Ole Shider
Member
- Oct 17, 2014
- 16
- 15
Salaam;
Katika Siasa zetu hapa Nchi hasa nikivilenga Vyama hasimu vya CCM na CHADEMA kumekuwako na namna tofauti tofauti kati yao katika kufanya siasa zao Nchi na na kufikisha ujumbe wao kwa Wananchi.
CHADEMA wamekuwa muda mwingi hasa nyakati za kampeini wakitumia CHOPPER wakiamini ndiyo njoa sahihi kwao. Jambo ambalo hata mimi binafsi.niliona hali tija hasa.ukizingatia gharama zinazotumika na taabu wanazopata Wananchi hasa katika Majimbo wanayoyaongoza wao.
Kwa upande mwingine CCM (Chama Tawala) wao wamekuwa wakijinasibu kama jeshi la ardhini lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa Wananchi wote wanafikiwa na kuelezwa yale yanayofaa. Jambo ambalo mtu yeyote anaweza kuelewa hasa ukirudisha kumbukumbu nyuma toka enzi za Mwalimu katika harakati zake za ukombozi.
Mwaka jana katika chaguzi kuna usemi ulivuma sana wa CHOPPER 3 Kata 3 ikimaanisha kuwa CHADEMA walirusha Chopper 3 na kuambulia Kata 3 ilihali wenzao wa CCM Wakipata zaidi ya Kata 26 japo hawakurusha Chopper yeyote vivyo hivyo kwa Majimbo mawili ya Kalenga na Chalinze.
Lakini binafsi na kwa namna ya kushangaza sana na kushtua walio wengi nimestaajabishwa kuona yale yaliyokuwa yakipingwa na wanaCCM dhidi ya wenzao nao pia CCM wameanza kuelekea na kufanya yale yale kwa njia ile ile iliyokuwa ikifanywa na CHADEMA. Ndiyo maana imefikia mahali nikakubali ule usemi usemao ukistaajabu ya CHADEMA utayaona ya CCM......
Swala hili limenipelekea nije na maswali yafuatayo kwa wanaCCM ili mimi na wengine tuweze kujiridhisha na yanayoendelea;
1. Je mtakuwa na majibu yepi kuntu ya kuwaeleza Watanzania pindi mtakapoulizwa kwa nini mlikuwa mnawanyooshea wenzenu vidole nanyi mmeamua kuwaiga??
2. Je mkiwa Chama tawala na mnapoyatazama na kufahamu kwa moyo wa dhati taabu wanazopitia watanzani mathalan madawa hakuna, changamoto za maabara na kadhalika hivi kweli mnastahili kufanya hayo mnayoyafanya??
3. Binafsi katika watu ambao labda ningependekeza atumie CHOPPER labda ni Katibu wenu Mkuu mzee Kinana na nyote mmeona kazi anayofanya ila hakuwahi fanya hivyo na naamini hajawahi kufikiri kufanya hivyo yeye hutumia usafiri anaoukuta huko aendako. Na nadhani hufanya hivyo ili kuwathibitishia Watanzania kuwa CCM nayo inataabika na kuomboleza pamoja nao ktk kila taabu wanazopitia. Je ni kwamba ninyi mmempuuza ama mmeamua kujikweza ili kuonekana ni wanaCCM wenye upeo mkubwa kuliko wenzenu wote?
4. Mtu wa pili pia ambaye ningedhani angestahili CHOPPER labda ni Raisi wa Taifa hili wakatio akikagua miradi ya maendeleo ila ameendelea kuwa muungwana sana na kutotaka kuudharau na kuupuza utu wa Watanzania amekuwa akisafiri kwa barabara ambazo amezisimamia yeye mwenyewe katika utawala wake na hili husadia hata kuwaeleza Watanznaia manake umejionea mwenyewe.. Sasa ninyi wanaCCM wengine wa CHOPPER huko angani mtanataka muwaambie Watanzania mnatekeleza Ilani gani? Ama ni Ilani ya UN ya kukwepa Ebola??
5. Nimepata kusikia kwamba wenzenu CHADEMA wakati mwingine hifanya hivyo ili angalau kupata umati wa watu kule wasiko kubalika hasa wale watakaokuna kushangaa CHOPPER.. Na ninyi mtueleze leo mnatumia Chopper ili kukusanya watu??
6. Moja ya falsafa ya Mwenyekiti wenu wa CCM ni maisha bora kwa kila Mtanzania. Sasa hamuoni hakutakuwa na maisha bora kwa kila Mtanzania hasa kwa kuwasumbua wanafunzi madarasani na makelele ya Chopper. Na ktk hili lazma mtazame na Polisi au jeshi vifaa kama Chopper hutumika panapo na shughuli maalum ili kutowasumbua Watanzania......
Ni hayo machache tu kwa leo mimi binafsi na Watanzania wengine ama wanaowaamini ama wenye kutaka kuwaamini na kuwa sehemu yenu wangependa kujua... Ili nasi tuweze kujiridhisha je mnatenda mnayo yaamini ama mnaamini wanayotenda wenzenu??
