuzi ya Chama, hivyo ni vya kujadiliwa tena kwenye kamati ya maadili na kutolewa karipio kali.

Ni nani hasa “UNTOUCHABLE DOMINANCE” katika CHADEMA…?
Ukifuatilia kwa undani mifarakano hii katika Chama inayo sababu zinazoshabihiana sana na mfanano wa hali ya juu, yote kwa pamoja yanatokana na kuwepo kwa kundi hili la “untouchable dominance” ambalo Mbowe anatajwa kuwa ni kinara wake na ndio maana anajaribu kuweka namna ya kutojadiliwa mifarakano hiyo. Tangu kuasisiwa kwake Chadema kumekuwepo na dhana hii ya kuwepo watu rasmi kuandaliwa kwa nafasi Fulani ya juu ya chama hicho. Mnamo mwaka 2004 katika mchakato wa kumpata mgombea urais, alinukuliwa muasisi wa chama hiko Mzee Mtei akieleza kauli inayofafanua hili linaloendelea leo katika Chama, alisema kwa kutumia lugha ya kigeni “.. We can’t give this position to anyone ..”
 
the horse

Acha kuingiza mambo ya majungu. Tunasherehekea ushindi wa Mnyika kuwabamiza vibaya magamba mafisadi. Hayo unayoyaomba hayawezi kamwe kuzuia wimbi la mabadiliko likiongozwa na CDM. CCM na vigogo wake mtabakia kutapatapa tu.
 
Last edited by a moderator:
KAWAULIZE MAGAMBA KWANZA MUKAMA Vs LOWASA AU MAKAMBA SNR Vs NAPE KIKWETE vS PINDA KUHUSU JAIRO NA SERIKARI YOTE YA CCM HUKU M4C HATUBABAIKI KANYWE KAHAWA MJOMBA KUMEKUCHA:israel:
 
Kwanza hiyo mifarakano ndani ya CDM unayozungumzia ni fraction tu, yaani ni kama moja chini ya elfu (1/1000) ya zile zilizomo ndani ya CCM, ukiachilia mbali tuhuma lukuki za ufisadi dhidi ya vigogo wao.

Nakubaliana na aliyesema hapo juu kwamba hili wimbi la CDM halizuiliki kwa vifitina na vichonganishi vyovyote kwani Watz wamesha sema YES! CCM iko katika reverse gear -- au tuseme katika FREE FALL. Sorry, your time has passed!!!
 
Sehemu nasema mtoa mada ni TUNTEMEKE ni kauli ya slaa dhidi ya lema.refer..mwananchi la juzi dr haku2mia kauli kali wala kumuignore lema.'DR alisema kuwa hayupo kuzungumzia kauli ya lema ama yoyote,wamwache ajadili maendeleo.MTOA MADA NI MZANDIKI.
 
Nawashangaa watu wa aina ya 'the horse' wanaoamini kwamba CDM lazima isambaratike kama vile NCCR au CUF. Kwa taarifa ya watu hawa CDM ni kitu kingine kabisa, kina viongozi na Wabunge makini, wasomi nk.

Watu kama akina Shibuda hawatateresha chama ambacho Watanzania wamekikubali, kwani ukilinganisha CCM na CDM, CDM ndiyo mkombozi wao kwani magamba wameshindwa kuboresha maisha yao.

Hata kauli za kusema ati CDM nao wakishika nchi watashindwa tu kama CCM tu hazina ushahidi wowote, lakini ushahidi wa CCM kushindwa tunao.
 
the horse

Moja hakuna chama kwa sasa chenye migogoro kama magamba, na kwa vyovyote vile hauwezi kufananisha na kinachoendelea CDM, pili kimsingi hakuna mgogoro CDM zaidi ya magamba kutaka kuaminisha umma kuna mgogoro, kwa kutumia vipandikizi vyao, kama akina Shibuda, tatu hoja hii inaendana na ule usemi wa mfa maji haachi kutapatapa, nne CDM wanaendelea kujengwa na kuwa maarufu na jinsi ambavyo magamba hawalali na kuitaja CDM mara nyingi kuliko chama chao.

CDM ni chama makini na lazima kiongozwe na watu makini. Aidha nui lazima hao wenye uchu wa madaraka wajuwe CDM imefika hapo ilipo kwa gharama na hivyo waliogharamia lazima wakilinde kwa nguvu zote, hivyo hakuna suala la untachable hapa, hizo ni porpaganda chafu ambazo zinzaweza kufanya kazi kwa wale wanaoamini utopian kind of thinking bila kujishughulisha kuona ukweli.
 
Last edited by a moderator:
Ugonjwa ulioanza kuwaingia watz ni mbaya sana sasahivi!!

Yaani kila kitu kinachokea mnataka kuaminisha watu kuwa kuna hujuma, udini au ukabila...

Hii ni akili mbovu sana...!

Hatuwezi kuendelea katika kuangalia mambo kwa mtazamo huo...
 
Nafikiri mtoa hoja angesema kuwa CDM kuna Changamoto badala ya migogoro,na mara zote katika maisha ya binadamu changamoto ni moja ya sababu za kuwepo kwetu hapa Duniani.
 
Back
Top Bottom