NdasheneMbandu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 940
- 308
Kwa wale waliofuatilia hotuba (siyo mazungumzo) ya Kikwete kwa anaowaita wazee wa Dar bila shaka watakubaliana nami kuwa madaktari wamedharirishwa mbele ya jamii na kuonekana kuwa ni watoto wadogo wasiotumia busara. Kwa ujumla, rais ametumia fursa hiyo kuonyesha kuwa yeye ndiye mshindi na madaktari hata iweje hawawezi kupambana na serikali.
Miongoni mwa kauli iliyonisononesha ni pale aliposema kwamba wao kama serikali waliamua kutulia tu. Eti nao wangekataa kuongea na madaktari hali ingekuwaje? Inavyoonekana huyu MTAWALA bado hajatambua vema dhamana aliyonayo kwa wananchi katika kulinda maisha yao. Yeye anadhani kwa kugoma kuongea na madaktari angekuwa amewakomoa lakini hajui kwamba kwa uamuzi huo, angekuwa anawaumiza waliomweka pale magogoni. Ama kweli sasa nimeamini bila busara huwezi kuitwa kiongozi.
Poleni madaktari kwa kudharirishwa kiasi hicho. Tulidhani movement yenu ingeiamusha serikali usingizini kumbe ndiyo imeiongezea blanketi lenye usingizi mnono zaidi.
Miongoni mwa kauli iliyonisononesha ni pale aliposema kwamba wao kama serikali waliamua kutulia tu. Eti nao wangekataa kuongea na madaktari hali ingekuwaje? Inavyoonekana huyu MTAWALA bado hajatambua vema dhamana aliyonayo kwa wananchi katika kulinda maisha yao. Yeye anadhani kwa kugoma kuongea na madaktari angekuwa amewakomoa lakini hajui kwamba kwa uamuzi huo, angekuwa anawaumiza waliomweka pale magogoni. Ama kweli sasa nimeamini bila busara huwezi kuitwa kiongozi.
Poleni madaktari kwa kudharirishwa kiasi hicho. Tulidhani movement yenu ingeiamusha serikali usingizini kumbe ndiyo imeiongezea blanketi lenye usingizi mnono zaidi.