Katika Siasa zetu hapa Nchi hasa nikivilenga Vyama hasimu vya CCM na CHADEMA kumekuwako na namna tofauti tofauti kati yao katika kufanya siasa zao Nchi na na kufikisha ujumbe wao kwa Wananchi.
CHADEMA wamekuwa muda mwingi hasa nyakati za kampeini wakitumia CHOPPER wakiamini ndiyo njoa sahihi kwao. Jambo ambalo hata mimi binafsi.niliona hali tija hasa.ukizingatia gharama zinazotumika na taabu wanazopata Wananchi hasa katika Majimbo wanayoyaongoza wao.
Kwa upande mwingine CCM (Chama Tawala) wao wamekuwa wakijinasibu kama jeshi la ardhini lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa Wananchi wote wanafikiwa na kuelezwa yale yanayofaa. Jambo ambalo mtu yeyote anaweza kuelewa hasa ukirudisha kumbukumbu nyuma toka enzi za Mwalimu katika harakati zake za ukombozi.
Mwaka jana katika chaguzi kuna usemi ulivuma sana wa CHOPPER 3 Kata 3 ikimaanisha kuwa CHADEMA walirusha Chopper 3 na kuambulia Kata 3 ilihali wenzao wa CCM Wakipata zaidi ya Kata 26 japo hawakurusha Chopper yeyote vivyo hivyo kwa Majimbo mawili ya Kalenga na Chalinze.
Lakini binafsi na kwa namna ya kushangaza sana na kushtua walio wengi nimestaajabishwa kuona yale yaliyokuwa yakipingwa na wanaCCM dhidi ya wenzao nao pia CCM wameanza kuelekea na kufanya yale yale kwa njia ile ile iliyokuwa ikifanywa na CHADEMA. Ndiyo maana imefikia mahali nikakubali ule usemi usemao ukistaajabu ya CHADEMA utayaona ya CCM......
Swala hili limenipelekea nije na maswali yafuatayo kwa wanaCCM ili mimi na wengine tuweze kujiridhisha na yanayoendelea;
1. Je mtakuwa na majibu yepi kuntu ya kuwaeleza Watanzania pindi mtakapoulizwa kwa nini mlikuwa mnawanyooshea wenzenu vidole nanyi mmeamua kuwaiga??
2. Je mkiwa Chama tawala na mnapoyatazama na kufahamu kwa moyo wa dhati taabu wanazopitia watanzani mathalan madawa hakuna, changamoto za maabara na kadhalika hivi kweli mnastahili kufanya hayo mnayoyafanya??
3. Binafsi katika watu ambao labda ningependekeza atumie CHOPPER labda ni Katibu wenu Mkuu mzee Kinana na nyote mmeona kazi anayofanya ila hakuwahi fanya hivyo na naamini hajawahi kufikiri kufanya hivyo yeye hutumia usafiri anaoukuta huko aendako. Na nadhani hufanya hivyo ili kuwathibitishia Watanzania kuwa CCM nayo inataabika na kuomboleza pamoja nao ktk kila taabu wanazopitia. Je ni kwamba ninyi mmempuuza ama mmeamua kujikweza ili kuonekana ni wanaCCM wenye upeo mkubwa kuliko wenzenu wote?
4. Mtu wa pili pia ambaye ningedhani angestahili CHOPPER labda ni Raisi wa Taifa hili wakatio akikagua miradi ya maendeleo ila ameendelea kuwa muungwana sana na kutotaka kuudharau na kuupuza utu wa Watanzania amekuwa akisafiri kwa barabara ambazo amezisimamia yeye mwenyewe katika utawala wake na hili husadia hata kuwaeleza Watanznaia manake umejionea mwenyewe.. Sasa ninyi wanaCCM wengine wa CHOPPER huko angani mtanataka muwaambie Watanzania mnatekeleza Ilani gani? Ama ni Ilani ya UN ya kukwepa Ebola??
5. Nimepata kusikia kwamba wenzenu CHADEMA wakati mwingine hifanya hivyo ili angalau kupata umati wa watu kule wasiko kubalika hasa wale watakaokuna kushangaa CHOPPER.. Na ninyi mtueleze leo mnatumia Chopper ili kukusanya watu??
6. Moja ya falsafa ya Mwenyekiti wenu wa CCM ni maisha bora kwa kila Mtanzania. Sasa hamuoni hakutakuwa na maisha bora kwa kila Mtanzania hasa kwa kuwasumbua wanafunzi madarasani na makelele ya Chopper. Na ktk hili lazma mtazame na Polisi au jeshi vifaa kama Chopper hutumika panapo na shughuli maalum ili kutowasumbua Watanzania......
Ni hayo machache tu kwa leo mimi binafsi na Watanzania wengine ama wanaowaamini ama wenye kutaka kuwaamini na kuwa sehemu yenu wangependa kujua... Ili nasi tuweze kujiridhisha je mnatenda mnayo yaamini ama mnaamini wanayotenda wenzenu??